Posts

Showing posts from April, 2023

TBS YATOA VYETI 29 VYA UBORA KANDA YA KATI

Image
  Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma Bw. Ally Senga Gugu amewatunuku  Vyeti na Leseni wafanyabiashara na wazalishaji  ambao bidhaa zao zimethibitishwa Ubora wake  na Shirika la Viwango Tanzania (TBS) kwa wazalishaji wa kanda ya kati (Dodoma, singida na Tabora) pamoja na Iringa na kuwaasa wazalishaji kuhakikisha bidhaa zote zinazozalishwa viwandani zinazingatia kanuni bora za uzalishaji.   Hafla hiyo imefanyika leo tarehe Aprili 28,2023 katika Ukumbi wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma. "Kazi hii iliyofanywa na Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, kupitia TBS ni mwendelezo wa azma ya Serikali katika kuhakikisha wazalishaji wa bidhaa viwandani kama wadau muhimu wa maendeleo ya ubora na usalama wa bidhaa, wanazalisha bidhaa zinazokidhi matakwa ya Viwango vya ubora Kitaifa na kimataifa na kuhakikisha Watanzania wananunua  na kutumia bidhaa zenye ubora na ambazo ni salama kwa afya zao na mazingira    "Nitoe rai kwenu nyote ambao mmeshiriki kutimiza waji...

ITUMIENI KAMPENI YA HUDUMA YA MSAADA WA KISHERIA YA MAMA SAMIA - MAJALIWA

Image
  Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amewataka watanzania kuitumia kampeni ya Huduma ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia kutoa taarifa kuhusu uwepo wa watu, au vikundi vya watu ambao ama wanajihusisha na ukatili wa kijinsia hususan kwa watoto.   Ametoa wito huo leo Alhamisi (Aprili 27, 2023) alipozindua kampeni hiyo ambayo itatekelezwa kwa miaka mitatu kuanzia Machi, 2023 hadi Desemba 2025. Amesema kuwa kampeni hiyo itasaidia kuongeza uelewa wa sheria na upatikanaji haki, mifumo ya utoaji haki, masuala ya kisheria na haki za binadamu kwa kushirikiana na taasisi za serikali, asasi za kiraia na wadau wa maendeleo katika utoaji huduma kwa wananchi. “Kampeni hii pia  itasaidia kuboresha upatikanaji wa haki kwa watu wasiojiweza, hususani wanawake, watoto na makundi mengine yaliyo katika mazingira magumu. Vilevile, itachangia kuimarisha amani na utulivu, kuongeza kipato cha mmoja mmoja na kuleta utengamano wa kitaifa”. Amesema Ameongeza kuwa, faida nyingine ya kampeni hiyo...

KUELEKEA MAADHIMISHO YA MIAKA 59 YA MUUNGANO VIONGOZI WAKIROHO JIJINI DODOMA WAKUTANA KULIOMBEA TAIFA

Image
  Mkuu wa Mkoa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule ameshiriki maombi maalumu  ya kuliombea Taifa la Tanzania kuelekea maadhimisho ya miaka 59 ya Muungano yalioandaliwa na ofisi ya yake kwa kushirikiana na Kamati ya amani chini ya uongozi wa Sheikh Mustapha Rajab Sheikh wa Mkoa wa Dodoma.   Lengo la maombi hayo ni kumuombea afya njema Rais wa Jamuhuri ya muungano wa Tanzania Mhe Dkt. Samia Suluhu Hassan, kuombea Uchumi,  kupinga uhujumu uchumi, kukemea ukatili wa kijinsia na Ushoga, rushwa, ukatili kwa Watoto, Watumishi wa Serikali wa ngazi zote, Vyombo vya ulinzi na usalama, hali ya hewa, Makao makuu ya nchi na kuombea Muungano ili uendelee kudumu pamoja na  viongozi waasisi wa Muungano wa nchi ya Tanganyika na Zanzibar ambao ni Mwalimu Julius K. Nyerere na Abeid Amani Karume.   Maombi hayo yamefanyika leo tarehe 24/4/2023 walipokutana  viongozi mbalimbali wa kiimani na serikali na kuhudhuliwa na viongozi wa Serikali mio...

SENYAMULE AWAKABIDHI TIKETI ZA KUTALII MWAKINYO NA KUVESA

Image
Mkuu wa Mkoa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule ametoa tiketi za kufanya utalii katika jijini la Dodoma kwa wachezaji wa mchezo wa masumbwi bondia Hassan Mwakinyo na Mardochee Kuvesa Katembo raia wa Afrika kusini mara baada ya pambano lao litakalofanyika kesho tarehe 23/04/2023.   Pambano hilo la kimataifa limeandaliwa na Kampuni ya Lady in Red limelenga kuchangia   upatikanaji wa taulo za kike zisizopungua 40,000 ambazo zitawasadia kusoma kwa uhuru na kuweza kutimiza ndoto zao.    Senyamule ameyasema   hayo leo tarehe 22/4/2023 alipokutana na  mabondia hao na kuwakabidhi tiketi hizo  katika  Ukumbi wa Mkapa Jijini Dodoma. Senyamule amesema amefurahishwa na pambano kufanyika katika uwanja wa Jamhuri Mkoa Dodoma kwakuwa ni fursa muhimu ya kutangaza utalii na kusisitiza kuwa mabondia hao watatembelea hifadhi  mbalimbali ambazo ni  Mkungunero, Kolo, Ngorongoro na Tarangire na kutoa rai kwao kuwa  mabalozi wazuri nje na ndani ya Mkoa wa...

DODOMA KUNUFAIKA NA MRADI WA BOOST WENYE THAMANI YA BILIONI 10.6

Image
Kiasi cha   Shilingi Billioni 10.6 zimetengwa kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya Idara ya Elimu katika kipindi cha Januari  hadi Aprili 2023  kupitia mradi wa Boost kwa Mkoa wa Dodoma. Akifungua kikao hicho leo 21/04/2023, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule amewataka wasimamazi wa mradi hiyo  kusimamia kwa umakini mkubwa ili kuhakikisha majengo yanayo kusudiwa yanakamilika kwa wakati ili kuleta tija ya Mhe Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan aliyokusudia ya wanafunzi kusoma kwenye mazingira mazuri. Akizungumza na Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi, Maafisa Elimu, Maafisa Manunuzi na Wahandisi katika ukumbi wa Jengo la Mkapa jijini Dodoma, Senyamule amesema fedha hizo zimelenga kujenga miundombinu mbalimbali ikiwa ni pamoja na Ujenzi wa shule mpya za msingi 16 zitakazogharimu kiasi cha billioni 6.1, idadi ya vyumba vya madarasa 153 kwa kiasi shilingi Milioni 3,519,000. madarasa ya mfano elimu ya awali 16  yatakayogharimu kiasi cha shilingi milioni 508,800...

BILIONI 17 KUJENGA MNARA WA MASHUJAA NA UKUMBI

Image
Mkuu wa Mkoa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule amewapongeza  wana Dodoma kwa miaka 59 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ikiwa ni wiki ya maadhimisho sherehe hiyo na kuwataka vijana kuchangamkia fursa zinazoendelea kujitokeza jijini Dodoma. Senyamule ameyasema hayo leo alipotembea mradi wa ujenzi wa uwanja na mnara wa mashujaa katika eneo  la Mji wa Serikali Mtumba. ‘’Leo nina furaha kubwa kwa kuwa maelekezo ya Mhe Rais wetu Dkt. Samia Suluhu Hassan aliyoyatoa hapa jijini Dodoma tarehe 25 Julai, 2022 wakati wa maadhimisho ya kumbukumbu ya mashujaa yanaendea kutekelezwa na hii ni heshma kubwa kwetu wana Dodoma kwakuwa Mradi huu kuanza kutekelezwa kwa vitendo. Kupitia mradi huu, tunakwenda kuweka alama nyingine muhimu itakayopendezesha Mkoa wetu ambao ndio Makao Makuu ya Nchi yetu, pia  wanadodoma watanufaika kiuchumi na kijamii” Senyamule amefafanua  Aidha Mhe. Senyamule amewataka wakandarasi kuhakikisha wanatekeleza ujenzi wa mradi kwa hadhi kubwa na sifa nzu...