ALAT WATEMBELEA JENGO LA MACHINGA











Uongozi wa Kamati tendaji za Serikali za Mitaa Tanzania ( ALAT), hivi karibuni umetembelea Ujenzi unaoendelea wa jengo la Machinga  Complex, lililiopo eneo la Bahi Road Jijini Dodoma. Viongozi hao wapo Jijini Dodoma kwa  ajili ya kuhudhuria, vikao vya kiutendaji.Aidha pamoja na vikao hivyo viongozi hao, waliamua  kutembelea jengo la Machinga Complex ili kuliona na kujifunza.

Wakiwa wameambatana na mwenyeji wao, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Anthony Mtaka, Mhe Mtaka aliwakaribisha kwenye mradi huo na kutoa shukrani na pongezi nyingi  sana kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan ambaye aliridhia ujenzi huo na kuchangia  kiasi ctah Tsh.2.5 bil, ambazo zitatumika kumalizia ujenzi wa   mradi huo. Mhe. Mtaka alisisitiza kuwa mradi huu unatakiwa kujenga ujasiri kwa Halmashauri kubuni miradi mingi zaidi kwani watu wa kuiunga mkono wapo.

Akielezea maendeleo ya mradi huo, Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma Bw. Joseph Mafuru, alisema kwa sasa Ujenzi upo kwenye awamu ya pili ya kukamilika na unatarajiwa kufanya kazi kwa saa 24 na mpaka kufikia Juni 30 mradi utakua umekamilika,ili ifikapo Julai Mosi, mradi uwe umezinduliwa rasmi kwa wafanyabiasha kuanza kuutumia.

Akizungumzia mradi huo, Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Mhe. Jabir Shekimweri amesema kuwa, mradi huo utasaidia Halmashauri ya Dodoma kuongeza mapato, kwani kwa  kipindi cha Mwaka  mmoja, mradi unatarajiwa kuingiza kiasi cha Milioni 100  ambazo zitakazotokana na ushuru wa huduma mbalimbali zitakazokua zikitolewa mahali hapo. Mhe. Shekimweli  ametaka mradi huu kutumika kama Mfano wa kuliweka Jiji katika mwonekano wa kuvutia na utumike kama sehemu ya utalii wa ndani ya Mkoa.

 Mwenyekiti wa ALAT Bw. Murshid Ngeze, alimshukuru Rais Samia  Suluhu Hassan kwa mchango wake kwa mradi huo na kuahidi kuwa watakuja kujifunza kupitia mradi huo. Aidha Bw. Ngeze ameitaka Halmashauri kuhakikisha  kuwa inasimamia vizuri mapato yatakayopatikana kutokana na mradi, kusimamia vizuri hali ya usalama kwenye eneo hilo kwa kuwa Biashara itafanyika kwa saa 24 pia ameshauri kuanzishwa mpango wa kutoa Mafunzo kwa wajasiriamali wanaotarajiwa kufanya biashara katika jengo hilo.

MWISHO


Comments

Popular posts from this blog

WALIMU WATAKIWA KUFUNDISHA UZALENDO SHULENI.

TRAMPA KANDA YA KATI WAFANYA KIKAO DODOMA

BARAZA LA MITUME NA MANABII WAMTEMBELEA MKUU WA MKOA WA DODOMA