KONGWA KUNUFAIKA NA MABINGWA WA MACHO








Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule ametembelea na kuzindua kambi ya madaktari Bingwa wa macho inayofanyika katika hospitali ya Wilaya ya kongwa, ambapo dhamira kuu ya kuwepo kwa kambi hiyo ni kuwasaidia wananchi kujua hali za kiafya za macho yao na hizo zinatolewa pasi na gharama zozote.

Mhe. Senyamule amesema kuwa Mkoa wa Dodoma ni miongoni mwa Mikoa inayotekeleza mradi wa Macho Yangu unaotekelezwa na shirika lisilo la kiserikali la` Sightsavers` linalojishughulisha na utoaji wa huduma za macho.

“Shirika hili linajishughulisha na utoaji wa huduma za macho ikiwepo upimaji wa miwani, pamoja na hayo shirika litasomesha madktari wasaidizi wa macho wawili na wauguzi sita pia litanunua baadhi ya vifaa vya macho na kusaidia kuundwa kwa mabaraza ya watu wenye ulemavu na kuwezesha huduma za kliniki tembezi za macho kama hii iliyozinduliwa leo,’’ Mhe. Senyamule

Hatahivyo licha ya manufaa yanayopatikana kutokana na uwepo wa madaktari hao Mhe. Senyamule amesema miongoni mwa changamoto zinazojitokeza katika utolewaji wa matibabu hayo ni pamoja na baadhi ya wagonjwa kutofika katika vituo vya huduma mapema hali inayopelekea baadhi yao kupoteza uwezo wa kuona.

“Pamoja na jitihada zinazofanyika bado kuna changamoto inayotokana na baadhi ya wagonjwa kushindwa kufika katika vituo vya kutolea huduma mapema hadi pale wanaposhindwa kuona kabisa, Mradi huu umekuja kwa wakati na ni matumaini yangu kuwa huduma hizi za kibingwa zitwanufaisha wananchi wengi,” amesisitiza Senyamule

Kambi ya madaktari bingwa wa macho katika halmashauri ya kongwa itadumu kwa takribani siku nne kuanzia Disemba 11 -14/12/2023 huku wananchi wakipatiwa matibabu ya macho bila kuchangia gharama zozote hali inayopelekea wananchi na wakazi wa Wilaya ya kongwa kunufaika na ujio wa mabingwa hao.

Comments

Popular posts from this blog

WALIMU WATAKIWA KUFUNDISHA UZALENDO SHULENI.

TRAMPA KANDA YA KATI WAFANYA KIKAO DODOMA

BARAZA LA MITUME NA MANABII WAMTEMBELEA MKUU WA MKOA WA DODOMA