Posts

Showing posts from September, 2024

VIONGOZI SOKO LA MACHINGA DODOMA WASIMAMISHWA KUPISHA UCHUNGUZI

Image
Viongozi wa soko la wazi la Machinga lililopo Mtaa wa Kitenge, Kata ya Majengo katika Jiji la Dodoma, wamesimamishwa uongozi kupisha uchunguzi kutokana na kudaiwa kutenda makosa ya kiuongozi na kijinai kwa wafanyabiashara wa soko hilo. Agizo hilo limetolewa Septemba 13, 2024 na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary S. Senyamule alipokua akitatua kero za wafanyabiashara wa soko hilo katika Mkutano wa hadhara aliouitisha ndani ya soko hilo. Wafanyabiashara hao, walipata fursa ya kutoa kero zao mbele ya Kiongozi huyo lakini kubwa zaidi ni lawama walizotupiwa viongozi wa soko ambao ni Mwenyekiti na Meneja kwa kuuza vizumba kinyume na taratibu pia kughushi barua za Mkurungenzi wa Jiji pamoja na vitambulisho vya wajasiriamali. "Zipo tuhuma za kiuongozi lakini nyingine za jinai kama kufoji vitambulisho na barua. Hatuna uhakika mpaka uchunguzi ufanyike. Wakati uchunguzi unafanyika Mwenyekiti na Meneja wasimamishwe kwani wameonekana katika sehemu kubwa ni sehemu ya tatizo." Ameagiza Mh...

RC ARIDHISHWA UTEKELEZWAJI WA MIRADI, ALIPONGEZA JIJI LA DODOMA.

 S eptemba 11, 2024 Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule ametembelea na kukagua miradi ya Elimu na Afya inayotekelezwa katika kata nne (4) ambazo ni kata ya Zuzu, Nala, Kikuyu kaskazini na Tambukareli zinazopatikana katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Akizungumza baada ya kumalizika kwa ziara hiyo RC Senyamule amewataka   uongozi wa Jiji la Dodoma kukamilisha miradi kwa wakati hususan miradi iliyotakiwa kukamilika katika kipindi cha mwaka wa fedha uliomalizika wa 2023/ 24 na kuwataka kukamilisha miradi hiyo Ifikapo Mwishoni mwa mwaka huu na wananchi waanze kupatiwa huduma. ‘’Mnapopata fedha za miradi mnatakiwa mzitoe mapema ili kuikamilisha miradi kwa wakati kwasababu kumekuwa na uchelewaji wa kutekeleza miradi kunakotokana na mwaka wa fedha kumalizika, hivyo nitoe wito kwa Jiji kuhakikisha miradi yote inakamilika na inaanza kutoa huduma kwa wananchi kwa muda uliokusudiwa. Awali akizungumza katika mradi wa ujenzi wa kituo cha Afya Zuzu kinachotarajiwa kukamil...

DODOMA YAWEKA MIKAKATI KUMALIZA VIFO VITOKANAVYO NA UZAZI.

Mkoa  wa Dodoma umejipanga  kufikia mwishoni mwa mwaka huu kuwa na  vituo 60 vinavyotoa huduma za dharura za upasuaji kwa kina mama wajawazito wenye viashiria vya hatari. Hayo yamebainishwa leo Septemba 09, 2024 na Mkuu wa Wilaya ya Kongwa Mhe. Simon Mayeka, wakati wa mkutano wa tathimini ya utekelezaji wa mradi wa uboreshaji huduma za  afya ya uzazi na mtoto chini ya ufadhili wa Shirika la KOFIH unaotekelezwa katika halmashauri ya Wilaya ya Kongwa na Mpwapwa. Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule, amesema Mkoa wa Dodoma una jumla ya vituo vya afya 546 vikijumuisha hospitali 17, vituo vya afya 68, zahanati  431 na kliniki 30. Aidha vituo 416 sawa na asilimia 76 vinatoa huduma za afya  ya uzazi na mtoto na vituo 48 sawa na asilimia 56 kati ya vituo 85 vinatoa huduma za dharura  za upasuaji kwa kina mama wajawazito. “Mkoa umejipanga kuongeza vituo hivyo ili kufikia vituo 60 ifikapo Desemba 2024, huduma za dharura za upas...