CHAMWINO DC YATAKIWA KUJITAFAKARI










 Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe.Rosemary Senyamule ameiagiza Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino kukamilisha ujenzi wa uzio wa ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo kabla ya tarehe 30/3 / mwaka huu.


Maagizo hayo yametolewa Leo Februari 21,2024  baada ya kuonekana kudorola Kwa mradi huo Kwa zaidi ya miezi 8 tangu ulipotakiwa kukamilika  mwezi julai 2023.

"picha ya Chamwino Kwa Sasa siyo nzuri, Mkoa una Halmashauri nane na katika Halmashauri hii kila miradi inayokuja lazima zijitokeze changamoto, tunapokea malalamiko yenu mengi  hasa suala la malipo Kwa wakandarasi wanaojenga miradi yenu, Mhe.Rais anatoa fedha zote ila nyie mnachelewesha kuwalipa  na hiyo ndio sababu inachangia mradi kutokukamilika kwa wakati. nitoe maagizo tarehe 30/03/2024 mradi uwe umekamilika kwa ubora wake na ukamilike kwa fedha ambazo zilitolewa  na ikiwezekana fedha zibaki na zifanye kazi nyingine". Ameelekeza Mhe.Senyamule 

Aidha Mhe. Senyamule amemsimamisha kazi mtendaji wa kata ya Manchali Bw.Waitara Wambura Kwa kuonesha utovu wa nidhamu na kukiuka maadili ya kazi kutokana kulewa pombe katika masaa ya muda wa kazi na kumtaka Mkurugenzi wa Halmashauri kufanya uchunguzi wa kina juu ya utendaji kazi wa mtendaji huyo.

Kwa upande wake kaimu  Mkuu wa wilaya ya Chamwino Mhe. Godwin Gondwe ameahidi kusimamia bega Kwa bega miradi inayotekelezwa katika wilaya hiyo na kukamilika Kwa ubora na muda uliopangwa.

Mhe.Senyamule  ikiwa ni muendelezo wa xiara zake za kikazi amekagua Ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Wasichana Mkoa  ,Ujenzi wa uzio wa Jengo la ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Chamwino, Ujenzi wa Zahanati ya Wilunze ,eneo la maadhimisho ya  siku ya wanawake pamoja na kufanya Mkutano wa hadhara na Wananchi wa Kata ya Manchali

Comments

Popular posts from this blog

WALIMU WA HALMASHAURI YA JIJI LA DODOMA WATAKIWA KUTIMIZA WAJIBU WAO

WALIMU WATAKIWA KUFUNDISHA UZALENDO SHULENI.

‘WANAWAKE NA SAMIA’ 3000 MKOA WA DODOMA KUPATA MAFUNZO VETA