TANZANIA NI MOJA NA HAITAGAWANYIKA-RAIS SAMIA.

















Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt.Samia Suluhu Hassan amewataka Watanzania kuendelea kuenzi mashujaa kwa kudumisha amani na kusisitiza kuwa Tanzania ni moja na haitagawanyika.

Rais Dkt.Samia amebainisha hayo leo Julai 25.2023 Jijini Dodoma katika Maadhimisho siku ya Kumbukumbu ya Mashujaa ambapo amesema ni muhimu kuenzi mashujaa kwa kudumisha amani ,Umoja na mshikamano.

Aidha, Rais Dkt. Samia ameagiza mnara wa mashujaa unaoendelea kujengwa katika mji wa Serikali Mtumba katika utekelezaji wa agizo alilolitoa Siku ya Kumbukumbu ya Mashujaa 2022 ukamilike kwa wakati huku akiagiza Wizara ya Fedha kutoa fedha kwa wakati.

Kwa upande wake Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe.Jenista Mhagama amesema mnara wa mashujaa wenye zaidi ya mita 100 utajengwa huku agizo la Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan la kujengwa mnara wa Mashujaa likitekelezwa.

Halikadhalika, Mhagama ameipongeza Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kutoa maelekezo ya kujengwa mnara wenye hadhi ya Makao makuu ya nchi Dodoma katika mji wa Serikali .

Kila ifikapo Julai 25 ya kila mwaka Tanzania imetenga siku maalum ya kumbukizi ya Mashujaa waliojitoa kulipigania Taifa la Tanzania wengine hata kupoteza maisha yao na hii ni kama ishara ya kukumbuka uzalendo , Ujasiri na ushujaa waliouonesha.

MWISHO

 

Comments

Popular posts from this blog

WALIMU WATAKIWA KUFUNDISHA UZALENDO SHULENI.

TRAMPA KANDA YA KATI WAFANYA KIKAO DODOMA

BARAZA LA MITUME NA MANABII WAMTEMBELEA MKUU WA MKOA WA DODOMA