RC SENYAMULE AHIMIZA WANADODOMA KUJITOKEZA KUPIGA KURA

 


Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary S. Senyamule akiwa kwenye foleni ya kupiga kura kwenye kituo cha Shule ya Msingi Dodoma Mlimani, Mtaa wa Salmini, Kata ya Tambukareli Jijini Dodoma leo Novemba 27, 2024





Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary S. Senyamule akitafuta jina lake kwenye orodha ya wapiga kura kwenye kituo cha Shule ya Msingi Dodoma Mlimani, Mtaa wa Salmini, Kata ya Tambukareli Jijini Dodoma.





Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary S. Senyamule akijaza karatasi za kupigia kura yake wakati wa zoezi la kupiga kura kwenye uchaguzi wa Serikali za Mitaa unaofanyika leo Novemba 27, 2024 




Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary S. Senyamule akitimiza haki yake ya kidemokrasia kwa kupiga kura kwenye uchaguzi wa Serikali za Mitaa katika Mtaa wa Salmini, Kata ya Tambukareli Jijini Dodoma.




Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma Bw. Kaspar K. Mmuya akipiga kura yake katika Mtaa wa Mathias, Kata ya Miyuji Jijini Dodoma kwenye uchaguzi wa Serikali za Mitaa unaofanyika leo Novemba 27, 2024




Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma akichovya wino kwenye kidole kidogo kama ishara ya kukamilisha haki yake ya kidemokrasia kupiga kura kuchagua viongozi wa Serikali ya mtaa wake leo Novemba 27, 2024




Meya Mstaafu wa Jiji la Dodoma Bw. Peter Mavunde, leo amejitokeza kupiga kura katika kituo cha Shule ya Msingi Dodoma Mlimani, Mtaa wa Salmini, Kata ya Tambukareli Jijini Dodoma kuchagua viongozi wa mtaa wake wakati wa zoezi la Uchaguzi wa Serikali za Mitaa lililofanyika leo Novemba 27, 2024





Na. Hellen M. Minja,

       Habari – DODOMA RS


Wito umetolewa kwa Wakaazi wa Mkoa wa Dodoma kufika katika vituo walivyojiandikishia kwa ajili ya kutimiza haki ya kidemokrasia kwa kushiriki kupiga kura kuchagua Viongozi wa Serikali za Mitaa yao pamoja na kulinda amani.

Hayo yamebainishwa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary S. Senyamule aliposhiriki zoezi hilo katika kituo chake alichojiandikishia Shule ya Msingi Dodoma Mlimani, Mtaa wa Salmini, Kata ya Tambukareli Jijini Dodoma mapema leo Novemba 27, 2024.

“Siku ya leo ni ya muhimu sana Dodoma kuwa salama. Tukumbuke kauli yetu ‘Uchaguzi salama kwa maendeleo ya Taifa letu’. Nitoe wito kuwa asikose mtu kwenda kupiga kura kwenye kituo alichojiandikishia na kila mmoja ahakikishe analinda usalama” Amesisitiza Mhe. Senyamule

Kadhalika, amewashukuru wana Dodoma wote kwa kuendelea kutunza amani na utulivu wakati wote tangu kuanza kwa mchakato wa Uchaguzi, wakati wa kampeni hadi leo hii  unapokwenda kutamatika.

Kwa upande wake Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma Bw. Kaspar K. Mmuya,  amepiga kura katika kituo alichojiandikishia Mtaa wa Mathias, Kata ya Miyuji, Jijini Dodoma na kutoa hamasa kwa wananchi kujitokeza kwa wingi kwani vituo vipo karibu na makaazi ili kutimiza haki ya kuchagua viongozi wanaowataka.

Miongoni mwa viongozi wastaafu wa Mkoa wa Dodoma aliyepata nafasi ya kushiriki zoezi hilo na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma ni Bw. Peter Mavunde (Meya mstaafu wa Jiji la Dodoma) ambapo ametoa hamasa kwa wanachi kujitokeza mapema, kwa wingi   kwenye vituo vya kupigia kura ili kutimiza haki yao ya msingi ya kuchagua viongozi watakaowafaa.


 “Serikali za Mitaa, Sauti ya Wananchi, Jitokeze Kushiriki Uchaguzi”


#kurayakosautiyako               

#ujanjanikupigakura               

#dodomatukotayarikupigakura

#mtiwangubirthdayyangu














Comments

Popular posts from this blog

WALIMU WATAKIWA KUFUNDISHA UZALENDO SHULENI.

TRAMPA KANDA YA KATI WAFANYA KIKAO DODOMA

BARAZA LA MITUME NA MANABII WAMTEMBELEA MKUU WA MKOA WA DODOMA