Posts

Showing posts from October, 2022

SOKO LA MACHINGA KUANZA RASMI OKTOBA 30

Image
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule, amefanya kikao na machinga wanaotarajiwa kufanya biashara katika soko la machinga lililopo barabara ya Bahi, lengo kuu likiwa kusikiliza na kutatua    kero zao. Katika kikao hicho, Mkuu wa Mkoa ameongozana na Katibu Tawala Mkoa Dkt. Fatuma Mganga, Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Mjini, Mhe. Jabir Shekimweri, Kamati ya Ulinzi na usalama ya Wilaya pamoja na viongozi wanaosimamia soko hilo kutoka katika Halmashauri ya Dodoma Jiji. Mkuu wa Mkoa, ameanza kikao kwa kusikiliza kero kadhaa zinazowakabili machinga hao wakati wakisubiri kuhamia katika soko hilo. Miongoni mwa kero hizo ni pamoja na baadhi ya wafanya biashara kupangiwa vizimba ambavyo haviendani na biashara zao, baadhi ya machinga kukosa mikopo, machinga wa vitabu na magazeti kukosa vizimba, baba na mama lishe kukosa vizimba, daladala kushusa abiria eneo hilo, n.k Kero hizo zimepata majawabu kutoka kwa kaimu Mkurugenzi wa Jiji Bw. Msangi pamoja na Mwenyekiti wa kamati ya kuratibu u...

"Hela za Lishe zifanye Shughuli za Lishe "Dkt. Fatuma Mganga

Image
Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma, Dkt. Fatuma Mganga ameyasema hayo wakati wa kikao cha kujadili utekelezaji wa Viashiria vya Mkataba wa Lishe robo ya kwanza ya mwaka wa fedha 2022/2023, taarifa ambayo hutolewa kila baada ya miezi mitatu. Taarifa hii ni ya kipindi cha Julai hadi Oktoba 2022. Dkt. Mganga amesisitiza kuwa vikao vya lishe viwe vikao vinavyoleta tija, kwani suala la lishe ni suala mtambuka.Tunapaswa kutoa taarifa sahihi ambazo zinaonyesha uhalisia. Akitoa taarifa ya robo mwaka Bi. Adela Mlingi ameeleza kuwa Mkoa wa Dodoma una jumla ya shule 947 (shule za msingi na sekondari ), kati ya shule hizo 947, shule 830   ndizo zinazotoa chakula shuleni hii ikiwa sawa na 87.6%. Akikazia umuhimu wa Watoto/wanafunzi wote kupata uji au chakula wakiwa shuleni, Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma amewaelekeza wakurugenzi wa halmashauri zote saba za mkoa kuongea na wazazi wa wanafunzi kwenye Halmashauri zao ili kuja na utaratibu wa kuhakikisha angalau wanafunzi hao wanapata uji wa saa 4.00...

WANANCHI WASISITIZWA KUJISAJILI PEMBEJEO ZA RUZUKU

Image
Hayo yamejiri wakati wa kikao cha kutathmini mwenendo wa zoezi la usajili wa wakulima kwenye mfumo kwa ajili ya kupata mbolea na pembejeo za kilimo kutoka Serikalini kwa bei punguzo(ruzuku) kilichoitishwa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma kwenye Ukumbi wa Mikutano wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa. Kikao hicho kimehudhuriwa na wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi wa Halmashauri zote za Jiji la Dodoma pamoja na maafisa ugani. Baada ya kuwasilishwa kwa ripoti ya hali ya kilimo kwa sasa kwa Mkoa wa Dodoma pamoja na zoezi la usajili wa wakulima kwenye mfumo kwa ajili ya pembejeo za kilimo za ruzuku, Mhe. Senyamule amesema; “Twendeni tukahamasishe wananchi wajisajili kupata na kutumia mbolea, muwape elimu ya namna ya kutumia mbolea ya ruzuku kwani nguvu ya Serikali kwa sasa inakwenda kwenye kilimo” Hata hivyo, amewataka maafisa ugani kufanya oparesheni ya kujiwekea malengo kwamba kwa siku lazima wasajiliwe wakulima hamsini ingawa ana imani inawezekana kusajili wengi zaidi ya hao. Akiwasilisha ripoti ya Kili...