DODOMA KUHAKIKISHA WANAFUNZI WOTE WANAKUNYWA MAZIWA SHULENI





























Katika kudhimisha wiki ya unywaji maziwa Duniani. Taifa la Tanzania limeadhimisha huku msisitizo ukiwa unywaji wa maziwa  kwa  wanafunzi shuleni. Kitaifa maadhimisho hayo yamefanyika Jijini Dodoma  katika Viwanja vya Nyerere Square  kuanzia 26.9.2022 hadi 28.9.2022.

Mkuu wa mkoa Mhe.Rosemary Senyamule  ndiye ambaye ndiye amekua mgeni rasmi wa shughuli hiyo. Akizungumza  Mkuu wa Mkoa  amesema  Mkoa wa Dodoma upo tayari kutekeleza mpango huo kwa kuhakikisha kila mwanafunzi anapata glasi ya maziwa shuleni.

“Dodoma tupo tayari kuwa kama mfano kwa mikoa mingine katika utekelezaji wa zoezi hili na kuhakikisha kila mwanafunzi anapata angalau glasi moja ya maziwa akiwa shuleni kila siku”. Amesema  Mhe. Senyamule.

Zaidi ya nchi 70 ikiwemo Tanzania zinaadhimisha wiki ya Unywaji maziwa Duniani ambapo mpango wa kuhakikisha kila mwanafunzi anapata maziwa shuleni ulianza kutekelezwa nchini mwaka 2017 na mpaka sasa takribani shule 48 zimenufaika huku kauli mbiu ya mwaka huu ikiwa “Faulu Mtihani kwa glasi moja ya maziwa kwa siku”

“Juhudi ziendelee ili kila mtoto afikiwe na mpango huu, kwani maziwa yana faida nyingi mwilini kwa Watoto hasa kiakili” Ameongeza.

Hata hivyo, mgeni rasmi ameendelea kusema kuwa Serikali inaendelea na juhudi za kuhakikisha sekta za kilimo, uvuvi na ufugaji zinafanya shughuli zake kisasa zaidi kwani mpaka sasa mikopo yenye thamani ya shilingi Milioni 275 imetolewa kwa wafugaji kwa lengo la kuimarisha ufugaji nchini.

Pia Serikali imesamehe kodi ya ongezeko la thamani kwa vifungashio vya maziwa hivyo Serikali inatarajia kuona gharama za maziwa na bidhaa zinazotokana na maziwa zinashuka bei ili kila mmoja aweze kutumia bidhaa hiyo kwa urahisi kwani mtu mmoja anahitaji kunywa angalau lita 200 za maziwa kwa mwaka lakini kwa takwimu zilizopo sasa, mtu mmoja anakunywa lita 60 tu.

Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya mifugo na uvuvi Dr. Charles Mhina amesema lengo la siku hii ni kuhamasisha unywaji wa maziwa hasa kwa Watoto waliopo shuleni. Ameongeza kwa sasa lita za maziwa zipatazo Bilioni 3.4 zinazalishwa nchini lakini bado watanzania hatunywi maziwa.

“Tunapanga utaratibu wa kuwawezesha wadau kupatikana kwa kiasi kikubwa cha maziwa kukidhi idadi ya wanafunzi wote waliopo shuleni” Dr. Mhina

Siku ya unywaji maziwa shuleni inatekelezwa kufuatia wito wa Shirika la Chakula na kilimo ulimwenguni (FAO) ambapo kwa Tanzania, Bodi ya maziwa nchini (TADB) ambayo inaratibu mpango huu ikiwemo kufanya kampeni mbalimbali za uhamasishaji unywaji maziwa shuleni ambapo wadau mbalimbali wamejitokeza na wanaendelea kujitokeza kufadhili mpango huu kwa kugawa maziwa kwa wanafunzi kila siku ambapo mpaka sasa paketi 299 zimeshagawiwa kwenye shule kadhaa huku lita 6500 zikipokelewa kutoka kwa wadau hao.MWISHO

Comments

Popular posts from this blog

WALIMU WA HALMASHAURI YA JIJI LA DODOMA WATAKIWA KUTIMIZA WAJIBU WAO

WALIMU WATAKIWA KUFUNDISHA UZALENDO SHULENI.

‘WANAWAKE NA SAMIA’ 3000 MKOA WA DODOMA KUPATA MAFUNZO VETA