Posts

Showing posts from November, 2022

WATOTO 695,508 KUPATA CHANJO YA POLIO MKOANI DODOMA

Image
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma chini ya Idara ya Afya, imefanya kikao cha kamati ya afya msingi ikiwa ni katika kuhamasisha awamu ya nne ya utoaji wa chanjo ya kuzuia ugonjwa wa Polio kwa Watoto wenye umri kuanzia miaka 0 hadi miaka 5. Chanjo hiyo itaanza   kutolewa tarehe 1 Desemba mpaka 4, 2022. Chanjo hii kama ilivyokua ikitolewa kwenye awamu zilizopita, inatarajiwa kutolewa nyumba kwa nyumba ili kuweza kufikia idadi kubwa ya Watoto wenye uhitaji wa huduma hiyo ambapo matarajio ni kuchanja Watoto 695,508. Akihamasisha wazazi kushiriki kikamilifu kuwatoa Watoto wao wapate chanjo, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule amesema;  “Dodoma tumefanya vizuri katika awamu zilizopita na leo tunajadili namna nzuri ya kwenda kutekeleza awamu hii ya nne.   Mhe.Rais ametimiza wajibu wake kwa kutoa fedha na sisi tutekeleze jukumu hili. Nasisitiza chanjo ni salama, wazazi andaeni Watoto wote. Ni imani yangu tutakwenda kutoa elimu tutakayoipata hapa kwa wazazi wenye Watot...

''CHUO CHA UFUNDI DONBOSCO, MFANO WA KUIGWA"RC SENYAMULE

Image
  Chuo cha Ufundi Don Bosco Mkoani Dodoma ni Chuo cha Ufundi Stadi,ambacho kipo chini ya Kanisa Katoliki. Hivi karibuni Chuo hicho kimefanya mahafali yake ya 36 ambapo Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule akiwa mgeni rasmi katika hafla hiyo. Mahafali hayo yamejumuisha wahitimu 213 ambapo ni mchanganyiko wa wale waliokua wakisoma kozi ndefu na wengine kozi fupi katika fani ya umeme, kilimo, ufundi bomba, ufundi magari, uchomeleaji, mapishi, seremala, ushonaji n.k Mhe. Senyamule amekipongeza chuo hicho kwa kuwa mfano wa kuigwa. “Don Bosco mmekua mfano kwa kushiriki katika michezo, uwezeshaji wa vifaa vya kufanyia kazi kwa wanafunzi wanaohitimu pamoja na kushirikiana na Serikali hususani Ofisi ya Waziri Mkuu Watu wenye ulemavu. Hongereni sana. Watu wenye ujuzi ndio wenye uwezo wa kufanya mabadiliko katika jamii. Serikali ina uelekeo wa kuwa na viwanda vingi ambayo vinahitaji wataalamu wenye ujuzi hivyo hata Halmashauri zetu zimeelekezwa kuwawezesha wanafunzi wanaomaliza ...

"Mwelekeo wa Serikali ya Awamu ya Sita ni Wananchi" Rais Samia Suluhu Hassan

Image
Mhe. Rais nikupongeze kwa kazi za kitaifa na kimataifa unazozifanya kwa manufaa ya Watanzania" Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule ameyasema hayo wakati wa Mkutano wa hadhala wa Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania pamoja na Wananchi wa Wilaya ya Chemba. Akizungumza, Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan amewaeleza wananchi wa Chemba kuwa  mwelekeo wa Serikali ya awamu ya Sita ni wananchi ambapo msisitizo mkubwa ni kwenye elimu, maji, umeme,afya pamoja na kilimo. Akizungumza miradi ambayo imefanywa na Serikali ya awamu ya sita katika Halmashauri ya Wilaya ya Chemba, Mkuu wa Mkoa wa  Dodoma,  Mhe. Rosemary Senyamule ametaja miradi mbalimbali ambayo Mhe. Rais ameifanya katika Halmashauri hiyo. Miradi hiyo ni pamoja na Elimu ambayo inahusisha ujenzi wavymba vya madarasa pamoja na mikopo ya vyuo vikuu, afya, kilimo, barabara pamoja na umeme. Mhe.Senyamule amesema kuhusu sekta ya elimu,Mhe. Rais ametoa kiasi cha Tsh.9.7 bln, amejenga chuo cha VETA kwa gharama ya  Ts...