WANANCHI WASISITIZWA KUJISAJILI PEMBEJEO ZA RUZUKU











Hayo yamejiri wakati wa kikao cha kutathmini mwenendo wa zoezi la usajili wa wakulima kwenye mfumo kwa ajili ya kupata mbolea na pembejeo za kilimo kutoka Serikalini kwa bei punguzo(ruzuku) kilichoitishwa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma kwenye Ukumbi wa Mikutano wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa.

Kikao hicho kimehudhuriwa na wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi wa Halmashauri zote za Jiji la Dodoma pamoja na maafisa ugani. Baada ya kuwasilishwa kwa ripoti ya hali ya kilimo kwa sasa kwa Mkoa wa Dodoma pamoja na zoezi la usajili wa wakulima kwenye mfumo kwa ajili ya pembejeo za kilimo za ruzuku, Mhe. Senyamule amesema;

“Twendeni tukahamasishe wananchi wajisajili kupata na kutumia mbolea, muwape elimu ya namna ya kutumia mbolea ya ruzuku kwani nguvu ya Serikali kwa sasa inakwenda kwenye kilimo”

Hata hivyo, amewataka maafisa ugani kufanya oparesheni ya kujiwekea malengo kwamba kwa siku lazima wasajiliwe wakulima hamsini ingawa ana imani inawezekana kusajili wengi zaidi ya hao.

Akiwasilisha ripoti ya Kilimo Mkoa pamoja na zoezi la usajili kwenye mfumo kwa Halmashauri zote, Katibu Tawala Msaidizi  Uchumi na Uzalishaji Mkoa Bi. Aziza Mumba amesema kuwa, kutokana na changamoto ya muda mrefu ya upatikanaji wa pembejeo na mbolea bora, Serikali imeandaa mwongozo wa kusimamia mbolea ya ruzuku.

“Lengo hasa la Serikali ni kumpunguzia mkulima gharama za pembejeo za kilimo kwani bei ambayo Serikali itamsaidia mkulima wakati akihitaji kupata pembejeo za kilimo ni zaidi ya asilimia 50” .Amesisitiza Bi.Aziza Mumba.

Kuhusu ripoti ya waliokwisha jiandikisha kwenye mfumo wa kununua mbolea na pembejeo za ruzuku,Bi. Aziza amesema mpaka sasa kiwango bado hakiridhishi kwani ni chini ya asilimia 50 huku akisisitiza kuwa hakuna mbolea itakayouzwa nje ya mfumo wa ruzuku kwa mwaka huu wa kilimo.

 

MWISHO

Comments

Popular posts from this blog

WALIMU WATAKIWA KUFUNDISHA UZALENDO SHULENI.

TRAMPA KANDA YA KATI WAFANYA KIKAO DODOMA

BARAZA LA MITUME NA MANABII WAMTEMBELEA MKUU WA MKOA WA DODOMA