MHE. SENYAMULE AONGOZA KIKAO CHA BARAZA LA BIASHARA MKOA
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe.Rosemary Senyamule tarehe 24.05.2024 ameongoza kikao cha baraza la biashara la Mkoa huo kilichofanyika kwenye ukumbi wa mikutano Jengo la Mkapa.
Lengo la kikao hicho ni kujadili masuala la biashara na uwekezaji kikiongozwa na mada mbalimbali ambazo ni pamoja na mfumo wa masoko wa kieletroniki, matokeo ya tathmini ya mazingira ya biashara yanayokwamisha ukuaji wa biashara kwa sekta binafsi na wasilisho kuhusu stakabadhi ghalani .
Sambamba na hayo kikao hicho kimeazimia mambo kadhaa ikiwamo timu ya watalaam iundwe kwa ajili ya kutangaza fursa za uwekezaji zilizopo Mkoa huo na mamlaka ya mapato Tanzania (TRA) kuboresha namna kutoa elimu kwa wafanyabiashara wadogo (machinga) nk.
Kwa upande wake Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma Bw. Kaspar Mmuya amewahimiza wadau wa sekta binafsi na Halmashauri zote za Mkoa huo kufanya uwekezaji katika sekta ya maliasili na utalii hususani ufugaji wa nyuki kwani ni ufugaji wa muda mfupi na ambao utasaidia kukuza uchumi wa kukidhi mahitaji muhimu.
Awali Afisa Kilimo Mkoa huo Bw.Bernard Abrahamu ametoa wito kwa wananchi wote wa Mkoa huo na Taifa kwa ujumla kuchangamkia fursa ya maonesho ya nanenane ambayo kitaifa yanafanyika Jijini hupo.
Ameongeza kuwa zipo fursa mbalimbali ambazo ni pamoja na upatikanaji wa huduma zote sehemu moja (one stop center) zikiwemo bima na kwamba maonesho hayo yatakuwa ya muda wa siku nane kuanzia tarehe 01/08 - 08/08/2024 na kuwakaribisha wafanya biashara kutumia maonesho hayo kwani yanahusisha kilimo kwa mapana na wananchi wanahamasishwa kupelaka bidhaa zao kwani ni eneo la biashara.
&&&
#keroyakowajibuwangu
#dodomafahariyawatanzania
ReplyForward |
Comments
Post a Comment