IBADA YA MAZISHI YA ALIYEKUWA KATIBU TAWALA MSAIDIZI RASILIMALI WATU MKOA WA DODOMA
Mkuu
wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule ameshiriki kwenye mazishi ya aliyekuwa
Katibu Tawala Msaidizi (Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu) Bw. Aloyce
Mwogofi katika ibaada ya mazishi iliyofanyika Mkoani wa Njombe, Kijiji cha
Itulike Kata ya Ramadhani.
Akizungumza
na wafiwa na waombolezaji Mkuu wa Mkoa wa Dodoma amewataka waombolezaji kuiga
mwenendo wake kwa kuiga mambo mema yoye aliyotekeza enzi za uhai wake.
“Mzee
Mwogofi alikuwa ni mchapa kazi kwa asili yake, muadilifu na mfano wa kuigwa
kuanzia vitendo, mavazi, nidhami na kwa kuwa kiongozi wa wa utumishi aliongoza
wengine kwa mfano”Alisisitiza Bi. Senyamule.
Kama
Serikali tunasema mapengo haya zibiki kwa maana hatutampata Mzee Mwogofi
mwingine lakini tunaomba Mwenyezi Mungu atusaidie tupate mtu ambaye hatutaona
hasara kubwa ya kumpoteza Mzee Mwogofi kwa maana ya alivokuwa.
"Mungu
awashike Mkono familia awatie nguvu endeleeni kumtegemea Mungu leo tunamlaza Mzee
wetu tuendelee kuiga mfano wa mzee wetu na tuige mema yake aliyokuwa anayanafanya”
Alisisitiza Mhe. Senyamule .
Naye
Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma Dkt. Fatuma Mganga amesema tunaomtegemea Mungu
tunaamini tunaeda kupata faraja kuu na tunaendelea na kazi itoshe kusema kwamba mzee Mwogofi alikuwa ni
mtu mwema akipenda upendo utamalaki katika eneo letu la kazi na hata nje ya
kazi, hivyo tumempoteza mtaalamu katika utumishi.
Marehemu Aloyce Mwagofi alishawahi kufanya kazi katika Ofisi mbalimbali ikiwemo Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Wizara ya Sheria na Katiba, Wizara ya ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Kama katibu Tawala Msaidizi seksheni ya Utawala na Usimamizi wa Rasimali watu.
Comments
Post a Comment