HUDUMA ZIENDANE NA UFANISI

 







Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule amefungua mafunzo ya wawezeshaji wa Mkoa na Wilaya (ToTs) wa Moduli ya Mfumo wa Mshitishi ('PVS IMPLEMENTATION MANUAL') pamoja na Mfumo wa kieletroniki wa mshitiri (PVIMIS) 

Amefungua mafunzo hayo leo yatakayo fanyika kwa siku tatu yanayo ongozwa na wakufunzi Mfamasia Kirti Joshi na Bw. Haji Kisesa Afisa Tehama huku washiriki wakiwa ni Katibu Tawala wa Mkoa Bw. Ally Gugu, Mganga Mkuu wa Mkoa Dkt. Best Magoma, Waganga Wakuu wa Wilaya Wafamasia, Watalaamu wa Maabara na Maafisa Tehama mafunzo yaliyofanyika katika ukumbi wa Mkuu wa Mkoa uliopo jengo la Mkapa.

 "Mtazamo wa Serikali, nchi na dunia kwa ujumla unaenda kwenye Tehama kila kitu kinafanyika kwa njia rahisi na kuondokana na mfumo wa Manual maana yake tunapopata njia ya tehama maana yake tunaongeza ufanisi wa jambo tunalo lifanya kwaharaka, ubora, muda mfupi kwa nia ya kuongeza uwazi na uwajibikajii katika masuala ya fedha.

Nendeni mkafanyie kazi mfumo huu, Mjifunze kwa makini kwasababu ninyi mlio kuja ni ngazi ya wilaya ndio mnaosimamia vituo vya afya na Zahanati msiishie kufundisha wengine muwasimamie watumie vizuri huo mfumo ili ufanisi ulio kusudiwa na serikali uweze kuonekana ,ule mda mtakao pewa kwa ajili yakuanza kutumia mfumo sisi Mkoa wa Dodoma tunaharaka yakuanza kuutumia ili wananchi waondokane na adha ya upatikanaji wa madawa "Amesisitiza Mhe.Senyamule 

Upande mwingine Mhe. Senyamule ametoa rai kwa watendaji hawa wanapoenda kufanya kazi na mshitiri kuondoa urasimu usio na sababu

Nae Bw. Edward Magelewanya Mfamasia wa Mkoa ameishukuru TAMISEMI, Ofisi ya Katibu Tawala wa Mkoa na serikali ya Uswiss (Swiss Hpss) kupitia mradi wa TUIMARISHE AFYA kwa kuleta mfumo huu kwani utawasidia kuimarisha maboresho kwa huduma wanazotoa kwa wananchi na kuboresha upatikaji wa bidhaa za afya.

Comments

Popular posts from this blog

WALIMU WATAKIWA KUFUNDISHA UZALENDO SHULENI.

TRAMPA KANDA YA KATI WAFANYA KIKAO DODOMA

BARAZA LA MITUME NA MANABII WAMTEMBELEA MKUU WA MKOA WA DODOMA