Posts

Showing posts from May, 2023

GWAJIMA AZINDUA PROGRAM YA JINSIA YA INTERNATIONAL FINANCE CORPORATION {IFC}

Image
  Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Mhe. Dkt. Dorothh Gwajima amezindua Programu ya Jinsia ya ANAWEZA itakayowawezesha wanawake kushiriki katika nafasi mbalimbali za uongozi kwa niaba ya Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Philip Isdor Mpango leo Mei 31, 2023. Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Dkt. Gwajima amesema Programu hiyo itakayogharimu fedha za Kimarekani milioni 7.5 inaendana na Dira ya Maendeleo ya Taifa ya mwaka 2025 , Mpango wa Taifa wa Maendeleo wa miaka mitano, Dira ya Maendeleo ya Zanzibar ya 2050, Sera ya Maendeleo na Jinsia ya 2000 na Sera ya Jinsia ya 2016 ya Zanzibar. "Uzinduzi wa Programu ya ANAWEZA ambayo inalenga kumkomboa mwanamke kiuchumi, imekuja kwa wakati muafaka ambapo Tanzania ipo katika jitihada za kumkomboa na kumuinua mwanamke kiuchumi. Tanzania ni mojawapo ya Mataifa yanayotekeleza malengo ya Jukwaa la Kimataifa ya Kukuza usawa wa Kijinsia. Katika hili Mhe Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri...

SENYAMULE ATATUA KERO ZA WAKAZI WA MBWANGA

Image
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule leo Mei 29, 2023 amefanya mkutano wa hadhara katika Kata ya Mnadani, Mtaa wa Mbwanga,Tarafa ya Dodoma Mjini, Wilaya ya Dodoma na kutoa ufumbuzi wa changamoto zilizokuwa zinawakabili wakazi hao. Awali, wakazi hao wa Mbwanga wamemshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwapatia kiasi cha Shilingi milioni 318.8 kwa ajili ya ujenzi waShule mpya yenye madarasa 7 ya msingi na mawili ya awali shule ambayo inaenda kutatua changamoto za wanafunzi kutembea umbali mrefu. Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Mhe. Godwin Gondwe amesema katika kufanikisha ujenzi wa shule hiyo wananchi wamechangia nguvu zao kwa kusafisha eneo lote la ujenzi, kujitolea huduma ya maji na kupanda miti kuzunguka eneo lote la shule hiyo. Hata hivyo Wakazi hao wametoa kilio chao mbele ya Mkuu wa Mkoa Mhe.Rosemary Senyamule kuwa wanakabiliwa na tatizo la kubwa la Maji, Umeme,Barabara na ukosefu wa huduma ya usafiri kuelekea katikati ya jiji. Senyamule ambae aliambatana na wataalam...

SENYAMULE AZINDUA PROGRAM YA WANAWAKE, UCHUMI NA VIWANDA

Image
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule amezindua Programu ya zunguka na Dkt. Samia ya wanawake na Uchumi wa Viwanda (WAUVI) Mkoa wa Dodoma wenye dhamira ya kuwainua wanawake kiuchumi na kukuza thamani ya mazao mbalimbali ya kimkakati Mkoani humo kupitia Semina na Mafunzo Mbalimbali yanayoandaliwa na Uongozi wa WAUVI. Uzinduzi huo umefanyika mwishoni mwa wiki katika Viwanja vya Nyerere Square jijini humo ambapo Mhe. Senyamule amewapongeza wanachama wa chama hicho na kuwataka waendelee kuhamasishana ili kuwa na wanachama wengi zaidi na kuboresha uchumi wao. "Niwapongeze kwa kuanza na kuthubutu nimesikia mikakati yenu kuwa mlianza na wanachama 65 pekee lakini leo ikiwa ni miaka miwili pekee mmefikia wanachama zaidi 3,700 hii ni idadi kubwa sana hongereni sana na nimeskia mmepanga kuwa na wanachama 10,000 kwa kasi hii mliyokuwa nayo inawezekana endeleeni kuhamasishana. "Maono yenu ya kuhakikisha wanachama wa WAUVI wanakuwa na nguvu ya kiuchumi nimeona pia kuna wanaume kwe...

SENYAMULE AAGIZA UJENZI WA MADARASA KUKAMILIKA KWA WAKATI

Image
  Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule leo Mei 29, 2023 ameendelea na ziara ya kikazi ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa mabweni katika Shule ya wasichana Bunge, ujenzi wa Shule mpya ya msingi katika eneo la Swaswa na madarasa ya awali katika Shule ya msingi Kisasa ambapo ujenzi wake uko katika hatua za ukamilishaji.   Katika kaguzi hizo Mhe. Senyamule ametoa maagizo kwa wasimamizi wa mradi kuhakikisha kazi inakamilika kwa muda uliopangwa na kuzingatia viwango vya ubora huku akitoa rai kwa wasimamizi wa ujenzi kukaa na mafundi ili kufanikisha ukamilishaji wake.   “Mkoa wa Dodoma tumejipanga kukamilisha hizi kazi kwa wakati hivyo wataalamu mkae na mafundi mpitie kwa pamoja mpango kazi wa miradi hii ili tujue kila siku ni kazi gani inatakiwa kukamilika kwa siku husika ili itakapofika tarehe 15 Juni 2023 ujenzi uwe umekamilika” Senyamule amesisitiza.   Aidha, Senyamule amesema kuwa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ametoa fe...

TUKUMBUKE KULIOMBEA TAIFA - SIMBACHAWENE

Image
Waziri wa Nchi Ofsi ya  Rais Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. George Simbachawene amewataka viongozi wa dini zote nchini kuendelea kuliombea Taifa amani, utulivu  pamoja na kukemea vitendo viovu vya mmomonyoko wa maadili vinavyoendelea duniani kote. Waziri Simbachawene ameyasema hayo wakati alipomuwakilisha Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa Majaliwa katika Ibada ya Harambee ya uchangishaji fedha katika Usharika wa Kongwa, Dayosisi ya Dodoma ambapo ameahidi kuchangia milioni kumi kwa ajili ya kumalizia jengo la Kanisa hilo huku akimbatana na viongozi mbalimbali wa Mkoa  wakiongozwa na Mkuu wa Mkoa Rosemary Senyamule na Spika Mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mbunge wa Jimbo la Kongwa Mhe. Job Ndugai. "Mhe. Rais amekuwa akitoa wito kila siku ya kwamba mara zote tukumbuke kuiombea nchi yetu iwe na amani, mshikamano, ustawi, mafanikio na maendeleo lakini pia tuliombee Taifa letu ili kuepukana na mmomonyoko wa maadili amb...