Posts

Showing posts from May, 2022

OFISI YA MKUU WA MKOA DODOMA YAFANYA MKUTANO WA KUMSHUKURU NA KUMPONGEZA RAIS,MHE. SAMIA SULUHU HASSAN

Image
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma leo imefanya mkutano wenye lengo la kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, Mkutano huo umefanyika katika ukumbi wa PSSSF ambapo watumishi wa sekta mbalimbali za Serikali katika mkoa wa Dodoma walihudhuria.  Akifungua mkutano huo, Katibu Tawala Mkoa Dkt Fatma Mganga, alianza kwa kupongeza jitihada za Rais Samia suluhu Hassan hasa kwenye ongezeko la mishahara pamoja na posho. Dkt. Mganga amewataarifu wajumbe wa mkutano huo kuwa Mkoa wa Dodoma una watumishi zaidi ya Elfu 20, hivyo ongezeko hilo litaleta afueni kwa kugusa familia zaidi ya hizo.  Katika kutoa pongezi na shukrani hizo, watumishi wa idara mbalimbali wakiwakilishwa na wasemaji wao,ambapo wengi wao wamempongeza Rais kwa kuwajali na kuwakumbuka katika ongezeko hilo kwani litakua chachu ya kuongeza ari ya kufanya kazi kwa bidii kwa lengo la kuinua uchumi wa familia zao pamoja na Taifa kwa ujumla.  Akizungumza kwa niaba ya Walimu, mwenyekiti wa C...

RC MTAKA AKUTANA NA KUFANYA KIKAO NA WAENDESHA BODABODA NA BAJAJI JIJINI DODOMA

Image
  Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Anthony Mtaka, hivi karibuni kwenye ukumbi wa Cavillum jijini Dodoma, alikutana na kuongea na madereva wa Pikipiki maarufu kama Bodaboda pamoja na Bajaji kuzungumzia utendaji kazi wao, hali ya ulinzi na usalama kutokana na matukio ya kihalifu yanayofanywa na baadhi yao pamoja na changamoto wanazokumbana nazo wakati wa usafirishaji wa abiria.  Katika kikao hicho, Mhe. Mtaka aliongozana na kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa, wakuu wa idara zinazohusika na usafirishaji kama vile Wakala wa barabara za vijijini TARURA, Mamlaka inayoshughulikia usafirishaji wa nchi kavu LATRA , Mkuu wa kitengo cha Usalama barabarani pamoja na wadau wanaoisaidia kuiwezesha sekta ya usafirishaji kifedha ambao ni Benki ya NMB pamoja na shirika la Bima la SANLAM.  Baadhi ya madereva wa vyombo hivyo, walitoa malalamiko yao mbele ya Mkuu wa Mkoa kwamba wananyanyaswa na vyombo vinavyohusika na usalama barabarani kwa kulipishwa faini zisizo na risiti, kubabimbikiwa makosa...

Mkoa Wa Dodoma Kuwatambua na Kutatua Changamoto za Wanafunzi Waliochaguliwa Kujiunga Kidato Cha Tano , 2022- Mhe. Mtaka

Image
K auli hiyo imetolewa leo na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Mhe Anthony Mtaka wakati akiongea na vyombo vya habari,kumtambulisha Mwanafunzi Mariam Leonard Mchilo na kuwashukuru wadau mbalimbali ambao wamejitolea kumsaidia mwanafunzi huyo. Wadau hao ni pamoja na Spika Mstaafu na Mbunge wa Kongwa Mhe.Job Ndugai ambaye  anamhfadhi Mwanafunzi Mariam hadi hapo atakapokamilisha taratibu za kujiunga na kidato cha tano mkatika shule ya sekondari Songea, shule ambayo amepangiwa. Aidha Mhe Mtaka amemshukuru aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa Maabara ya Taifa Bw. Nyambura Moremi, Mwanza University pamoja na Equity Bank ambao kwa njia moja au nyingine wamechangia ada za masomo na gharama zingine za Mwanafunzi Mariam.  Akizungumzia Ufadhili wao kwa mwanafunzi Mariam , Makamu Mkuu wa Chuo/ 'Vice Chancellor' wa Mwanza University Prof. Florah Fabian ameeleza kuwa, Mwanza University ni chuo kikuu kipya ambacho kitakuwa kikiendesha elimu ya masomo ya uuguzi na udaktari. Pamoja na elimu hizo kila mwaka...