Posts

Showing posts from September, 2022

TIMU YA OFISI YA MKUU WA MKOA WA DODOMA KUSHIRKIKI SHIMIWI 2022

Image
  Baadhi ya wafanyakazi wa ofisi ya Mkuu wa mkoa Dodoma wamekwenda kushiriki mashindano ya Shirikisho la Michezo la Wizara na Idara za Serikali (SHIMIWI), yanayotarajiwa kuanza Tarehe 01 Oktoba hadi tarehe 16 Oktoba 2022 huko Mkoani Tanga . Mashindano hayo yatafanyika katika viwanja tofauti tofauti   nane ambavyo ni Viwanja vya Mkwakwani ,Shule ya Sekondari Popatlal, Galanos sekondari, Bandari,Shule ya Tanga, Polisi Chumbageni na Viwanja vya Gymkhana. Mashindano hayao yakishirikisha timu mbalimbali kama vile mpira wa miguu, mpira wa pete,riadha, kuvuta Kamba na kukimbia.   geni rasmi katika mashindano ya SHIMIWI anatarajiwa kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Kassim Majaliwa. Mashindano hayo yatafunguliwa rasmi Oktoba 5. Kauli mbiu ya mashindano ya SHIMIWI 2022 ni ``Michezo hupunguza magonjwa yasiyo ambukiza na kuongeza tija mahala pa kazi``. Nahodha wa timu ya Mkoa Bw.Victor Makayula, amesema timu  ya mpira wa miguu  imejipanga...

"WIZARA TAFUTENI SULUHU YA MBWA WOTE WANAOZURULA MITAANI "-MHE.SENYAMULE

Image
Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Mkoa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule alipokuwa akizindua maadhimisho ya utoaji chanjo kwa mbwa na ili   kujikinga dhidi ya ugonjwa wa kichaa cha mbwa yaliyofanyika katika viwanja vya Mpunguzi Jijini Dodoma. “Kila mtu ambaye anafuga mbwa lazima afuate sheria na taratibu zake, naagiza wataalamu wa mifugo wa Wizara na Sekretarieti kutafuta suluhu ya mbwa wote wanaozurura mitaani. Mtu kama hawezi kufuata sheria, aache kufuga wanyama hao”   Amesema Mhe. Senyamule Mkuu wa Mkoa ameeleza, ugonjwa wa kichaa cha mbwa husababisha vifo 1500 kila mwaka nchini na Watoto chini ya miaka mitano ndio wamekuwa wahanga wakubwa zaidi. Hivyo, Serikali inatekeleza mpango mkakati wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi katika kutoa chanjo hii kila mwaka ambapo mpaka sasa takribani mbwa 338,000 wameshachanjwa. Mhe. Senyamule ametaja   lengo la Dunia ni kutokomeza ugonjwa wa kichaa cha mbwa ifikapo mwaka 2030 kwa kuhakikisha kuwa kila mbwa anapatiwa chanjo kila mwaka. “Na...

DODOMA KUHAKIKISHA WANAFUNZI WOTE WANAKUNYWA MAZIWA SHULENI

Image
Katika kudhimisha wiki ya unywaji maziwa Duniani. Taifa la Tanzania limeadhimisha huku msisitizo ukiwa unywaji wa maziwa   kwa   wanafunzi shuleni. Kitaifa maadhimisho hayo yamefanyika Jijini Dodoma   katika Viwanja vya Nyerere Square   kuanzia 26.9.2022 hadi 28.9.2022. Mkuu wa mkoa Mhe.Rosemary Senyamule   ndiye ambaye ndiye amekua mgeni rasmi wa shughuli hiyo. Akizungumza   Mkuu wa Mkoa   amesema   Mkoa wa Dodoma upo tayari kutekeleza mpango huo kwa kuhakikisha kila mwanafunzi anapata glasi ya maziwa shuleni. “Dodoma tupo tayari kuwa kama mfano kwa mikoa mingine katika utekelezaji wa zoezi hili na kuhakikisha kila mwanafunzi anapata angalau glasi moja ya maziwa akiwa shuleni kila siku”. Amesema   Mhe. Senyamule. Zaidi ya nchi 70 ikiwemo Tanzania zinaadhimisha wiki ya Unywaji maziwa Duniani ambapo mpango wa kuhakikisha kila mwanafunzi anapata maziwa shuleni ulianza kutekelezwa nchini mwaka 2017 na mpaka sasa takribani shule 48 zimenufa...