''CHUO CHA UFUNDI DONBOSCO, MFANO WA KUIGWA"RC SENYAMULE



























 

Chuo cha Ufundi Don Bosco Mkoani Dodoma ni Chuo cha Ufundi Stadi,ambacho kipo chini ya Kanisa Katoliki. Hivi karibuni Chuo hicho kimefanya mahafali yake ya 36 ambapo Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule akiwa mgeni rasmi katika hafla hiyo.

Mahafali hayo yamejumuisha wahitimu 213 ambapo ni mchanganyiko wa wale waliokua wakisoma kozi ndefu na wengine kozi fupi katika fani ya umeme, kilimo, ufundi bomba, ufundi magari, uchomeleaji, mapishi, seremala, ushonaji n.k

Mhe. Senyamule amekipongeza chuo hicho kwa kuwa mfano wa kuigwa. “Don Bosco mmekua mfano kwa kushiriki katika michezo, uwezeshaji wa vifaa vya kufanyia kazi kwa wanafunzi wanaohitimu pamoja na kushirikiana na Serikali hususani Ofisi ya Waziri Mkuu Watu wenye ulemavu. Hongereni sana. Watu wenye ujuzi ndio wenye uwezo wa kufanya mabadiliko katika jamii. Serikali ina uelekeo wa kuwa na viwanda vingi ambayo vinahitaji wataalamu wenye ujuzi hivyo hata Halmashauri zetu zimeelekezwa kuwawezesha wanafunzi wanaomaliza vyuo vya ufundi” RC Senyamule

Pia ameongeza kuwa Serikali imeendelea kutengeneza fursa mbalimbali kwa vijana kama vile kuziamuru halmashauri kutoa mikopo ya asilimia 10 kwa makundi yenye uhitaji kwenye jamii wakiwemo wanawake, vijana na watu wenye ulemavu, hivyo amewataka wahitimu hao kujiunga kwenye vikundi ili nao waweze kuwa wanufaika wa mikopo hiyo itakayowawezesha kujiajiri kwa ujuzi walioupata chuoni hapo.

Bi. Prisca Byala, Afisa Elimu Msingi ambaye amemuwakilisha Afisa Elimu Mkoa katika Mahafali hayo, amesema mafunzo haya ni hazina kwa vijana na Taifa kwa ujumla na anaamini kuwa yatawanufaisha huko wanapokwenda hivyo hakusita kuishukuru Serikali kwa kuyapa kipaumbele mafunzo ya ufundi stadi kwa vijana.

Kadhalika akiongea kwa niaba ya uongozi wa Chuo, Mkuu wa chuo hicho Mkoa wa Dodoma Father Boniface Mchami, amesema “Chuo kinawalea vijana katika maadili mema na ucha Mungu, chuo kina ushirikiano na vyuo vingine kupitia michezo, semina na shughuli mbalimbali. Tumefadhili vijana 67 wanaosoma hapa ambao hawana uwezo wa kulipa ada pia Chuo kimepata nafasi ya kushirikiana na kampuni 5 kutoka nchini Marekani zinazojishughulisha na uchimbaji wa mafuta na wametoa scholarship kwa wanafunzi wetu 10 pamoja na walimu wanne kwenda kwenye mafunzo ya mwaka mmoja nchini Marekani”. Amesema Father Mchami

 

MWISHO

 

 

Comments

Popular posts from this blog

WALIMU WA HALMASHAURI YA JIJI LA DODOMA WATAKIWA KUTIMIZA WAJIBU WAO

WALIMU WATAKIWA KUFUNDISHA UZALENDO SHULENI.

‘WANAWAKE NA SAMIA’ 3000 MKOA WA DODOMA KUPATA MAFUNZO VETA