Posts

Showing posts from December, 2023
Image
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule leo Desemba 21, 2023 amekabidhi zawadi kwa niaba ya Wanawake na Samia Geita kwa Mkurungenzi wa STAMICO Dr. Venance Mwasse kwenye Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma jengo la Mkapa Jijini Dodoma.  

MAKUTANO YA BARABARA YA KONGWA - MPWAPWA KUJENGWA

Image
Bodi ya Barabara Mkoa wa Dodoma leo Desemba 20, 2023 imefanya kikao chake cha kwanza mwaka 2023/24 kuwasilisha, kujadili na kushauri juu ya utekelezaji wa miradi ya Barabara za Mkoa kwa kipindi cha Julai hadiNovemba. Kikao hicho kilichoongozwa na Mwenyekiti wake Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule, kimefanyika kwenye ukumbi wa ofisi ya Mkoa jengo la Mkapa Jijini Dodoma  Katika kikao hicho, Mwenyekiti amewasilisha taarifa ya bajeti ya jumla ya Mkoa kwenye ujenzi wa miundombinu ya Barabara na kuwataka wajumbe kwa niaba ya wananchi kufanya maendeleo ili kuinua Uchumi kulingana na maendeleo yaliyopatikana. "Mkoa umepata jumla ya shilingi Bilioni 230.29 kutekeleza miradi ya Barabara kwa kipindi cha miaka mitatu ambapo TANROADS wamewezeshwa kutengeneza Barabara zenye jumla ya urefu wa Km 9248.12, TARURA wamewezeshwa kutengeneza Barabara zenye urefu wa jumla ya Km 7540.9 ambapo jumla wote wamepatiwa kiasi cha Shilingi Bilioni 593 na Milioni 69. " Utekelezaji huu wa miradi...

WATUMISHI WA UMMA WATAKIWA KUACHA LUGHA ZA MAUDHI NA MATUSI - DODOMA

Image
  Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi  (CCM ) Mkoa wa Dodoma chini ya Mwenyekiti  Ndg. Alhaj Adam Kimbisa Leo tarehe 19 Disemba 2023 imekutana kwa kikao cha kawaida cha kujadili hali ya kisiasa ,uchumi na mambo mbalimbali yanayohusu ustawi ndani ya Mkoa huo kwa kipindi cha Januari hadi Disemba 2023. Akizungumza na Waandishi wa Habari baada ya kikao hicho   Katibu wa Siasa na Uenezi Mkoa wa Dodoma Ndg.Jawadu Mohamed  amesema Halmashauri hiyo imeelekeza kuwa  Watumishi wote wa serikali ndani ya Mkoa huo kuendelea kutoa huduma bora kwa wananchi, kusikiliza kero pamoja na kutotoa lugha za maudhi na matusi kwa wananchi.  " Halmashauri kuu imeelekeza kwa Watumishi wote wa serikali ndani ya Mkoa wa Dodoma kuendelea kutoa huduma bora kwa wananchi, kusikiliza kero lakini kutotoa lugha za maudhi na matusi kwa wananchi " Amesema Ndg.Mohamed Ndg.Mohamed amesema Halmashauri hiyo imeazimia kwa kauli moja ya kumpongeza Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania...

"WAHITIMU TUMIENI ELIMU ZENU KUONGEZA TIJA SERIKALINI " RC SENYAMULE .

Image
Serikali imeahidi kuendelea Kushirikiana na Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM)Tawi la Dodoma katika kutatua changamoto mbalimbali kwa kuwa na wafanyakazi wenye ujuzi na weledi wa kutosha kuhudumia Watanzania. Kauli hiyo imetolewa  na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe.Rosemary Senyamule wakati akitoa hotuba yake kwenye Mahafali ya 49 ya Chuo cha IFM yaliyofanyika Disemba 16,2023 katika Ukumbi wa Mikutano wa St.Gaspar Jijini Dodoma. "Serikali inaahidi kuendelea Kushirikiana na Chuo cha Usimamizi wa Fedha katika kutatua changamoto mbalimbali, lengo ni kuhakikisha kuwa chuo kinakuwa kwanza wafanyakazi wakutosha wenye ujuzi na weledi kutosha kuhudumia Watanzania pili kuwa na miundombinu ya kutosha  kuendelea kuhudumia Wanafunzi waliojiunga katika chuo hicho na pia chuo kuendeleza majukumu yake kwa ufanisi". Aidha ,Mhe.Senyamule amewataka wahitimu na Chuo kwa ujumla kujitathmini juu ya elimu iliyotolewa na waliyoipata kuona ni namna gani inatumika kuongeza tija Serikalini na hata katika so...

TIMU YA ITIFAKI YATAKIWA KUTAMBUKIWA NA VIONGOZI WAO

Image
TIMU YA ITIFAKI YATAKIWA KUTAMBULIWA NA VIONGOZI WA Vijana wanaosimamia Itifaki kwenye dhifa mbalimbali za Kiserikali na hata za Taasisi binafsi wametakiwa kujitambulisha kwenye ofisi zao ili waweze kutambulika na kutumika kwa ajili ya kusimamia taratibu na ustaarabu wakati wa shughuli tofauti tofauti zinazotekelezwa Mkoa wa Dodoma na Mikoa mingine pia pindi huduma yao inapohitajika. Hayo yameelezwa Leo Desemba 15, 2023 na Mhe. Rosemary Senyamule wakati akifungua mafunzo siku tatu yanayotolewa kwa timu ya huduma ya Itifaki yanayofanyika kwenye ukumbi wa Chuo kikuu cha Mipango kilichopo Jijini Dodoma. "Nimetiwa Moyo na vijana hawa kwa kuweza kuhudhuria mafunzo haya. Dodoma ikiwa ndio makao makuu ya nchi, Kuna takribani ofisi 100 za Serikali hapa hali inayopelekea kuwa na matukio mengi yenye uhitaji wa huduma hii. Kumekua na changamoto kwenye suala la usimamizi wa Itifaki kwenye dhifa mbalimbali. "Mafunzo haya yatawasaidia huko muendapo na nitoe Wito kwenu, baada ya maf...

MAAFISA ELIMU KATA WANOLEWA KUPANDISHA UFAULU.

Image
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule amewaelekeza Maafisa Elimu Kata wa Halmashauri zote 8 za Mkoa huo kuhakikisha wanatekeleza mpango Mkakati wa Elimu wa Mkoa ifikapo mwishoni mwa mwaka 2024. Maelekezo hayo yametolewa tarehe 14/12/2023 katika ukumbi wa mikutano wa Shule ya Msingi St. Gaspal Miyuji Jijini Dodoma ulipofanyika Mkutano kazi. Mkutano huo uliwajumuisha Maafisa Elimu Kata wote wa Mkoa wa Dodoma kwa dhumuni la kuinua ubora wa Elimu na Ufaulu wa Mkoa wa Dodoma. "Nawaagiza muende mkatekeleze mpango Mkakati wa Mkoa na ifikapo mwisho wa mwaka 2024 Mkoa uwe na Ufaulu ubora kulingana na malengo yaliyowekwa kwenye mpango Mkakati wa Elimu wa Mkoa kwa mwaka 2024".Ameelekeza Mhe.Senyamule Pia ,Mkuu wa Mkoa huyo amewaagiza Maafisa Elimu hao kuhakikisha Kila Mwanafunzi aliyechaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza kwa muda uliopangwa kwa kushirikiana na watendaji wengine wa ngazi ya Kijiji na kata. "Hali ya uripoti wa kidato cha kwanza kwa mwaka 2023 haikufi...

KONGWA KUNUFAIKA NA MABINGWA WA MACHO

Image
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule ametembelea na kuzindua kambi ya madaktari Bingwa wa macho inayofanyika katika hospitali ya Wilaya ya kongwa, ambapo dhamira kuu ya kuwepo kwa kambi hiyo ni kuwasaidia wananchi kujua hali za kiafya za macho yao na hizo zinatolewa pasi na gharama zozote. Mhe. Senyamule amesema kuwa Mkoa wa Dodoma ni miongoni mwa Mikoa inayotekeleza mradi wa Macho Yangu unaotekelezwa na shirika lisilo la kiserikali la` Sightsavers` linalojishughulisha na utoaji wa huduma za macho. “Shirika hili linajishughulisha na utoaji wa huduma za macho ikiwepo upimaji wa miwani, pamoja na hayo shirika litasomesha madktari wasaidizi wa macho wawili na wauguzi sita pia litanunua baadhi ya vifaa vya macho na kusaidia kuundwa kwa mabaraza ya watu wenye ulemavu na kuwezesha huduma za kliniki tembezi za macho kama hii iliyozinduliwa leo,’’ Mhe. Senyamule Hatahivyo licha ya manufaa yanayopatikana kutokana na uwepo wa madaktari hao Mhe. Senyamule amesema miongoni mwa cha...