WANAFUNZI WAASWA KUZINGATIA NIDHAMU SHULENI.

Juma la wadau wa Elimu Mkoa wa Dodoma limetamatika Kwa viongozi mbalimbali wa Mkoa wa Dodoma kuzungumza na kushiriki Chakula Cha Mchana na wanafunzi wa Shule za kidato Cha Sita za Mkoa huo. Kwa nyakati tofauti akiwa katika shule ya Sekondari ya wavulana Kongwa na Shule ya wasichana kibaigwa amewaasa wanafunzi hao wa kidato Cha sita kuendelea kudumisha nidhamu hususani katika kipindi hiki wanachojiandaa na mitihani Yao na kuachana na marafiki wasiofaa ambao watawasababishia matokeo yatakayogharimu maisha ya ndoto zao. "Tunataka A zenye nidhamu, hapa Kuna wenzenu wamechafua jina la Shule na nyie mliopo hapa tunategemea nyie mtabadilisha sura hii ambayo sio njema Kwa Mkoa, acheni tabia ya kufata mkumbo Kwa kushawishiana mambo yasiyofaa kwasababu Kila mtu ana ndoto zake na Kila moja atarudi nyumbani kwao kivyake na usipokuwa makini utaharibu maisha yako Kwa mikono yako mwenyewe kwasababu tuu ya ushawishi usiofaa kutoka Kwa marafiki zenu. "Lazima muamue kuachana na baadhi ya mamb...