SERIKALI IMEJIPANGA KUPAMBANA NA DAWA ZA KULEVYA : WAZIRI GWAJIMA

 













Na; Happiness E. Chindiye 
Habari - Dodoma RS 

Serikali imejipanga vema kupambana na tatizo la dawa za kulevya kwa kuanzisha chombo mahsusi kijulikanacho kama Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA), ambacho pamoja na majukumu mengine ina jukumu la kupunguza madhara yatokanayo na matumizi ya dawa za kulevya, kuratibu na kusimamia masuala ya tiba na huduma za utengamao kwa waraibu wa dawa za kulevya Nchini ikiwemo nyumba za upataji nafuu. 

Hayo yamebainishwa na Waziri wa Mandeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Mhe. Doroth Gwajima wakati la Kongamano la Vijana lililo andaliwa mahususi kwa ajili ya elimu juu ya tatizo la dawa za kulevya lililofanyika ukumbi wa Mabele Jijini Dodoma.

“Mamlaka yetu ina jukumu la kutoa elimu sahihi kwa Umma juu ya athari za biashara na matumizi ya dawa za kulevya, kuhamasisha jamii kushiriki katika mapambano dhidi ya tatizo la dawa za kulevya. 

“Kwa hiyo tukio letu la leo linashabihiana kabisa na malengo na mikakati ya Serikali katika kuimarisha mapambano dhidi ya tatizo la dawa za kulevya. “ - Mhe. Gwajima 

Hata Hivyo, Mhe. Gwajima amewasihi Vijana  kuwa mabalozi wazuri wa utekelezaji wa majukumu ya Serikali dhidi ya tatizo la dawa za kulevya.

Kwa upande wake Kamishna Jenerali wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya(DCEA), Bw. Aretas Lyimo amewaasa vijana kuachana na  Matumizi ya dawa za kulevya  kwani yanazima ndoto na kuweza kuwaingiza kwenye matokeo mabaya, ikiwa ni pamoja na uraibu, vitendo vya ukatili, matatizo ya kiafya kama vile UKIMWI, Magonjwa ya Akili, Kifua Kikuu pamoja na Homa ya Ini. 

Kongamano hili ni mojawapo ya matukio yaliyopangwa kufanyika kuelekea Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Kupiga Vita  Dawa za Kulevya Duniani ambayo yanatarajiwa kufanyika Juni 26,2025 Jijini hapa.



#drugday2025
#wekezakwenyekinganatibadhidiyadawazakulevya










Comments

Popular posts from this blog

WALIMU WA HALMASHAURI YA JIJI LA DODOMA WATAKIWA KUTIMIZA WAJIBU WAO

WALIMU WATAKIWA KUFUNDISHA UZALENDO SHULENI.

‘WANAWAKE NA SAMIA’ 3000 MKOA WA DODOMA KUPATA MAFUNZO VETA