Posts

Showing posts from September, 2023

MRADI WA KOFFIH WAIMARISHA HUDUMA ZA AFYA YA UZAZI NA MTOTO

Image
Idara ya Afya chini ya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma imefanya kikao cha tathmini ya utekelezaji wa mradi wa huduma ya afya ya uzazi na mtoto kilichofunguliwa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe Rosemary Senyamule ambaye amewakilishwa na Katibu Tawala Mkoa Bw. Ally Gugu katika Hoteli ya Vizano Jijini Dodoma. Mradi huo unatekelezwa katika Halmashauri mbili za Mkoa wa Dodoma ambazo ni Kongwa na Mpwapwa chini ya udhamini wa Taasisi ya nchini Korea inayojulikana kama KOREA FOUNDATION FOR INTERNATIONAL HEALTH CARE (KOFIH) ambapo wadau mbalimbali wa afya kutoka katika Halmashauri hizo wamehudhuria kikao hicho. Akifungua kikao hicho Bw. Gugu amesema tafiti zilizofanywa na Tanzania Demographic Health Survey ya mwaka 2022, inaonyesha viashiria vya huduma ya afya ya uzazi kwa Dodoma inafanya vizuri. Pia ameainisha idadi ya vituo vinavyotoa huduma ya afya kwa Mkoa wa Dodoma ambavyo vimekua chachu ya utoaji wa huduma Bora za afya. "Kwa mujibu wa sensa ya watu na makazi ya mwaka 2022, Mkoa wa Dodom...

MWENGE WA UHURU KUZINDUA MIRADI YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 16

Image
Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma Bw.Ally Senga Gugu  kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule amepokea Mwenge wa Uhuru kutoka kwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Singida Dkt. Fatuma Mganga kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Singida Mhe. Peter Serukamba. Makabidhiano hayo ya Mwenge wa Uhuru 2023 yamefanyika leo tarehe 29 Septemba 2023 katika Viwanja vya Bahi - Sokoni Wilayani Bahi Mkoani Dodoma. Akipokea mwenge huo Bw. Gugu amesema kuwa lengo kubwa la kuupokea mwenge ni kufanya uchechemuzi wa miradi pamoja kuhamasisha upendo, amani na ushirikiano. Katibu Tawala huyo akizungumza muda mfupi baada ya kupokea mwenge huo wa Uhuru amesema kuwa utapita katika Wilaya zote saba (7) na Halmashauri  nane (8) zikiwemo Bahi, Chemba, Kondoa Dc, Kondoa Mji, Dodoma jiji, Chamwino, Mpwapwa na kumaliza ratiba kwenye Wilaya ya Kongwa. Amesema mwenge huo wa Uhuru utakimbizwa kwa kilometa elfu moja Mia nane na tini na tatu (1893) na katika mbio zake utapitia jumla ya Miradi arobaini na tano (4...

WANANCHI WA KATA YA CHIHANGA WAASWA KUTOA USHIRIKIANO KWA SERIKALI

Image
  Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule amewataka wananchi wa kata wa Chihanga kutoa ushirikiano kwa Serikali popote wanapohitajika kwani hakuna Serikali yenye dhamira mbaya kwa watu wake ili katika kutatua changamoto za uvamizi katika chanzo cha maji cha Bonde la Mzakwe.  Senyamule ameyasema hayo Septemba 27, 2023 wakati wa ziara yake ya kikazi ya kuzungumza na wananchi wa  Kata ya Chihanga iliyopo katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Amesema lengo la ziara yake katika Kata hiyo ni kuendelea kutekeleza maelekezo ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya kuongea na wananchi, kusikiliza kero na kuzipatia ufumbuzi.  "Ndugu zangu naombeni mtoe ushirikiano hakuna Serikali yenye dhamira mbaya na wananchi wake na mnamfahamu Rais  wenu hataki kusikia mtu ananyanyaswa wala kupigwa, anataka wananchi wake wawe na amani na wasikilizwe kero zao ili kuendelea kudumisha umoja na mshikamano wa Tanzania."amehimiza Senyamule  Pia,...

"KUSTAAFU SIYO KUCHOKA" - MHE .SENYAMULE

Image
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule ametoa wito kwa Wastaafu watarajiwa kuendelea kutumia ujuzi wao kwakuwa wanamaarifa na uzoefu hivyo kuhakikisha wanajiunga katika taasisi zingine kwani Taifa bado linawahitaji. Kadhalika, amewaalika kuwekeza Mkoa wa Dodoma kwani  ndio Makao Makuu ya nchi hivyo bado kuna fursa mbalimbali za uwekezaji ikiwemo miundombinu mbalimbali kama vile Hoteli ,Kilimo  na Utalii. Mhe.Senyamule ametoa wito huo Leo Semptemba 26,2023 wakati akifunga semina ya wastaafu watarajiwa wa Mfuko  wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) iliyofanyika kwa muda wa siku mbili  katika Ukumbi wa Mikutano Jengo la PSSSF Jijini Dodoma.  "Kustaafu siyo kuchoka nikiwaangalia hapa sioni hata mmoja ambaye anaonekana kuchoka hivyo wekeni juhudi na maarifa pia tumieni uzoefu wenu katika taasisi nyingine za binafsi kwani muda baada wa serikali kuisha "Amesisitiza Senyamule  Mhe.Senyamule amesema lengo la semina hiyo ni kuwaandaa na kuwaelimi...
Image
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule mwishoni mwa wiki amefunga kongamano la kidini la waumuni wa Kiislamu (IJITIMAI) lililofanyika kwa takribani siku tatu katika Msikiti wa Gadaffi Jijini Dodoma. Akifunga kongamano hilo Senyamule amewasisitiza wanawake waumini wa dini hiyo kuendelea kuliombea Taifa ili maadili yaendelee kuimarika kutokana na kumomonyoka na kuibuka kwa maadili yasiyo ya Kitanzania ambayo yanaharibu Utamaduni wa Nchi. "Sisi ni wanawake tuna kazi ya kulea, kutunza, kufundisha tabia na kujenga watoto wetu, kwahiyo kazi hii tusiifanyie mzaha ni kazi ambayo ina nafasi nzuri kwa mwenyezi Mungu lakini maadili yanajengwa kama mtu ameiva ki-imani kwahiyo tuendelee kumuomba Mwenyezi Mungu watoto na vijana wetu wakuwe katika misingi na imani thabiti kwakuwa mtu mwenye imani anakuwa muadilifu.  "Hata Serikali tunawadhamini watu walioshika dini kwasababu fedha za Serikali zitatumika vizuri na Miradi inatunzwa ili kila mtanzania ataendelea kufurahia na kufaidika ...