Posts

Showing posts from July, 2022

Kwa Pamoja Tunaweza _ Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Dodoma

Image
Katika kujenga Umoja, ushirikiano  na kujengeana uwezo katika Masuala mbalimbali ya kiofisi na kijamii. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Dodoma iliamua kuja na utaratibu wa Chakula cha Pamoja kila jumatano ya mwisho wa mwezi. Katika Jumatano hiyo Taasisi mbalimbali hukaribishwa kuja kutoa mada na kuwaeleimisha wafanyakazi wa mkoa kuhusu masuala mbalimbali.Sanjari na hayo chakula hicho cha mchana hutumika kuwapongea wafanyakazi wote waliozaliwa katika mwezi husika .  Katika Chakula cha mchana kilichofanyika 27/7/2022 Bpodi ya maziw ilikaribishwa kutoa mada na kuwahamasisha Watumishi kuhusu matumizi bora ya maziwa kuliko kimiminika kingine ,kwani kila binadamu anatakaiwa kunywa nagalau lita 200 mza maziwa kwa mwaka. Mwisho   Watumishi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa waliozaliwa mwezi wa Julai wakifungua Champagne Watumishi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Wa  Dodoma  waliozaliwa mwezi Julai Wakikata  keti kwa pamoja  Watumishi wa Bodi ya Maziwa wakionyesha bidhaa zao

"Machinga Complex -Dodoma. Mfano wa Kuigwa "- Mhe. Seleman Jafo

Image
  Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais,Muungano na Mazingira Mhe. Selemani Said Jafo (Mb) ameyasema hayo leo wakati wa ziara yake ya kutembelea   Soko la Machinga Complex lililopo jijini Dodoma. Mhe. Jafo amesema kuwa pamoja na kutembelea soko nimekuja kuona kama mambo ya mazingira yamezingatiwa katika   Ujenzi wa Soko hili la Machinga Complex. “Hii ni pamoja na kuangalia mambo makubwa matatu, kuangalia matumizi ya nishati,maana nimesikia kutakuwa na wamachinga ambao watakuwa wanapika vyakula   hivyo nimekuja kuona kama watatumia nshati ya aina gani kama kuni au mkaa   au gesi, pia   nimekuja kuona mfumo wa maji safi na maji taka, pamoja na mfumo wa kuhifadhi maji ya mvua.   Aidha nimekuja kuona jinsi ambavyo mtahifadhi taka maana Wizara yangu inashughulika na mambo yote hayo “ Amesema Mhe. Jafo. Akielezea hali ya ujenzi wa Soko hilo ambao umezingatia mazingira kwa kiasi kikubwa,   Kaimu Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma, Bw.Dickson Kimaro   amemshu...

"Sanaa na Utamaduni ni Ajira"- RC MTAKA

Image
  Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Anthony   Mtaka ameeleza kuwa Sanaa, Utamaduni   na michezo ni fani zinazotoa ajira kwa vijana na kuchangia kwa kiasi kikubwa katika uchumi wa nchi. Mhe. Mtaka amesema hayo Julai 23, 2022 Chamwino Dodoma wakati akifungua Tamasha la 13 la Muziki wa Cigogo linaloazimishwa kila mwaka. "Nawaomba wazazi na walezi kuwaruhusu   vijana wenu   kushiriki shughuli za   Sanaa , utamaduni na michezo ni mojawapo ya ajira ambazo   zinachangia   katika pato la taifa"amesema Mhe. Mtaka Aidha Mhe. Mtaka ametoa wito   kwa waandaaji wa   tamasha la Cigogo kuliongezea thamani tamasha hilo ili lifikie kiwango cha kitaifa na kimataifa kama lilivyo   tamasha la Sauti za Busara la Zanzibar. Vilevile Mhe. Mtaka ametumia nafasi hiyo,kumpongeza Mwanzilishi wa Tamasha hilo Dkt. Kedmon Mapana kwa kuaminiwa na Mhe. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuteuliwa kuwa   Katibu Mtendaji wa Baraza la S...