Posts

Showing posts from October, 2023

MRADI WA BARABARA YA MACHINGA WAKABIDHIWA KWA MKANDARASI

Image
Mradi wa ujenzi wa barabara ya Machinga complex yenye urefu wa Km 0.65 kwa kiwango cha lami, umekabidhiwa kwa mkandarasi Oktoba 30, 2023. Hafla hiyo ya makabidhiano imehudhuriwa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe Rosemary Senyamule akiwa ndiye mgeni rasmi kwenye viwanja vya soko la Machinga Jijini Dodoma. Akitoa taarifa ya ujenzi wa barabara hiyo, Meneja wa Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) Mkoa wa Dodoma Injinia Edward Lemelo, ametoa ufafanuzi wa namna utekelezaji wa Mradi huo utakavyofanyika. "Ujenzi wa Machinga complex umesainiwa tarehe 25 Oktoba kwa shilingi 1,034,876,565.55 na Mkandarasi Nyanza Road Works Limited wa Dodoma kwa kipindi cha siku 180. Leo hii tupo hapa kwa ajili ya kumkabidhi eneo la mradi tayari kwa kuanza kazi. Kukamilika kwa matengenezo haya, kutarahisisha uingizwaji wa bidhaa sokoni na pia kutaboresha mazingira ya soko letu. Ujenzi huu utaambatana na ujenzi wa kitako cha barabara Km 0.65, matabaka manne ya barabara yaani G7, G15, C1 na CRR, ...

UZALENDO WAHITAJIKA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA SERIKALI.

Image
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe Rosemary Senyamule, leo Oktoba 30, 2023, amehudhuria kama mgeni rasmi hafla ya utekelezaji wa Mradi wa uboreshaji wa miundombinu ya Miji Tanzania ikihusisha ushindani (TACTIC) kwa Mkoa wa Dodoma unaotekelezwa na Kampuni ya CHINA GEO ENGINEERING CORP chini ya Mhandisi Msimamizi HONG - IK CONSULTANT CO. LTD kwa kushirikiana na GAUZE- PRO CONSULT (T) LTD na G & Y ENGINEERING CONSULT PLC hafla ambayo imefanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Mradi huo unaotekelezwa na Serikali kuu chini ya ufadhili wa Benki ya Dunia, una lengo la kuboresha miundombinu ya Barabara, madaraja, mitaro, majengo mbalimbali, vivuko vya barabara n.k pia una lengo la kujengeana uwezo kwa Taasisi tofauti tofauti. Akizungumzia wakati wa hafla hiyo, Mhe. Senyamule amesema Dodoma ina hadhi ya Miji ya Kimataifa kutokana na vipimo vya hadhi hiyo hivyo miradi hii izingatie hadhi ya Jiji hili. "Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ana maono na utashi mkubwa kwa Dodoma hivy...

DODOMA KUTUMIA GESI ASILIA MAJUMBANI

Image
  Uongozi wa Kampuni  inayojishughulisha na usambazaji wa gesi asilia kwa matumizi mbalimbali ikiwemo viwandani, usafirishaji na majumbani kutoka nchini Japan (JIKA), leo Oktoba 30, 2023, imekutana na uongozi wa Mkoa wa Dodoma chini ya Mkuu wa Mkoa Mhe. Rosemary Senyamule kujadili mpango wa kusambaza gesi asilia ndani ya Mkoa wa Dodoma ikiwa ni miongoni mwa mikoa mitatu iliyochaguliwa ambayo ni Dar es Salaam, Dodoma na Pwani. Akifafanua sababu za kuichagua Dodoma kuwa moja kati ya mikoa itakayofanikisha mpango huo, Msimamizi wa Mradi wa gesi asilia kutoka JICA Bw. Shinji Omoteyama amesema Dodoma ni Mji ambao hauna msongamano mkubwa hivyo ni salama kwa upitishaji wa mabomba ya gesi yatakayochimbiwa ardhini.  Kadhalika, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe Rosemary Senyamule, ameipongeza JICA kwa kuichagua Dodoma kwani kwa Sasa ndio Mkoa unaokua na kujengeka kwa kasi huku miradi mbalimbali ya kimkakati ikitekelezwa. "Dodoma inahitaji maendeleo mapya kwani ni Mji mpya unaokua kwa kasi...
Image
  Timu ya Wataalamu kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma iliyopewa jukumu la kutembelea na kukagua Miradi mbalimbali ya maendeleo katika Halmashauri za Kongwa na Mpwapwa imekamilisha zoezi la ukaguzi wa Miradi hiyo ikiwemo miradi ya Elimu, Afya na Nyumba za Watumishi. Timu hiyo  ikiongozwa na Mwenyekiti Bw. Jofrey Pima imefanikiwa kutembelea Miradi mbalimbali inayotekelezwa kupitia fedha kutoka Serikali Kuu, Miradi ya Sequip na Fedha za mapato ya ndani ya Halmashauri. Ikiwa Wilayani Kongwa timu hiyo imetembelea na kukagua Miradi mbalimbali ikiwemo Ujenzi wa nyumba ya Mkurugenzi unaogharimu Millioni 150, Ujenzi wa Jengo la Ofisi ya Mkuu wa Wilaya unaojengwa kupitia fedha kutoka Serikali Kuu unaogharimu Billioni 2.5, Shule Mpya ya Kata ya Sekondari Manungu iliyogharimu Millioni 544 Fedha kutoka Mradi wa Sequip pamoja na Ujenzi wa kituo cha Afya Pandambili uliogharimu Millioni 500 fedha kutoka Serikali Kuu. Aidha timu iliendelea na ukaguzi wa Miradi katika Wilaya ya Mpwapwa amb...

"ELIMU JUU YA MADHARA YA MVUA ZA EL- NINO ITOLEWE KWA WANANCHI" RAS GUGU

Image
Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa wameelekezwa kutoa elimu na maelekezo kwa wananchi wa Wilaya hiyo kuchukua tahadhari za kiusalama kuhusiana na tangazo la Mamlaka ya Utabiri wa hali ya hewa (TMA) kuhusiana na kuwepo uwezekanao wa kunyesha kwa mvua kubwa ya El-Nino ambayo inaweza kusababisha madhara hasa kwa wananchi wanaoishi maeneo hatarishi. Maelekezo hayo kwa watumishi wote yametolewa na Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma Bw. Ally Gugu  Leo Oktoba 26, 2023  wakati akiendelea na  ziara yake ya kikazi ya kufanya tathmini ya miradi na vyanzo vya mapato kwa Halmashauri, kukagua  na kufuatilia miradi hiyo kwa kipindi cha Julai hadi Septemba katika Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa Mkoa wa Dodoma. "Ndugu zangu kama tunavyo endelea kuhimizwa na mamlaka ya hali ya hewa, tunatarajia kuwa na mvua nyingi mwaka huu (EL-NINO) kwa hiyo niendelee kusisitiza tuchukue tahadhari kwa kuweka mazingira wezeshi kwa kipindi hicho ili kujiepusha na athari zake " Amesisitiza Bw.Gug...
Image
  Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma Bw. Ally Gugu  leo Oktoba 26, 2023 amekutana na kufanya mazungumzo na viongozi kutoka Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) katika Ofisi yake. Ugeni huo kutoka NBC umefika Ofisini hapo kwa lengo la kujitambulisha na kukuza ushirikiano uliopo kati ya Serikali na Benki hiyo na kujadili fursa zilizopo Mkoa wa Dodoma ikiwa ni miongoni mwa wadau muhimu wa maendeleo katika sekta ya uchumi wa Mkoa huo. Ugeni huo umeongozwa  na  Uongozi wa Benki hiyo akiwemo  Meneja wa Kanda Bw. Mirage Msuya ,Meneja wa Mahusiano kwa Wateja Binafsi Bi. Zawadi Kanyawana na Meneja Mahusiano Taasisi za Serikali  Bw. Abdallah Pazi .