MHE. SENYAMULE AZINDUA BARAZA LA WAFANYAKAZI LATRA





                                        

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma amezindua rasmi Baraza la wafanyakazi  wa Mamlaka ya Udhibiti Usafiri ardhini  LATRA katika kikao  cha kwanza cha Baraza la wafanyakazi kilichofanyika ukumbi wa mikutano wa LATRA makao makuu Dodoma.

Akizungumza na wafanyakazi Senyamule amesema anawapongeza kwa kukamilisha taratibu za kisheria za kuunda baraza hili na Kusajiliwa na Kamishna wa kazi viongozi wa chama cha cummunication and workers traders union (COWTU) Taifa na Tawi la LATRA  kwa kuwezesha kufikia makubaliano na Menejimenti ya LATRA kwa kusaini mkataba na kuunda baraza la kwanza la wafanyakazi wa Mamlaka hii

‘’Katika kuendeleza mshikamano hapana budi Menejimenti ihakikishe kwamba haki za msingi za mtumishi zinatolewa  juhudi zitolewe katika kujifunza kujiendekeza kimasomo ili kuendeleza ufanisi wa kazi na kujiwekea misingi imara ya kujenga utumishi wa umma uliombora.

‘’Mfanyakazi ambaye ni mweledi na mwelewa anarahisisha kazi kwa kiongozi wake na kuifanya kuwa rahisi. Kila mmoja anatakiwa kuwa mfano wa kuingwa mahali pa kazi ili hata mtu anaweza kumsoma utendaji wake na kazi na ueledi wake wakati wa kazini

Naye Habibu Suluo Mwenyekiti wa Baraza la wafanyakzi na Mkurugenzi wa Mamlaka ya Udhibiti usafiri ardhini (LATRA ) Amesema kuwa wana mkataba mpya ambao unajumisha wafanyakazi wa Mkoa yote 26 pia Mamlaka ilianzishwa na sheria ya Bunge namba 5 ya mwaka 2019 iliyoanza kutekeleza majukumu yake tarehe 29 April 2019.

Comments

Popular posts from this blog

WALIMU WATAKIWA KUFUNDISHA UZALENDO SHULENI.

TRAMPA KANDA YA KATI WAFANYA KIKAO DODOMA

BARAZA LA MITUME NA MANABII WAMTEMBELEA MKUU WA MKOA WA DODOMA