TIMU YA OFISI YA MKUU WA MKOA WA DODOMA KUSHIRKIKI SHIMIWI 2022

 Baadhi ya wafanyakazi wa ofisi ya Mkuu wa mkoa Dodoma wamekwenda kushiriki mashindano ya Shirikisho la Michezo la Wizara na Idara za Serikali (SHIMIWI), yanayotarajiwa kuanza Tarehe 01 Oktoba hadi tarehe 16 Oktoba 2022 huko Mkoani Tanga .

Mashindano hayo yatafanyika katika viwanja tofauti tofauti  nane ambavyo ni Viwanja vya Mkwakwani ,Shule ya Sekondari Popatlal, Galanos sekondari, Bandari,Shule ya Tanga, Polisi Chumbageni na Viwanja vya Gymkhana. Mashindano hayao yakishirikisha timu mbalimbali kama vile mpira wa miguu, mpira wa pete,riadha, kuvuta Kamba na kukimbia.

 geni rasmi katika mashindano ya SHIMIWI anatarajiwa kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Kassim Majaliwa. Mashindano hayo yatafunguliwa rasmi Oktoba 5. Kauli mbiu ya mashindano ya SHIMIWI 2022 ni ``Michezo hupunguza magonjwa yasiyo ambukiza na kuongeza tija mahala pa kazi``.

Nahodha wa timu ya Mkoa Bw.Victor Makayula, amesema timu ya mpira wa miguu  imejipanga kurudi na tshindi kutokana na kujiandaa vema kukabiliana na wapizani wao. ``Tumejipanga vyema kwani tulikua tunafanya mazoezi kila siku na vijana wangu wote wapo imara kabisa, Mkuu wetu wa Mkoa Mhe. Rosemary Senyamule ategemee vijana wake tutarudi na Kombe kwani tunakwenda na kauli mbiu yetu ya Dodoma, Fahari ya watanzania, hivyo lazima tuiheshimishe Makao Makuu ya nchi.  

Akizungumza kwa niaba ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma Dkt . Fatuma Mganga, Katibu Tawala msaidizi – Utawala Bw. Alois Muogofi amewataka wanamichezo hao kujiamini na kuuwakilisha vyema Mkoa wa Dodoma ambayo ndio makao makuu ya nchi.Aidha kwa niaba ya Dkt. Mganga, Bw. Muogofi  amewaombea kwa   Mwenyezi Mungu awatunze,awaongoze vyema ili waweze kushinda.  

 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Dodoma imewakilishwa na wanamichezo zaidi ya 35 ambao watashiriki michezo ya mpira wa miguu, mpira wa pete,riadha, kuvuta Kamba na kukimbia. MWISHO














Comments

Popular posts from this blog

WALIMU WA HALMASHAURI YA JIJI LA DODOMA WATAKIWA KUTIMIZA WAJIBU WAO

WALIMU WATAKIWA KUFUNDISHA UZALENDO SHULENI.

‘WANAWAKE NA SAMIA’ 3000 MKOA WA DODOMA KUPATA MAFUNZO VETA