Posts

Showing posts from January, 2026

RC DODOMA AKAGUA MIRADI YA ELIMU KATIKA SHULE YA MSINGI MAYAMAYA, AAGIZA WANAFUNZI WOTE KUREJEA SHULENI

Image
  Na Mwandishi wetu Habari - DODOMA RS  Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Mhe. Rosemary Senyamule, tarehe 14, Januari 2026 amefanya ziara ya kikazi katika Shule ya Msingi Mayamaya iliyopo Wilayani Bahi kwa lengo la kukagua utekelezaji wa miradi ya miundombinu ya elimu. Akiwa shuleni hapo, Mhe. Senyamule amesisitiza wajibu wa watendaji wa kata na vijiji kuhakikisha kuwa ndani ya wiki hii wanafunzi wote wanarejea shuleni kuendelea na masomo yao. “Ninaagiza watendaji wa kata na vijiji kupita kaya kwa kaya kuhakikisha kila mwanafunzi anarejea shuleni. Hatupaswi kuwa na mtoto anayebaki nyumbani wakati wenzake wakiendelea na masomo, kwani hali hiyo inarudisha nyuma maendeleo ya elimu,” alisema Mhe. Senyamule. Kwa upande wake  Mkuu wa Wilaya ya Bahi, Mhe. Joachim Nyingo, amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa uwekezaji mkubwa alioufanya katika Mkoa wa Dodoma, hususan Wilaya ya Bahi na Kata ya Zanka, unaolenga kuboresha sekta ya elimu na maen...

WAZIRI WA AFYA (MALAWI) NA UJUMBE WAKE WAFIKA DODOMA KUJIFUNZA UTEKELEZAJI WA M-MAMA

Image
  Ujumbe kutoka nchini Malawi ukiongozwa na Waziri wa Afya wa nchi hiyo  Mhe. Madalitso Baloyi wakiwa kwenye ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule kwa lengo la kujitambulisha kabla ya kuanza ziara kuelekea Zahanati ya Chalinze Wilayani Chamwino, Januari 14, 2026, wkwa ajili ya kujifunza utekelezaji wa Mpango wa dharura wa kuokoa maisha ya kina mama wajawazito na watoto wachanga (M-MAMA) ikiwa ni siku ya pili ya ziara yao Nchini, katika Mkoa wa  Dodoma. Waziri wa Afya wa Malawi  Mhe. Madalitso Baloyi na Ujumbe wake wakiwa kwenye ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule kwa lengo la kujitambulisha kabla ya kuanza ziara kuelekea Zahanati ya Chalinze Wilayani Chamwino, Januari 14, 2026, kwa ajili ya kujifunza utekelezaji wa Mpango wa dharura wa kuokoa maisha ya kina mama wajawazito na watoto wachanga (M-MAMA) ikiwa ni siku ya pili ya ziara yao Nchini, katika Mkoa wa  Dodoma. Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule akizungumza ...

UGENI WA AFYA MALAWI WATUA DODOMA KUJIFUNZA MFUMO WA M-MAMA

Image
  Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Wizara ya Afya, leo Januari 13, 2026, imepokea ugeni kutoka nchini Malawi. Ugeni huo, ukiongozwa na Waziri wa Afya wa Malawi, Mhe. Madalitso Baloyi, umetembelea Hospitali ya Rufaa ya Dodoma kwa lengo la kujifunza na kujionea utekelezaji wa mfumo wa usafiri wa dharura kwa mama wajawazito, akina mama waliojifungua hadi siku 42, pamoja na watoto wachanga wenye umri wa siku 0–28 (M-MAMA). Aidha, ugeni huo ulikutana na viongozi wa sekta ya afya pamoja na wadau mbalimbali ili kubadilishana uzoefu na kujifunza mbinu bora za utoaji wa huduma za afya. Ujio wa ugeni huu unalenga kuimarisha ushirikiano wa kiafya kati ya Malawi na Tanzania, pamoja na kuchochea ubadilishanaji wa uzoefu miongoni mwa wataalamu wa afya. Katika ziara hiyo, Mganga Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dkt. Thomas Rutachunzigwa, alishiriki kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma. #dodomafahariyawatanzania

WAZAZI/WALEZI WATAKIWA KUSIMAMIA MAANDALIZI YA KUWAPELEKA WATOTO SHULE

Image
  Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhe. Prof. Riziki Shemdoe akizungumza alipokua kwenye shule ya Sekondari Dkt. Samia wakati wa ziara ya kuangalia maandalizi ya kuwapokea wanafunzi wapya wa awali, msingi na sekondari kwenye shule ya msingi Iyumbu na shule ya sekondari Dkt. Samia za Jijini Dodoma Januari 12, 2026. Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule akizungumza alipokua kwenye shule ya Sekondari Dkt. Samia wakati wa ziara ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhe. Prof. Riziki Shemdoe kuangalia maandalizi ya kuwapokea wanafunzi wapya wa awali, msingi na sekondari kwenye shule ya msingi Iyumbu na shule ya sekondari Dkt. Samia za Jijini Dodoma Januari 12, 2026. Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhe. Prof. Riziki Shemdoe akielekea kwenye madarasa ya shule ya sekondari Dkt. Samia kukagua maandalizi ya kuwapokea wanafunzi ...