BODABODA WATAKIWA KUCHUKUA TAHADHARI JUU YA ABIRIA WAO
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule ametoa angalizo kwa Maafisa usafirishaji wa Pikipiki (bodaboda) kuchukua tahadhari juu ya abiria wanaowapakia kutokana kuibuka kwa matukio ya kihalifu yanayofanywa na watu wasiojulikana dhidi ya Maafisa hao siku za hivi karibuni.
Rai hiyo imetolewa Juni 18, 2024 wakati wa muendelezo wa utekelezaji wa kauli mbiu "kero yako, wajibu wangu" kwenye mkutano wa hadhara na wananchi wa kijiji cha Bahi Sokoni katika Halmashauri ya Bahi wenye Lengo la kusikiliza na kutatua kero zinazowakabili.
"Bodaboda tuendelee kufuata maelekezo ambayo tunapewa juu ya umuhimu wa sisi kuchukua tahadhari ili kuongeza usalama wetu kwa kuangalia abiria tunao wapakia. Kama unaona humuelewi, achana naye usimpakie ili kuondoka na adha za namna hii" Ameagiza Mhe. Senyamule
Kero hiyo, iliibuliwa na mmoja wa wakazi wa eneo hilo Bw. Andrew Laurent wakati wa mkutano huo ambapo amesema siku za hivi karibuni kumetokea matukio ya aina hiyo ambayo yamekuwa kero kwa Maafisa usafirishaji hao hivyo kuhatarisha usalama wao.
Comments
Post a Comment