KUELEKEA MAADHIMISHO YA MIAKA 59 YA MUUNGANO VIONGOZI WAKIROHO JIJINI DODOMA WAKUTANA KULIOMBEA TAIFA
Mkuu wa Mkoa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule ameshiriki
maombi maalumu
ya kuliombea Taifa la Tanzania kuelekea maadhimisho ya miaka
59 ya Muungano
yalioandaliwa na ofisi ya yake kwa kushirikiana na
Kamati ya amani chini ya uongozi
wa Sheikh Mustapha Rajab Sheikh wa Mkoa wa Dodoma.
Lengo la maombi hayo ni kumuombea afya njema Rais wa
Jamuhuri ya muungano
wa Tanzania Mhe Dkt. Samia Suluhu Hassan, kuombea
Uchumi, kupinga uhujumu
uchumi, kukemea ukatili wa kijinsia na Ushoga, rushwa,
ukatili kwa Watoto,
Watumishi wa Serikali wa ngazi zote, Vyombo vya ulinzi na
usalama, hali ya hewa,
Makao makuu ya nchi na kuombea Muungano ili uendelee kudumu
pamoja na
viongozi waasisi wa Muungano wa nchi ya Tanganyika na
Zanzibar ambao ni
Mwalimu Julius K. Nyerere na Abeid Amani Karume.
Maombi hayo yamefanyika leo tarehe 24/4/2023
walipokutana viongozi mbalimbali
wa kiimani na serikali na kuhudhuliwa na viongozi wa
Serikali miongoni mwao ni
Wakuu wa Wilaya ya Chemba, Bahi na Dodoma mjini, hafla
iliyofanyika katika
ukumbi wa ‘Dear Mama’ jijini Dodoma.
“Tuendelee kuombea Muungano huu wa nchi ya Tanganyika na Zanzibar
uwe
wamfano siyo tu Afrika bali hata duniani kote watu
waseme upo muungano nchi ya
Tanzania ambao hauyumbi uendelee kuimarika kila siku,
tuombee viongozi wetu kila
siku waendelee kuongezewa hekima, maarifa, upendo na utayari
wa kuendelea
kutumika kwa ajili ya Watanzania na nchi yetu
iendelee kustawi kiuchumi, kuwa na
amani na utulivu ili kuendelea kukua katika kila sekta
za kijamii.
“Kadhalika kuombea mambo ya maadili ya Vijana wetu na
kutoa elimu kwa vijana
kuhusu maadili mema ya nchi yetu na kuwa mstari wa mbele
kupinga mambo yasio
faa katika nchi yetu “Amesisitiza Senyamule.
Naye, Katibu Tawala wa Mkoa Dodoma Bw. Ally Senga Gugu
amewashukuru
viongozi wakiimani kwa muutikio mzuri walio uonyesha na kuwa
mstari wa mbele
katika kushirikiana kwa kila kitu ikiwa pamoja na maombi
amewaasa kuwa na umoja
endelevu na kuendeleza maombi hayo ili mambo ya
maendeleo Mwenyezi Mungu
aweze kuongeza baraka.
Aidha, maombi hayo ya kuombea taifa na maadhimisho ya miaka
59 ya Muungano
Comments
Post a Comment