SERIKALI IMEJIZATITI KULETA MAENDELEO KWA KUIMARISHA MAZINGIRA YA UWEKEZAJI NA BIASHARA

Na. Happiness E. Chindiye Habari - Dodoma RS Serikali ya Awamu ya Sita, chini ya Uongozi madhubuti wa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imejizatiti kuleta maendeleo edelevu katika taifa la Tsnzania, ikiwemo kuboresha na kuimarisha mazingira ya uwekezaji na biashara Nchini. Hayo yamebainishwa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary S. Senyamule wakati akifunga maadhimisho ya kitaifa ya udhibiti wa bidhaa bandia Duniani yaliyofanyika katika ukumbi wa Mabele Jijini Dodoma. Tarehe 25.06.2025. “Kupitia uwezeshaji wa Serikali kwa wananchi waliojiunga kwenye vikundi na kupatiwa mikopo katika ngazi mbalimbali, zikiwemo Mikoa na Wilaya, vikundi vya uzalishaji vinaendelea kupata nguvu ya kutengeneza bidhaa zilizo halisi na bora, baada ya kupatiwa mafunzo ya ujasiriamali kutoka SIDO, TBS, BRELA na FCC. “Serikali kuendelea kuiamini na kuiwezesha Tume ya Ushindani kusimamia usalama wa soko, utimamu ...