JITIHADA NDO CHACHU YA MAFANIKIO "DKT MGANGA"

 







Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma Dkt. Fatuma Mganga, amefungua rasmi

mkutano wa kutoa mrejesho wa kazi zilizofanyika katika awamu ya kwanza na ya

pili ya utafiti wa kutumia mbinu za vinasaba katika ufuatiliaji wa malaria katika

kikao kazi kilichofanyika katika ukumbi wa jengo la Mkapa.


Akizungumza na Wajumbe walioshiriki kwenye kikao hicho, Dkt. Mganga

amesema kazi ya uchakataji sampuli zilizokusanywa mwaka 2021 imekamilika

na matokeo zaidi yalitolewa kwenye mkutano wa wadau uliofanyika mwezi mei

2022.

“Jitihada zenu mnazoendelea nazo ndizo zitakazokuwa chachu ya kufanikisha

kazi muhimu kwa nchi yetu mchango mkubwa unatolewa na wadau mbalimbali

katika mapambano dhidi ya malaria, katika ngazi ya Mkoa na Halmashauri na

katika vituo vya kutolea huduma za afya.


Napenda kuzishukuru taasisi na mashirika yote yanayohusika na Utafiti na

Taasisi ya Bill and Melinda Gates kwa kutoa ufadhii kwa ajili ya kutekeleza utafiti

huu, nawaomba muongeze juhudi ili tuweze kutokomeza malaria” amesema Dkt

Mganga.


Hata hivyo Mtafiti Mkuu wa ukusanyaji taarifa Mkoa wa Dodoma 2022 Dkt.

Deusdedith Ishengoma amesema kuwa wanatekeleza Utafiti wa kufuatilia

Ugonjwa wa Malaria Tanzania Bara kwa kutumia mbinu ya vinasaba MSMT

(Molecular Surveillance of Malaria in Mainland Tanzania) na lengo kuu la Utafiti

ni kuchunguza mabadiliko ya vimelea vya malaria ili kubaini Kama mbinu

wanazotumia kupambana na Ugonjwa huo zinafanya kazi ipasavyo.


“Utafiti huu unafanyika kwa lengo kufuatilia ubora na uwezo wa dawa za kutibu

Ugonjwa wa Malaria pamoja na ufanisi wa vipimo vya malaria vya papo kwa

papo (performance of rapid diagnostic tests for malaria” Amesema

Dkt. Ishengoma


Ameongeza kuwa kazi ya kukusanya Sampuli na Takwimu ilifanyika katika vituo

kumi vya kutolea huduma za kiafya kwa kila mkoa na kazi hii ilitekelezwa na

wafanyakazi wa vituo hivyo chini ya Usimamizi wa Waganga wakuu wa Mikoa na

Halmashauri wakisaidiwa na waratibu wa malaria wa Mikoa.

MWISHO

Comments

Popular posts from this blog

WALIMU WATAKIWA KUFUNDISHA UZALENDO SHULENI.

TRAMPA KANDA YA KATI WAFANYA KIKAO DODOMA

BARAZA LA MITUME NA MANABII WAMTEMBELEA MKUU WA MKOA WA DODOMA