Posts

Showing posts from April, 2024

DCT NA NEEMA YA MILLIONI 32.8 MWITIKILA-BAHI

Image
Vifaa vya Shule vyenye thamani ya Tsh.Millioni 32.8 vimekabidhiwa katika Shule za Msingi Mwitikira, Lupeta Mwitikira B na Shule ya Sekondari Mwitikira kwa ufadhili wa Kanisa la St. Pauls Richmond kutoka Marekani kwa kushirikiana na kanisa la Anglican Dayosisi ya Central Tanganyika (DCT), ambapo makabidhiano hayo yamefanyika April 17, 2024 katika viwanja vya kanisa la Anglican Parish ya Mwitikila Wilayani Bahi. Vifaa hivyo ni madawati 290, meza 13, Viti 113  na Mashine ya kuchapia na kutolea kopi (printer machine) vimekabidhiwa na Askofu wa DCT Dickson Daud Chilongani kwa kaimu Mkuu wa Mkoa wa Dodoma  Mhe. Mayeka S. Mayeka ambaye amewakabidhi uongozi wa Halmashauri ya Bahi na Uongozi wa Shule hizo. Akizungumza katika Hafla hiyo Mhe.Mayeka amewataka wakazi wa kata ya Mwitikira kuacha tabia ya kuwaachisha Watoto wao shule na kuwapeleka katika majiji mbalimbali kwa lengo la kufanya kazi za ndani zisizo na maslahi katika Maisha ya Watoto hao. “Kuna mawakala wanaobeba Watoto vijijin...
Image
Wanawake na Samia Mkoa wa Dodoma Kwa kushirikiana na Shirika la Madini Tanzania (STAMICO) wameandaa Iftar iliyowajumuisha watoto wenye Mahitaji maalum, walemavu, wazee na wajane iliyofanyika Leo April 7 katika bwalo la Shule ya Sekondari Dodoma. Mkuu wa Mkoa  wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule ameshiriki hafla hiyo ambapo amewapongeza wanawake hao kwa kuikumbuka jamii inayowazunguka hususani katika kipindi hiki cha Mwezi mtukufu wa Ramadhan. Aidha Mhe. Senyamule amewataka wajane hao kuchangamkia fursa mbalimbali zinazotelewa na serikali kwani serikali inatambua na kuthamini uwepo wao ikiwemo kuchukua mikopo  inayotolewa na Serikali kupitia Halmashauri zao na kufanya biashara ambazo zitawasaidia kukidhi mahitaji yao. Hata hivyo Senyamule ametumia fursa hiyo kutoa zawadi mbalimbali kwa watoto wahitaji, wajane na wazee waliofika kushiriki Iftar hiyo. Reply Forward Add reaction  
Image
 Ziara ya kikazi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule, imeendelea Wilayani Kondoa April 3/ 2024 ambapo amefanya ukaguzi wa miradi mbalimbali inayotekelezwa wilayani humo ikiwemo Ujenzi wa Wodi ya wazazi, jengo la Mochwari na jengo la upasuaji katika hospitali ya wilaya ya kondoa. Aidha amekagua ujenzi wa vyumba vya madarasa katika shule ya sekondari  ya wasichana Kondoa pamoja ukaguzi wa nyumba ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya kondoa mji ambapo ujenzi unaendelea na unatarajia kukamilika muda wowote kwani umefika hatua za umaliziaji ( Finishing). Hatahivyo Mhe. Senyamule ameendelea kuwahimiza watumishi wa sekta ya afya kuendelea kutunza mazingira yanayozunguka katika vituo vyao ili kuendelea kuweka mazingira safi na ya kuvutia siku zote ikiwemo kupanda miti kwa mpangilio unaofaa.