Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma Bw. Ally Gugu  leo Oktoba 26, 2023 amekutana na kufanya mazungumzo na viongozi kutoka Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) katika Ofisi yake.


Ugeni huo kutoka NBC umefika Ofisini hapo kwa lengo la kujitambulisha na kukuza ushirikiano uliopo kati ya Serikali na Benki hiyo na kujadili fursa zilizopo Mkoa wa Dodoma ikiwa ni miongoni mwa wadau muhimu wa maendeleo katika sekta ya uchumi wa Mkoa huo.

Ugeni huo umeongozwa  na  Uongozi wa Benki hiyo akiwemo  Meneja wa Kanda Bw. Mirage Msuya ,Meneja wa Mahusiano kwa Wateja Binafsi Bi. Zawadi Kanyawana na Meneja Mahusiano Taasisi za Serikali  Bw. Abdallah Pazi .

Comments

Popular posts from this blog

WALIMU WA HALMASHAURI YA JIJI LA DODOMA WATAKIWA KUTIMIZA WAJIBU WAO

WALIMU WATAKIWA KUFUNDISHA UZALENDO SHULENI.

‘WANAWAKE NA SAMIA’ 3000 MKOA WA DODOMA KUPATA MAFUNZO VETA