Kata ya Ipagala Yawapongeza Walimu wa Shule Za Msingi Na Sekondari
Walimu wa Shule za Msingi na Sekondari za Serikali pamoja na wanafunzi kutoka Kata ya Ipagala, leo wamepongezwa kwenye hafla iliyoandaliwa na Diwani wa Kata hiyo Bw. Gombo Kamuli Doto. Mgeni rasmi katika hafla hiyo alikuwa Naibu Waziri- Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia Mhe.Omari Kipanga (Mb) ambapo mwenyeji wake alikuwa Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe Anthony Mtaka.Hafla hiyo ilifanyika katika viwanja vya Shule ya Msingi Mtemi Mazengo ambayo ni moja kati ya shule tano za Msingi za mfano nchini Tanzania.
Akielezea Shule hiyo Bw.
Gombo amesema kuwa Shule ya Msingi Mtemi Mazengo ni moja kati ya shule 5 za
majaribio zilizojengwa na Serikali kwa lengo la kupima ufaulu kulinganisha na
ule wa shule binafsi ambapo shule ina Madarasa 17, Miundo mbinu ya umeme na
maji, maktaba, nyumba za walimu 4, ukumbi wa mkutano, viti na meza nzuri za
kukalia waalimu pamoja na wanafunzi. Ujenzi wa shule hii umegharimu kiasi cha
Shilingi Bilioni 1 ambao kati ya hizo Tsh.700 milioni zilitolewa na Serikali
Kuu wakati zilizobakia zilitokana na mapato ya ndani. Shule ya Mteni
Mazengo imehitimisha darasa la Saba la
kwanza mwaka 2021 kwa kuwa na wahitimu 84 ambao wote walifaulu kwa viwango vya
juu.
Akiendelea, Diwani Gombo alitoa
taarifa fupi ya Shule zilizopo katika Kata yake ambapo alieleza kuwa Kata ya
Ipagala ina shule Sita za Serikali huku 4 zikiwa shule za msingi na 2 shule za
sekondari (shule ya sekondari Makole na shule ya sekondari Meria). Shule za Msingi
zina jumla ya wanafunzi 3190 ambao wote wamefanya vizuri kimkoa na Kitaifa
katika matokeo ya Mitihani ya Darasa la Nne na darasa la Saba mwaka 2021.
Akizungumza, Mkuu wa Wilaya
Mhe. Jabir Shekimweri, alimpongeza Diwani wa Kata hiyo Bw. Gombo na kuwaasa
wazazi kununua wakati ili kupata muda wa
kuongea na watoto wao,kwani hiyo itawasaidia Wazazi waweze kufahamu maisha ya watoto wao wakiwa shule, njiani na hata
wanapokua nyumbani kwa kuwa matukio ya ulawiti kwa watoto yameshamiri sana
kipindi hiki. Aidha Mhe.Shekimweri amefurahia maendeleo ya shule hiyo na
kuahidi kuupeleka Mwenge wa uhuru katika shule hiyo mara utakapo tembelea Mko wa Dodoma. "Nichukue fursa hii kuwafahamisha kuwa hiki ni deni kwangu Mwenge utakapokuja MNkoa wa Dodoma basi nitahakikisha utatenmbelea shule ya Msingi Mtemi Mazengo".Amesema Mhe. Shekimweri.
Nae, Mbunge wa Dodoma Mjini, Mhe. Anthony Mavunde, amempongeza sana Diwani Gombo, kwa kuwathamini na kuwatambua waalimu,kwani hiyo imekuwa chachu katika utendaji kazi wao, pia imewafanya wanafunzi kuzingatia masomo na kufaulu kiasi cha kutoa mwanafunzi wa kwanza katika mashindano yaliyohusisha shule binanfsi.Aidha Mhe. Mavunde amepongeza sana Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Mhe. Mtaka kwa kipaumbele chake katika Masuala ya Elimu.
Mkuu wa Mkoa wa
Dodoma,Mhe. Anthony Mtaka, ametoa maelekezo kwa shule
zote za Serikali Mkoani Dodoma na kuziagiza kuandaa vikao vya wazazi kila muhula, pindi shule zinapofungwa ili kujadili maendeleo ya Elimu kwa
watoto wao kwa kuwa malezi ya watoto ni baina ya mzazi, mwalimu na mtoto
mwenyewe, kwani matokeo yakiwa mazuri, pongezi huenda kwa wote hivyo wazazi
wawajibike kwa watoto wao.
Nae,Mgeni rasmi Naibu Waziri
wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe.Omary Kipanga,ameeleza kuwa suala la elimu
ni la lazima na si hiyari ndio maana Serikali inatimiza wajibu wa kutengeneza
Miundombinu Bora ya kufundishia kwani
Taifa Bora ni lile lenye watu wenye elimu." Serikali kwa kutambua umuhimu
wa elimu kwenye Mkoa wa Dodoma ambao ndio makao makuu ya nchi, imetoa Shilingi
Bilioni 17 kwa ajili ya Ujenzi wa Chuo kikubwa cha Tehama katika eneo la Nala
ambacho tayari kimeanza kujengwa" Mhe. Kipanga
Kwa niaba ya Walimu, Afisa
elimu Wilaya ya Dodoma Bi. Celina Shirati alimshukuru Diwani Gombo kwa kuandaa
shughuli hiyo na alisema walimu wamejisikia kuheshimiwa, kuthaminiwa na
kupendwa hivyo wataendelea kuchapa kazi kwani kipaumbele cha Mkoa ni kusimamia
Elimu.
MWISHO
Comments
Post a Comment