Posts

Showing posts from November, 2023

WAZAZI/WALEZI WALINDENI WATOTO DHIDI YA UKATILI.

Image
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule amewaasa wazazi na walezi kuwajengea watoto uwezo wa kujitambua na kujilinda dhidi ya ukatili wa kijinsia kufuatia hatari ya matukio ya ukatili na unyanyasaji yanayoendelea katika jamii. Ni katika viwanja vya 'Nyerere square' Jijini Dodoma ulipofanyika uzinduzi wa siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia leo Novemba 30/2023. "Nitumie fursa ya kampeni hii ya siku 16 kuwakumbusha wazazi/ walezi na jamii kuwajengea watoto wetu uwezo ili waweze kujitambua na kujilinda dhidi ya matukio ya ukatili kwani watoto Wapo katika hatari zaid ya kufanyiwa vitendo vya ukatili. "Nitoe rai kwa watendaji katika ngazi mbalimbali kuhakikisha kunakuwa na mifumo ya utoaji wa msaada wa haraka pale inapobainika mtu amefanyiwa ukatili  wa kijinsia ili manusura awezeshwe kupata huduma kwa haraka kuepusha athari zaidi," amesema Senyamule Aidha Senyamule ametaja maeneo ya kupeleka taarifa ikiwa mtu amefanyiwa ukatili ni Kituo cha huduma za Afya, D...

NZUGUNI KUNUFAIKA NA MRADI MKUBWA WA MAJI.

Image
  Wananchi na wakazi wa Eneo la Nzuguni wanaelekea kupata afueni ya changamoto ya muda mrefu ya ukosefu wa maji baada ya kukamilika kwa mradi Mkubwa wa Maji unaotekelezwa kwa fedha za Serikali kiasi cha Shilingi Bilioni 4.8 unaotarajiwa kuanza kutumika mwezi Januari 2024. Mradi huo una lengo la kuongeza kiasi cha maji yanayosambazwa kwa wananchi kwa asilimia 11.7 Hayo yamebainishwa leo Novemba 27, 2023 wakati Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule alipotembelea mradi huo wa maji kujionea hatua iliyofikiwa. Mhe. Senyamule ameshuhudia ujenzi wa tanki kubwa la kuhifadhia na kusambazia maji lenye ujazo wa Lita Milioni 3 likiwa na urefu wa mita 300 pamoja na uchimbaji wa visima virefu Hadi mita 300 kwenda chini ya ardhi. "Leo tunashuhudia matokeo ya Matumaini yetu ya siku nyingi ya kuwa siku moja tutapata maji kwenye eneo hili na maeneo ya jirani. Nilikua natamani sana maji yapatikane Dodoma kwa hadhi ya makao makuu. Jambo hili limekua la kihistoria kwa Dodoma. Wananchi, tuende...

KONGWA AFRICAN LIBERATION MARATHON YAFANA.

Image
Mkuu wa Wilaya ya Kongwa Mhe. Remidius Mwema Emmanuel amesema mashindano ya 'Kongwa African Liberation Marathon' yana lengo la kuwakumbusha Watanzania namna Tanzania kupitia Wilaya ya Kongwa ilivyoshiriki katika kupigania Uhuru wa Mataifa Mengine ya Afrika. Ni katika viwanja vya Saba Saba Halmashauri ya Kongwa leo Novemba 25/2023 kulipofanyika mbio hizo ambapo Mhe. Mwema ameweka bayana dhamira ya kuanzishwa kwa mbio hizo ni kuukumbusha Umma wa Watanzania namna Wilaya yake ilivyoshiriki katika kupigania Uhuru wa baadhi ya Mataifa ya kusini mwa Afrika. "Tunachokifanya leo ni kuwakumbusha Watanzania ili watambue kuwa nchi Yetu hususan Mkoa wa Dodoma na Wilaya ya Kongwa, ilisaidia kwa kiasi kikubwa kupigania Uhuru wa baadhi ya Nchi za kusini mwa Afrika kupitia Kambi ya mafunzo ya wapigania Uhuru ambayo ilikuwa hapa Kongwa," Mhe. Mwema Hata hivyo, Mhe. Mwema amebainisha kuwa mbio hizo za 'Kongwa African Liberation Marathon' zitaendelea kufanyika Kila mwaka huku wak...

WACHIMBAJI MADINI WANEEMEKA NA TEKNOLOJIA .

Image
  WACHIMBAJI MADINI WANEEMEKA NA TEKNOLOJIA Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule amesema uwepo wa kifaa cha kupima uwepo na umbali   wa Madini Chini ya ardhi kilichonunuliwa na Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, kitawasaidia Wachimbaji Madini kuchimba kwa tija na kupata faida. Mhe. Senyamule amebainisha hayo leo Novemba 24/2023 katika Ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Jengo la Mkapa ambapo amefanya kikao kazi cha kusikiliza na kutatua kero mbalimbali za wafanyabiara wakubwa na wa kati wa Mkoa huo. "Serikali Imenunua Mashine za kupima mkondo wa Madini ili kuwaondolea adha wachimbaji ili kujua kiwango na umbali ambao wachimbaji watakumbana nao hadi kuyafikia Madini yalipo na wataepukana na uchimbaji wa kubashiri hali ambayo itawaondolea kadhia ya kupoteza muda na nguvu walizotumia katika kuchimba eneo lisilo na Madini" Mhe. Senyamule Aidha Mhe. Senyamule ametoa wito kwa wafanyabiashara kujenga hoteli zenye hadhi ya nyota tano ili kufungua furs...

RAIS SAMIA AMEOKOA MAISHA YA WATOTO NJITI-NDG CHATANDA

Image
  Mwenyekiti wa UWT Taifa Ndg. Mary Chatanda, amesema Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameokoa maisha ya watoto njiti kwa kuongeza wodi ya Mama na Mtoto kwenye Hospitali ya Wilaya ya Bahi. Ameyasema hayo leo 24 Novemba 2023 katika ziara yake ya kikazi ya kukagua miradi na kuongea na wanachi Katika Halmashauri ya Wilaya ya Bahi Mkoa wa Dodoma. “Hatuna budi kumshukuru Rais wetu Mama Samia kwa kuleta wodi yingi za Mama na Mtoto na kuokoa maisha na vifo vya watoto njiti kwani maisha yao yalikuwa hatarini. “ lakini tunaona wananchi wanavyofurahia huduma zinazoletwa kwao kwani ni bora na sahihi kwa watoto” Amesema Chatanda. Pia Chatanda, amefanya ziara ya kukagua miradi inayotekelezwa na ilani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) katika Nyumba ya Katibu wa UWT WIlaya ya Bahi yenye thamani ya Shilingi 7,900,000 Hospitali ya Wilaya yenye thamani ya shilingi Bilioni 3.2, na Shule Mpya ya Sekondari ya Chali yenye thamani ya shilingi Bilioni 544 na kusik...

WAZAZI TUWAJIBIKE KATIKA MALEZI YA WATOTO - NDG. KINGWANDE.

Image
Uongozi wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) unaofanya ziara ya kukagua utekelezaji wa ilani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) ndani ya Mkoa wa Dodoma chini ya Mwenyekiti wake Ndg. Mary Chatanda,  Novemba 23, 2023  umeendelea na ziara yake kwa siku ya pili ikiwa imefikia katika Halmashauri ya Wilaya ya Chemba Mkoani humo. Ziara ya Uongozi huo imegawanyika katika timu mbalimbali ambapo Naibu Katibu Mkuu Ndg. Riziki Kingwande amefanikiwa kutembelea mradi wa Ujenzi wa Vyumba 4 vya madarasa na Ofisi 3 katika Shule ya Msingi Mwaikisabe wenye thamani ya Shilingi 90,000,000 kituo cha Afya cha Soya kilichopo kwenye kata ya Soya ndani ya Halmashauri ya Chemba pamoja na kusikiliza kero za wananchi. Akizungumza na wananchi wa Kata za Soya na Kimaha  amewataka wazazi kuwajibika katika malezi ya watoto wao na kuwa walinzi  kwani kwa Sasa maadili yameporomoka hivyo amewasihii kundokana na desturi ya kuamini watu kwa urahisi kwani Dunia imeharibika . "Wazazi naombeni tuwajibike katika ku...