Posts

Showing posts from August, 2022

Mradi wa Bwawa la maji Membe- Chamwino, Utakaogharimu Tsh. 11.965 Bln Kuanza hivi Karibuni

Image
  Akikabidhi mradi wa ujenzi wa bwawa la maji  la Membe, mradi utakaogharimu kiasi cha Tsh. 11.965 bln, Mkuu wa Wilaya ya Chamwino Mhe.Gift Msuya amesema, mara bwawa hili litakapokamilika litawezasha umwagiliaji wa hekari 8000.Bwawa litakuwa na maji kwa mwaka mzima. Mhe.Msuya, ametoa shukrani za dhati  kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan Kwa kuongeza bajeti ya Wizara ya Kilimo. Aidha Mhe. Msuya amemshukuru Waziri wa Kilimo, Mhe. Hussein Bashe kwa kuridhia fedha hizi zije kwenye mradi wa bwawa la maji la Membe.  Mradi huu ulisanifiwa mwaka 2016 lakini kwa kipindi chote chote hicho haukutekelezeka hadi mwaka huu ambapo utaanza 01/9/2022 na kukamilika 01/9/2023.Miradi huu ukikamilika  Wilaya ya Chamwino tutakuwa na chakula cha kutosha.  Kutakuwa na  utaratibu maalum  wa kuingia kwenye bwana nalo bwawa hili litatengeneza ajira kwa vijana.Ombi langu kwa Wanamembe ni kutoa ushirikiano katika mradi huu kwani ni wenu. Ombi...

MIRADI 6 HALMASHAURI YA WILAYA BAHI YAPITISHWA NA MWENGE WA UHURU 2022

Image
Ikiwa ni siku ya kwanza tangu Mwenge wa Uhuru uingie na kuangaza Mkoani Dodoma, Halmashauri ya Wilaya ya Bahi imekuwa Halmasuri ya kwanza  kuangaziwa na Mwenge wa uhuru. Akizungumza wakati wa kuwakaribisha viongozi wa mwenge wa uhuru mwaka 2022 , Mkuu wa Wilaya ya Bahi Mhe. Mwanahamisi Munkunda amesema kuwa Wilaya ya Bahi ina miradi sita ambayo itatembelewa na Mwenge wa Uhuru. Mhe.Munkunda ameitaja miradi hiyo kuwa mradi wa uogeshaji wa Mifugo.Zaidi ya 60% za makusanyo ya Halmashauri ya Bahi hutokana na Mifugo. Mradi wa Shule shikizi Mpamantwa, mradi huu umesaidia kuwapunguzia wanafunzi umbali wa kutembea mbali mkubwa kwenye shule mama. Aidha mradi huu umesaidia kuongeza idadi ya wanafunzi walioandikishwa darasa la awali na darasa la kwanza. Mradi wa tatu ni wa kikundi cha Vijana Technician Corporation, mradi huu ni wa vijana ambao awali walikuwa mafundi umeme ila baadae wakaamua kaunzisha duka la vifaa vya umeme, mradi huu umewanufaisha vijana kwani umeongeza ajira. Mradi wa nne n...

Mwenge Wa Uhuru Wamulika Dodoma,Kukimbizwa Km 1162

Image
Mwenge wa Uhuru leo umeingia Mkoa wa Dodoma , Makao Makuu ya Nchi ambapo utakuwa Mkoani hapo kwa kipindi cha Siku nane kuanzia tarehe 16/8 hadi 23/8/2022. Akizungumza baada ya kupokea Mwenge wa Uhuru kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Singida Mhe. Peter  Serukamba,Mkuu wa  Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule, amesema mwaka huu 2022 , Mwenge wa Uhuru katika Mkoa wa Dodoma utapita katika Wilaya saba na halmshauri nane za mkoa wa Dodoma ambazo ni Bahi, Dodoma Jiji, Chemba, Kondoa (V), Kondoa Mji, Chamwino, Mpwapwa na kumalizia Kongwa.  Ukiwa Mkoani Dodoma Mwenge wa Uhuru utakimbizwa kilometa 1162 na utapitia jumla ya miradi 39 ambapo kati ya miradi hiyo 39, 19 itawekewa mawe ya msingi, 10 itazinduliwa na 10 itatembelewa. Akileleza thamani ya miradi hiyo Mhe. Senyamule amesema kuwa miradi hiyo ina thamani ya Tsh.14,156,615,332/-. "Miradi hii imetekelezwa kwa ushirikiano mkubwa uliopo kati ya Serikali Kuu, Halmashauri, Wananchi na Wadau wa Maendeleo".Amesema RC Senyamule. Mhe. Seny...