"Mwelekeo wa Serikali ya Awamu ya Sita ni Wananchi" Rais Samia Suluhu Hassan










































Mhe. Rais nikupongeze kwa kazi za kitaifa na kimataifa unazozifanya kwa manufaa ya Watanzania" Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule ameyasema hayo wakati wa Mkutano wa hadhala wa Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania pamoja na Wananchi wa Wilaya ya Chemba.

Akizungumza, Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan amewaeleza wananchi wa Chemba kuwa  mwelekeo wa Serikali ya awamu ya Sita ni wananchi ambapo msisitizo mkubwa ni kwenye elimu, maji, umeme,afya pamoja na kilimo.

Akizungumza miradi ambayo imefanywa na Serikali ya awamu ya sita katika Halmashauri ya Wilaya ya Chemba, Mkuu wa Mkoa wa  Dodoma,  Mhe. Rosemary Senyamule ametaja miradi mbalimbali ambayo Mhe. Rais ameifanya katika Halmashauri hiyo. Miradi hiyo ni pamoja na Elimu ambayo inahusisha ujenzi wavymba vya madarasa pamoja na mikopo ya vyuo vikuu, afya, kilimo, barabara pamoja na umeme.

Mhe.Senyamule amesema kuhusu sekta ya elimu,Mhe. Rais ametoa kiasi cha Tsh.9.7 bln, amejenga chuo cha VETA kwa gharama ya  Tsh. 2.2 bln na hivyo kwa mara ya kwanza Halmashauri ya Wilaya ya Chemba imepata chuo cha VETA. Aidha ujenzi wa vyumba vya  madarasa 46 unaendelea na madarasa hayo yatakamilika kabla ya mwezi Januari 2023 ili kuhakikisha wanafunzi wa kidato cha kwanza wanaingia madarasani. Aidha katika kuhakikisha kuwa wanafunzi wote wa vyuo vikuu wanaendelea na masomo Mhe. Rais ametoa Tsh.24.5bln ikiwa mikopo kwa wanafunzi wa vyuo vikuu.

"Kwa Upande wa Sekta ya afya Mhe Rais ametoa Tsh. 3.3 bln na bado kuna mradi wa kimkakati wa hospital ya Wilaya ambayo ujenzi wake bado unaendelea kwa gharama ya Tsh.2.0 bln" RC Senyamule.

Mhe. Senyamule amesema kuwa Uchumi wa  Wilaya ya Chemba unategemea sana Kilimo na Ufugaji.Kwa kuwajali wananchi wa Chemba Mhe. Rais ametoa Tsh. 1.0 Bln kwa ajili ya ujenzi wa ghala la kuhifadhia mazao ambalo ujenzi wake umekamilika.Hali kadhakila Mhe.Rais kwa kuwajali wakulima ametoa mbegu na mbolea za ruzuku pamoja,kwa kuwajali wafugaji Mhe. Eais ametoa fedha ambazo  zimewezesha ujenzi wa Majosho ya kuogeshea wanyama.

Aidha katika kukabiliana na kupanda kwa bei za vyakula Mhe. Senyamule amemueleza Mhe. Rais kuwa kuanzia wiki ijayo wananchi wa Chemba wameahidiwa kupata vyakula kwa bei rahisi.

"Kuhusu sekta ya maji, upatikanaji wa maji katika Halmashauri ya Wilaya ya Chemba ni 32%, hata hivyo kuna miradi 11 ya maji ambapo ikikamilika itapunguza changamoto hiyo, kwani itaongeza upatikanani wa maji kufikia 55%. Pamoja na miradi hiyo 11 ujenzi wa bwawa la Farkwa ambalo Serikali ya awamu ya sita chini ya utawala wa Rais Samia Suluhu Hassan umetoa jumla ya Tsh. 300 bln, mradi huu utatatua changamoto ya maji katika Halmashauri za Bahi, Chemba, Chamwino, Kondoa pamoja na Jiji la Dodoma.

Akizungumzia barabara Mkuu wa Mkoa amesema kuwa Serikali ya awamu ya sita imetoka kiasi cha Tsh. 3.3 trilioni kwa ajili ya ujenzi wa barabara za Halmashauri ya Chemba. Pamoja na hayo Serikali ya awamu ya sita imetoa kiasi cha Tsh. 30 bln kuhakikisha kila nyumba katika Halmashauri ya Chemba inapata umeme.


MWISHO.








Comments

Popular posts from this blog

WALIMU WATAKIWA KUFUNDISHA UZALENDO SHULENI.

TRAMPA KANDA YA KATI WAFANYA KIKAO DODOMA

BARAZA LA MITUME NA MANABII WAMTEMBELEA MKUU WA MKOA WA DODOMA