VIJANA WA SKAUTI WATAKIWA KUSIMAMIA MAADILI KATIKA MAENEO YAO
Ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya juma la Elimu Mkoa wa Dodoma Leo Machi 21,2024 Afisa Vijana kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Bw.Tumsifu Mwasamale amefunga mafunzo ya wahitimu 30 wa Skauti kutoka katika Halmashauri zote za Mkoa huo ikiwa ni moja ya mkakati wa Mkoa wa kuendeleza mafunzo hayo katika hafla iliyofanyika katika ukumbi wa chuo cha Don Bosco Jijini Dodoma.
Akizungumza na wahitimu hao Bw. Mwasamale amewataka kuhakikisha wanakuwa chachu kwa wengine katika Halmashauri zao kwa kuonesha weledi waliojifunza ili kupunguza mmomonyoko wa maadili miongoni mwao.
Kilele cha juma la Elimu lililoanza tarehe 18 Machi, 2024 kinatarajiwa kutamatika tarehe 25 Machi,2024 ambapo kauli mbiu ni "Uwajibikaji wangu,ndio Msingi wa kuinua ubora wa Elimu na Ufalu Dodoma".
Comments
Post a Comment