RAS MMUYA ATOA SALAMU ZA POLE KWA FAMILIA YA MAREHEMU MAGUO.
Na Sofia Remmi.
Habari-Dodoma Rs
Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma Bw.Kaspar K.Mmuya ametoa salamu za Pole kwa Familia na waombolezaji mbalimbali kufuatia kifo cha Mhe. Abdallah Maguo aliyekuwa Diwani na Mwenyekiti na Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa, aliyefariki tarehe 24 Februari 2025,katika hospitali ya Benjamin Mkapa wakati akipatiwa matibabu.
RAS Mmuya amewaombea faraja ya mwenyezi Mungu iwafikie familia,ndugu,jamaa na marafiki walioguswa na msiba huo.
Akizungumza na waombolezaji RAS Mmuya amesema marehemu Maguo alikuwa muadilifu aliyezingatia maadili ya kazi yake ya kuwatumikia wananchi wake wa Kata ya Mnenia wakati wote.
“ Jambo la msiba si jambo la kuzoeleka, na njia pekee ya Kumuenzi Maguo ni kuyaenzi mema yake ya wakati wote kipindi cha uhai wake.
Muda wa kuishi duniani ni mfupi sana tunapaswa kutenda mema wakati wote sio kwa ajili yetu,bali kwa ajili ya wote” Amesema Mmuya.
Aidha msiba huo umefanyika Katika Kijiji cha Mnenia kata ya Mnenia Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa tarehe 25 Februari 2025. Marehemu Abdallah Maguo ameacha Mjane Mmoja, watoto watatu na wajukuu Saba .Wote ni wa Mwenyezi Mungu,na kwake tutarejea.
#dodomafahariyawatanzania
#keroyakowajibwangu
Comments
Post a Comment