WARATIBU WA M-MAMA WANOLEWA DODOMA










Wizara ya Afya kwa kushirikiana na Ofisi ya  Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI ) wametoa mafunzo  ya kuwajengea uwezo  maafisa habari ,waratibu na waelimishaji jamii ngazi ya Halmashauri na Mkoa wa Dodoma kuhusu  Mfumo wa m - mama .

Mafunzo hayo yamefanyika Julai 10,2024 katika  ukumbi wa Mikutano uliopo   Nashera Hoteli na kufunguliwa na Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt.Nelson Bukuru. 

Akitoa mafunzo hayo Mwezeshaji  wa Kitaifa wa m-mama Bi. Kambarage Makuri amesema lengo la mafunzo hayo  ni kuongeza uelewa kuhusu mfumo wa m-mama, kuwawezesha washiriki kuwa na ujuzi na uwezo wa kuhamasisha jamii katika Mfumo huo kwa ufanisi pamoja na kutengeneza mpango kazi wa utekelezaji. 

Kupitia mafunzo hayo wataalam hao wameweza kutengeneza Mpango Kazi wa Mkoa unaolenga kuwafundisha na kuwaelimisha viongozi wa ngazi zote pamoja na wananchi ili kuwa na uelewa wa pamoja  juu ya matumizi sahihi ya namba 115.

&&&

#dodomafahariyawatanzania 
#keroyakowajibuwangu

Comments

Popular posts from this blog

WALIMU WATAKIWA KUFUNDISHA UZALENDO SHULENI.

TRAMPA KANDA YA KATI WAFANYA KIKAO DODOMA

BARAZA LA MITUME NA MANABII WAMTEMBELEA MKUU WA MKOA WA DODOMA