MAFANIKIO YA SERIKALIYA AWAMU YA SITA TRA








 Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule amesema kumekuwa na ongezeko la ukusanyaji wa Mapato kutoka kwenye Halmashauri na kuwezesha maendeleo ndani ya Mkoa pia kupitia Mamlaka ya Mapato Tanzania – Mkoa wa Dodoma.

kizungumza na Waandishi wa Habari leo Ofisi kwake kupitia programu ya kutangaza Mafanikio ya Awamu ya Sita katika Kipindi cha miaka miwili, Mhe. Senyamule amesema Mkoa wa Dodoma ulipangiwa Fedha za miradi ya maendeleo kupitia mapato ya ndani ambapo kumekuwa na ongezeko kutoka shilingi 32,1 hadi kufikia shilingi 35.0 Sawa na 9%. 

Mhe. Senyamule amesema ongezeko hili limesaidia kuboresha huduma za jamii kwa kujenga vituo vya afya 4 zahanati 12 na vyumba vya madarasa 135 kupitia fedha za mapato ya ndani ya Halmashauri.

“Tunaposema mapato yanaweza kuchangia ongezeko la huduma kwa wananchi ni pamoja na sura hii ambayo imeonyesha ,Pia mapato ya Halmashauri yanapoongezeka yameonyesha ongezeko la utoaji asilimia 10 kwa wananchi kwa makundi maalumu, Wanawake ,Vijana na Watu wenye ulemavu” Alisisitiza Mhe. Senyamule

Amesema, Fedha za Mikopo ya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu (Asilimia 10) zimeongezeka kutoka shilingi 4,68 hadi kufikia shilingi 5,58 sawa na 19%. Ongezeko hili limesaidia kuongezeka kwa kiasi cha fedha kinachokopeshwa na idadi ya vikundi vinavyonufaika na mikopo inayotolewa.

“Hii maana yake wananchi hawa wote wataendelea kuongeza Mkopo ambao utawawezesha kuanzisha, kukuza na kuongeza  biashara ili kuwainua kiuchumi kwa wananchi kwakuwa ndio lengo la Serikali kuwatengenezea wananchi mazingira mazuri ,lakini fedha hizo pia za ongezeko katika Halmashauri zimewezesha kupatikana kwa Shillingi millioni 250.8 ambazo zinatolewa kwa ajili ya Watendaji wa kata 209 katika Mkoa wa Dodoma, Mpango ambao haujawahi kufanyika katika awamu zote zilizopita” Senyamule alibainisha.

Kwa upande wake Meneja Msaidizi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania Mkoa wa Dodoma, Sylver Rutagwelera ameelezea mafaniko yaliopatika kwenye taasisi hiyo katika kipindi cha miaka miwili.

Amesema katika kuhaikikisha Mamlaka ya Mapato inapanua wigo wa walipakodi na kuongeza makusanyo ya kodi, Mamlaka ya Mapato Mkoa wa Dodoma imefanikiwa kusajili walipakodi wapya 12,076 kwa kipindi cha Januari 2021 hadi Disemba 2022 kutokana na kuimarisha mahusiano mazuri kati yake na walipakodi ndani ya Serikali ya Awamu ya Sita.

Lakini pia,Mamlaka ya Mapato Mkoa wa Dodoma imefanikiwa kusajili walipa kodi wapya 2,237 wanaotumia Mashine za kieletroniki kwa mwaka 2022 pekee sambamba na hilo mkoa umeendelea kusimamia matumizi ya mashine za EFD kwa kutoa elimu na pia kutoa adhabu kwa wanaokiuka sheria.

Hata hivyo, Mamlaka imefanikiwa kutoa  elimu kwa walipa kodi na jamii kwa ujumla  ili kodi ilipwe bila shuruti na matumizi ya nguvu yasio na lazima pia imekuwa ikisimamia na kudhibiti makusanyo ya kodi.

Rutagwelera ameeleza katika kuhakikisha wanaongeza makusanyo ya kodi mamlaka ya mapato Mkoa wa Dodoma imejipanga kutekeleza ufatiliaji wa karibu wa matumizi ya mashine za EFD na ufatiliaji na usajili wa wafanyabishara wapya kwenye kodi ya mapato na kodi ya ongezeko la thamani.

Hata hivyo, ameelezea changamoto katika ukusanyaji wa mapatao licha ya kutoa elimu ya kutosha imekuwa bado wafanyabiashara na wananchi wamekuwa hawana elimu ya kutosha na ndio maana wamekuwa wakitoa elimu hasa pembezoni mwa mji katika vijiji vya Chipogolo, Mtera, Mbande, Songambele, Tubugwe, Hombolo, Mvumi misheni, Kibakwe, Wilaya ya Bahi, Chemba, Chamwino na Kondoa.

Comments

Popular posts from this blog

WALIMU WATAKIWA KUFUNDISHA UZALENDO SHULENI.

TRAMPA KANDA YA KATI WAFANYA KIKAO DODOMA

BARAZA LA MITUME NA MANABII WAMTEMBELEA MKUU WA MKOA WA DODOMA