Posts

PBZ WAMTEMBELEA KATIBU TAWALA MKOA WA DODOMA

Image
  Na.Sofia Remmi. Habari-Dodoma Rs Uongozi wa Bank ya PBZ umemtembelea Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma  Bw. Kaspar K. Mmuya ofisini kwake jengo la Mkapa Jijini Dodoma,mapema Februari 19,2025. Lengo la ziara hiyo ni kusalimia na  kuzungumza kuhusu fursa mbalimbali za kiuchumi zilizopo katika Mkoa wa Dodoma. Uongozi huo uliambatana na Meneja wa Benki ya PBZ Dodoma Bi. Mwanaharusi Ally na Afisa Mahusiano Abdul Khamis. #dodomafahariyawatanzania. #keroyakowajibuwangu.

MTI WANGU, BIRTHDAY YANGU FEBRUARI YAFANYIKA NZUGUNI

Image
  Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma Bw. Kaspar Mmuya, akizungumza umuhimu wa kupanda miti wakati wa hafla ya kampeni ya Mti wangu Birthday yangu kwa mwezi Februari iliyofanyika kwenye viwanja wa Nanenanae, Nzuguni Jijini Dodoma Februari 18, 2025 Mwenyekiti wa Taifa wa Chama cha Utunzaji Mazingira na Ufugaji wenye Tija Bw. Jeremia John Wambura ambaye ni moja ya mdau aliyealikwa kwenye hafla ya kampeni ya Mti wangu Birthday yangu kwa mwezi Februari akizungumza kwenye viwanja wa Nanenanae, Nzuguni Jijini Dodoma Februari 18, 2025  Afisa TEHAMA kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma ambaye pia ni mzaliwa wa Februari Bi Grace Moshi akizungumza kwa niaba ya wazaliwa wote wakati wa hafla ya kampeni ya Mti wangu Birthday yangu kwa mwezi Februari iliyofanyika kwenye viwanja wa Nanenanae, Nzuguni Jijini Dodoma Februari 18, 2025 Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma Bw. Kaspar Mmuya, akipanda mti wakati wa hafla ya kampeni ya Mti wangu Birthday yangu kwa mwezi Februari iliyofanyika kwenye viwanja wa Na...

RC SENYAMULE ATOA MAELEKEZO KWA TRC DODOMA SUALA LA FOLENI

Image
  Na; Happiness E. Chindiye         Habari - Dodoma RS Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary S. Senyamule leo  Februari 17,2025 ametembelea Stesheni ya SGR  ya Samia Suluhu Hassan iliyopo Mkonze  Jijini Dodoma kujionea namna huduma zinavyotolewa, hususani wakati wa kushuka abiria. Lengo la ziara hiyo ni kutatua changamoto zilizoibuliwa na abiria wanaoshuka eneo hilo na kukumbana na adha ya foleni inayotokana na uwepo wa mageti machache ya kuhakiki stakabadhi za malipo ya ushuru wa vyombo vya moto vinavyotoka katika Stesheni hiyo. Akizungumza na Uongozi wa TRC Dodoma, baada ya abiria kushuka majira ya saa 07;25 na kujionea hali halisi,Mhe. Senyamule ametoa maelekezo haya  “Rais wetu Dk. Samia Suluhu Hassan, ameleta SGR, ni jambo zuri sana lakini sasa tumekuwa tukipokea malalamiko kutoka kwa watumiaji wa Stesheni hii kuhusu kero ya msongamano wa magari unaosababishwa na idadi ndogo ya mashine za kusoma tikeketi za magari wakati wa kutoka. N...

WAKULIMA 40,000 WA MTAMA KUNUFAIKA NA MRADI WA CSAP DODOMA

Image
  Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule alipokua akizungumza na Balozi wa Ireland Nchini Tanzania Bi. Nicola Brennan, (hayupo pichani) ofisini kwake Jengo la Mkapa Jijini Dodoma leo Februari 17, 2025 kuhusu Mradi wa  ‘Climate Smart Agriculture Project (CSAP)’ wenye lengo la kuwanufaisha wakulima wa zao la Mtama .  Balozi wa Ireland Nchini Tanzania Bi. Nicola Brennan, akizungumza na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule (hayupo pichani) alipomtembelea ofisini kwake Jengo la Mkapa Jijini Dodoma leo Februari 17, 2025 kuzungumzia utekelezaji wa Mradi wa  ‘Climate Smart Agriculture Project (CSAP)’ wenye lengo la kuwanufaisha wakulima wa zao la Mtama .  Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule na Balozi wa Ireland Nchini Tanzania Bi. Nicola Brennan pamoja na wajumbe wengine walioambatana na Balozi huyowakizungumza kuhusu Mradi wa  ‘Climate Smart Agriculture Project (CSAP)’ wenye lengo la kuwanufaisha wakulima wa zao la Mtama Mkoa wa Dodoma...

DODOMA YAPO MADINI YA KUTOSHA"-RC SENYAMULE.

Image
  Na Sofia Remmi. Habari-Dodoma Rs. Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule ameyasema hayo mara baada ya kutembelea kiwanda cha Kuchenjua Mawe ya Shaba kwenda Kwenye Shaba halisi. Ziara hiyo iliyofanyika leo tarehe 16 Februari 2025 katika Mtaa wa Nala, Kata ya Nala, iliandaliwa na Waziri wa Madini Mhe. Anthony Mavunde. Akizungumza mara baada ya kutembelea kiwanda hicho Mhe. Senyamule Amesema tunaendelea kufurahi kuona mambo mazuri yanayoendelea kutokea katika Mkoa wetu kwa kuongezeka kiwanda ambacho vijana wengi watanufaika nacho. “Hii ni moja ya fursa ambayo vijana wengi watanufaika nayo kwa kupata ajira katika kiwanda hiki hivyo niendelee kupongeza Jitihada za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama yetu hodari Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan” “Madini ni kitu cha Mkakati Katika Mkoa wetu na yanazidi kuongezeka kwa wingi zaidi na Kuzidi kuifaharisha dodoma kwa kuwajali wawekezaji ambao wanaendelea Kuja na tunazidi kuwapokea maana bado Mkoa una madini Mengi na unahitaji w...

MAKAMU WA RAIS AIFARIJI FAMILIA YA MAREHEMU NKONDO

Image
  Na Sofia Remmi. Habari-Dodoma Rs Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango na mwenza wake Mama Mbonimpaye Mpango wameifariji familia na waombolezaji mbalimbali kufuatia kifo cha Bw. Johnson Nkondo aliyekuwa Msaidizi wa Ofisi Mkuu - Ofisi ya Makamu wa Rais aliyefariki tarehe 13 Februari 2025 katika Hospitali ya Benjamini Mkapa mkoani Dodoma wakati akipatiwa matibabu.   Makamu wa Rais na Mwenza wake wametoa faraja hiyo walipowasili katika makazi ya familia ya Marehemu Johnson Nkondo eneo la Veyula Mkoani Dodoma leo tarehe 16 Februari 2025.   Akizungumza na waombolezaji, Makamu wa Rais amesema marehemu Nkondo alikuwa muadilifu aliyezingatia maadili ya Utumishi wa Umma na taratibu za kiofisi wakati wote wa utumishi wake. Amesema ni vema kumuenzi marehemu Nkondo kwa kujifunza namna alivyojitolea kulitumikia Taifa kwa uadilifu mkubwa pamoja na kuhakikisha kila mmoja anatimiza wajibu wake vema, kuishi vema na ndugu, majirani na marafiki.   ...

WANUFAIKA WA TASAF DODOMA, WATAKIWA KUTUMIA MIRADI YA MAENDELEO KUJIONGEZEA KIPATO.

Image
  Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule, akizungumza na wanufaika wa Mpango wa kusaidia Kaya Masikini Nchini (TASAF) juu ya ajira nyepesi za kujiongezea kipato alipofanya ziara ya kutembelea na kuzungumza na wanufaika hao katika Kata ya Makutupora, Jijini Dodoma leo Februari 14, 2025. Katibu Tawala Wilaya ya Dodoma Mjini Bi. Sakina Mbugi kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Mjini Mhe. Jabir Shekimweri akizungumza na wanufaika wa Mpango wa kusaidia Kaya Masikini Nchini (TASAF) wakati wa ziara ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule kutembelea na kuzungumza na wanufaika hao katika Kata ya Makutupora, Jijini Dodoma leo Februari 14, 2025. Mnufaika wa Mpango wa Kusaidia TASAF Bi. Ester Chitojo, Mkazi wa Mchemwa Jijini Dodoma, ambaye amefanikiwa kujenga nyumba kwa fedha za TASAF akisimulia safari yake ya mafanikio mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule pindi alipomtembelea nyumbani kwake wakati wa ziara yake leo Februari 14, 2025 Nyumba ya Mnufaika wa...