SERIKALI KUENDELEA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WANANCHI DODOMA












 

Serikali ya Awamu ya Sita, inayoongozwa na Mhe Dkt. Samia Suluhu Hassan

imeendelea kutatua changamoto mbalimbali ndani ya jiji la Dodoma kwa lengo la

kuwawezesha wananchi kujikwamua kiuchumi.


Kauli hiyo imetolewa na Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Ndugu

Daniel Chongolo katika viwanja vya Mtekelezo vilivyopo Shule ya Sekondari Central

Jijini Dodoma akihitimisha  ya ziara yake ya siku kumi ndani ya Mkoa wa Dodoma.

Ndugu Chongolo amesema kuwa changamoto hizo ni pamoja na migogoro ya ardhi,

sekta ya kilimo, elimu, Maji na ubovu wa miundombinu ya kufika kwenye vituo vya

kutolea huduma za afya. Ndugu Chongolo amesema kuwa lengo la ziara yake

 mkoani humo ni ilikuwa ni kusikiliza wananchi wa Mkoa wa Dodoma na kutatua

changamoto zao.

 

Vile vile amewaasa wafanyakazi wote waliopata nafasi za ajira kwenye miradi

mbalimbali inayoendelea kutekelezwa kufanya kazi kwa bidii ili kulinda ajira zao

pamoja na kuacha tabia ya wizi na kuchukua vitu visivyo halali badala yake

watangulize  uzalendo mbele kwa maendeleo ya Mkoa na taifa kwa ujumla.

 

Naye Naibu Waziri OR-TAMISEMI, Mhe. Deogratius Ndejembi amesema barabara

zinaendelea  kuboreshwa na kutengewa fedha kwa ajili ya Ujenzi na kukamilishwa

kwa Zahanati na Shule ya Sekondari. Aidha amesema kuwa changamoto za

miundombinu ya Zahanati ya Chali iliyopo Wilaya ya Bahi, Kituo cha afya cha

Msaada Wilayani Chemba vyote vitakamilishwa.

 

Kwa upande wake Waziri wa Ardhi, Nyumba na Makazi Mhe. Dkt. Angelina Mabula

amewataka wananchi wanaonunua ardhi kuanzia kwenye Halmashauri kabla ya

kununua ili kupunguza migogoro ya ardhi na utapeli

Mheshimiwa Mabula amesema hayo wakati akijibu hoja kuhusu migogoro ya ardhi

iliyopo ndani ya jiji la Dodoma kwani hadi sasa migogoro mingi ya ardhi imefanyiwa

kazi na ipo kwenye ngazi za Kiutawala kwa ajili ya Uamuzi. Amesema kuwa Wizara

yake imeweka Makamishina wawili wa ardhi maalumu, ambapo mmoja

atashughulikia migogoro ya jiji na mwingine nje ya jiji.

 

Huku, Waziri wa Kilimo Hussein Bashe amesema kiwanda cha kuchakata zabibu

kitajengwa na kitaendeshwa na sekta binafsi na viwanda vilivyopo ndani ya Mkoa wa

Dodoma ikiwa ni pamoja na kuendelea kukamilisha skimu za umwagiliaji Mkoani

Dodoma.

 

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Mhe. Rosemary Senyamule

amesema ziara ya Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi imekukuwa na manufaa

kwakuwa ameweza kupata elimu na kujifunza vitu mbalimbali sambamba na

kuzifanyia kazi changamoto zilizojitokeza na kuahidi kuendelea kutekeleza Ilani ya

Chama cha Mapinduzi kikamilifu. .

MWISHO















Comments

Popular posts from this blog

WALIMU WATAKIWA KUFUNDISHA UZALENDO SHULENI.

TRAMPA KANDA YA KATI WAFANYA KIKAO DODOMA

BARAZA LA MITUME NA MANABII WAMTEMBELEA MKUU WA MKOA WA DODOMA