BILIONI 17 KUJENGA MNARA WA MASHUJAA NA UKUMBI













Mkuu wa Mkoa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule amewapongeza  wana Dodoma kwa miaka 59 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ikiwa ni wiki ya maadhimisho sherehe hiyo na kuwataka vijana kuchangamkia fursa zinazoendelea kujitokeza jijini Dodoma.

Senyamule ameyasema hayo leo alipotembea mradi wa ujenzi wa uwanja na mnara wa mashujaa katika eneo  la Mji wa Serikali Mtumba.

‘’Leo nina furaha kubwa kwa kuwa maelekezo ya Mhe Rais wetu Dkt. Samia Suluhu Hassan aliyoyatoa hapa jijini Dodoma tarehe 25 Julai, 2022 wakati wa maadhimisho ya kumbukumbu ya mashujaa yanaendea kutekelezwa na hii ni heshma kubwa kwetu wana Dodoma kwakuwa Mradi huu kuanza kutekelezwa kwa vitendo. Kupitia mradi huu, tunakwenda kuweka alama nyingine muhimu itakayopendezesha Mkoa wetu ambao ndio Makao Makuu ya Nchi yetu, pia  wanadodoma watanufaika kiuchumi na kijamii” Senyamule amefafanua 

Aidha Mhe. Senyamule amewataka wakandarasi kuhakikisha wanatekeleza ujenzi wa mradi kwa hadhi kubwa na sifa nzuri kwa kuzingatia ubora na imara kwa miundombinu na kuzingatia muda waliopatiwa.

Katika hatua nyingine Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Senyamule amezungumzia maandalizi ya Mkoa wake kuelekea maadhimisho ya miaka 59 ya Muungano.

"Tunaelekea maadhimisho ya sherehe ya Muungano tarehe 26/4/2023 na hapa Dodoma tumeanza kuadhimisha toka tarehe 17/4/2023 ambapo tunajivunia mashujaa wetu walioweza kuunganisha Tanganyika na Zanzibar na kuleta Tanzania ambayo hii leo tunajivunia Muungano wenye mshikamano ,usio yumba,  wenye mtizamo sahihi kwa wananchi wake wa pande zote mbili na muungano ulio imarika kila sekta kwa Tanzania na Dunia kwa ujumla "Amesema Senyamule 

Kwa upande wake Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Dkt. Jimmy Yonaz amesema  fedha za ujenzi zipo tayari na zinatoka kwa wakati ambapo kiasi cha Shilingi bilioni 17  zitatumika kufanikisha ujenzi wa Mnara huo wa mashujaa pamoja na zahanati na sehemu ya kupumzikia na kusisitiza kuwa upande wa usimamizi wamejipanga vizuri .

Nae Meneja wa Kanda wa SUMA JKT Meja Generali Samwel Jambo ambaye pia  ndio Mkandarasi wa Ujenzi amesema wamejipanga kutekeleza kazi hiyo kwa wakati na ubora hadi kufikia siku maalumu.

MWISHO

 

Comments

Popular posts from this blog

WALIMU WATAKIWA KUFUNDISHA UZALENDO SHULENI.

TRAMPA KANDA YA KATI WAFANYA KIKAO DODOMA

BARAZA LA MITUME NA MANABII WAMTEMBELEA MKUU WA MKOA WA DODOMA