Posts

Showing posts from August, 2023
Image
  Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma Bw. Ally Gugu amefungua kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mradi ya uboreshaji wa huduma za afya ya uzazi na mtoto kwa Halmashauri ya Mpwapwa kilichofanyika leo tarehe 30 agosti 2023 katika ukumbi wa Hospitali ya Mpwapwa. Akizungumza katika kikao hicho Gugu amesema ni vyema kuzingatia mikakati iliyopo ili miradi ambayo ipo katika Halmashauri inakamilika kwa wakati na kuleta manufaa kwa wananchi. Amesema wataalamu wanatakiwa kuhakikisha miradi inatekelezwa na kusimamia kwa ubora kama serikali ilivyokubaliana na wadau wa KOFIH kwa lengo la kuhakikisha miradi hiyo inakamilika kwa wakati kama ilivyokubalika. “Kila Halmashauri ni lazima kuhakikisha vifaa tiba vinanunuliwa kwa wakati na wananchi  waweze kuvitumia, kunufaika na kuongeza tija kwa wananchi. “Serikali yetu inatoa kipaumbele kwenye suala la afya hivyo tunaona Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ametoa kipaumbele kwenye suala la afya ya mama na mtoto hiv...

EAST AFRICA BICYCLE TOUR' WAAGWA DODOMA

Image
Waendesha baiskeli wanaozunguka nchi za Afrika Mashariki ambao waliwasili jana Mkoa wa Dodoma nchini Tanzania, wameagwa rasmi leo Agosti 29 na uongozi wa Mkoa ili kuendelea na safari yao kuelekea nchini Burundi. Akiwaaga waendesha baiskeli hao, Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma  Bi. Coletha Kiwale, amewapongeza na kuwasisitiza kuimarisha umoja. "Hongereni kwa kupumzika Dodoma. Nimefurahi kuanzisha Tour kama hii ambayo inawakutanisha wote wana Afrika Mashariki, inaimarisha amani na umoja hivyo tunatakiwa kuendeleza utaratibu huu. Tunashukuru pia kwa ajenda yenu ya utunzaji wa mazingira kwani Dunia nzima sasa inahamasisha hilo. Nawaomba muendelee kuimarisha umoja huu" Amesema Bi. Kiwale. Aidha, waendesha baiskeli hao wameshukuru kwa mapokezi mazuri waliyoyapata kwenye Mkoa wa Dodoma na wameahidi kuendelea kusambaza amani na kusafisha mazingira hasa kwa kuwafundisha watoto umuhimu wa utunzaji wa mazingira. Safari ya waendesha baiskeli hao ilianzia katika Jiji la Kampala nchini ...

WAENDESHA BAISKELI WAWASILI DODOMA - TANZANIA

Image
                                           Kikundi cha waendesha baiskeli kinachojulikana kama East Africa Bicycle Tour, leo Agosti 28 kimewasili nchini Tanzania katika Mkoa wa Dodoma wakitokea Jiji la Kampala nchini Uganda wakiwa kwenye safari ya kuzunguka nchi za Afrika Mashariki.  Waendesha baiskeli hao wapatao 22 wakiwa ni muunganiko kutoka nchi za Afrika Mashariki zikiwemo Uganda, Kenya, Burundi, Tanzania, Congo na Rwanda, wamepokelewa na Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma Bi. Coletha Kiwale ambaye amewapongeza kwa lengo la safari yao. "Nawapongeza kwa Tour hii mnayoifanya ambayo lengo lake ni kuleta umoja kwa Afrika Mashariki pia kuhimiza utunzaji wa mazingira kwa ajili ya kuwa na utoshelevu wa chakula, niwatakie safari njema huko mnapoelekea" Bi. Kiwale amesema Bw. John Balongo ambaye ndiye kiongozi wa msafara huo ameelezea lengo kuu la safari yao. " Lengo kuu la saf...
Image
  Katibu Tawala Msaidizi (Uchumi na Uzalishaji) Bi. Aziza Mumba leo tarehe 28 Agosti ,2023  amemwakilisha  Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma Bw. Ally Gugu kufungua mafunzo kwa Watumishi wa Mkoa na Halmashauri zote za Mkoa wa Dodoma kuhusu Mfumo Mpya wa Manunuzi NEST. Bi Mumba ametoa wito kwa watumishi hao kuhakikisha wanashiriki kikamilifi na kusikiliza kwa makini ili kuyafanyia kazi kwa vitendo mafunzo hayo kuelekea utekelezaji wake unaotarajiwa kuanza tarehe 01/10/2023 kupitia mfumo huo ambao utaanza kufanya kazi rasmi Akifungua mafunzo hayo kwa Watumishi katika ukumbi wa Mkutano Ofisi ya Mkuu wa Mkoa amesema lengo la kufundishwa Mfumo huo  mpya wa Manunuzi  ni mbadala wa mfumo wa TANePS uliokuwa ukitumika awali. Amesema mfumo huo mpya umejengwa na kusimamiwa na Watanzania, umepunguza changamoto nyingi na utaondoa kazi kubwa kwa maafisa Manunuzi kwani Mchakato wa Manunuzi utaanzia kwa idara tumizi.  Aidha, Katibu Tawala Msaidizi huyo amesema kuwa matumizi ya M...
Image
  Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe Rosemary Senyamule leo tarehe 16 Agosti 2023 amefanya kikao kazi na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa na Wakuu wa Wilaya za Dodoma katika ukumbi wa Mkapa Jijini Dodoma Pamoja na mambo mengine kikao hicho pia kimejadili mikakati ya kuhamasisha uzalishaji wa mazao ya kimkakati na upatikanaji wa masoko katika Mkoa wa Dodoma.
Image
  Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe Rosemary Senyamule leo tarehe 13 Agosti 2023 amefunga sherehe ya Wiki ya Jamhyatul Akhlaaqul Islaam (JAI) iliyoanza tangu tarehe 07 Agosti 2023 katika viwanja ya Nyerere Square Jijini Dodoma. Akizungumza na wana JAI Senyamule amesema shughuli au kazi zinazofanywa na JAI ni zenye thamani ya juu kwa wananchi na zimetukuka mbele za mwenyezi Mungu. “Kazi za JAI hazina ubaguzi wala upendeleo wa kabila, rangi, jinsia wala dini hata itikadi za siasa bali wanachoangalia ni kutoa huduma na kutarajia malipo kutoka kwa Mwenyezi Mungu. “Kama mnavojua kuwa Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imefungua milango ya ushirikiano baina ya Serikali na Sekta Binafsi kwa ajili ya maendeleo endelevu ya wananchi ikiwemo taasisi za kidini” amesema Senyamule. Naye sheikh Ally Kanda kiongozi na Amiri wa JAI wa Mkoa wa Dodoma amesema JAI ilianziwa mwaka 2008 na lengo kuu ni kutoa huduma za kimatibabu kwa ...