LISHE BORA : KICHOCHEO CHA MAENDELEO ENDELEVU KATIKA JAMII
Na Sofia Remmi.
Habari Dodoma RS
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe.Rosemary Senyamule, ameiasa jamii kuzingatia suala la lishe Bora kutokana na umuhimu wake.
Mhe Senyamule ametoa kauli hiyo wakati akiendesha kikao cha tathmini ya utekelezaji wa Mkataba wa Lishe kwa Kipindi cha Julai- Disemba 2024.
Kikao hicho kimefanyika Machi 28,2025 katika ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma (Manispaa ya Zamani).
"Lishe ni jambo muhimu, tukifanikiwa watu wakaelewa vizuri kuhusu lishe,wale vizuri,watu wakila vizuri,mengine yote yatakaa vizuri" Amesisitiza Mhe. Senyamule.
Awali akifungua kikao hicho, Mhe.Senyamule amesema
ni dhahiri kuwa, lishe bora katika jamii ni kichocheo cha maendeleo endelevu katika nyanja zote na hasa ya viwanda, afya, kilimo, elimu, biashara, uchumi.
“Athari za lishe duni au utapiamlo zitakapodhibitiwa au kutokomezwa ndipo malengo ya maendeleo katika nyanja hizi yataweza kufikiwa kwa ufanisi. Tafiti ya kidemografia ya mwaka 2022”
“Wataalam wetu kupitia tafiti mbalimbali walibaini afua kadhaa ambazo iwapo zitafanyiwa kazi zinaweza kubadili hali iliyopo kwa sasa. Afua hizo, ziliandaliwa mkakati wa utekelezaji kwa mfumo wa mkataba. Kama nilivyoeleza hapo awali.” Amesema Senyamule
Kwa upande wake Afisa Lishe Mkoa Bw.Ally Mvungi amesema Mkoa unafikia malengo yaliyotarajiwa katika Halmashauri zote kwa kufanya vizuri kwenye utekelezaji wa afua za lishe.
“Jamii kuhusishwa katika kupewa Elimu kuhusu matumizi ya vyakula vya asili vyenye virutubisho kwa Wingi ili kuhamasisha afya na lishe bora”amesema Mvungi.
Comments
Post a Comment