Posts

Showing posts from July, 2023
Image
  Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule amesema Mkoa wa Dodoma kwa kushiriana na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Singida wamejipanga vizuri katika kuhakikisha vijana na watu mbalimbali wanapata fursa ya kupata Elimu kupitia maonyesho ya Wakulima na wafugaji (Nananane). Senyamule ameyasema hayo leo julai 31/2023 Ofisini kwake Jengo la Mkapa alipozungumza na waandishi wa Habari kuhusu Sherehe na Maonyesho hayo yanayotarajiwa kuanza  Agosti mosi na kilele chake ni Agosti 8 mwaka huu katika viwanja vya Nane nane Nzuguni Jijini Dodoma.  "Katika maonyesho hayo kutakuwa na Teknolojia mbalimbali za kuongeza tija na faida katika mnyororo wa thamani, wadau watapata fursa za kubaini Teknolojia zitakazoongeza tija katika uzalishaji. Senyamule amesema kuwa Dhamira ya maonyesho ya mwaka huu ni kuongeza hamasa ya uzalishaji wenye tija,kusambaza mbinu za kukabiliana na mabadiliko ya Tabianchi na uharibifu wa mazingira,kutoa ajira kwa vijana na kusambaza teknolojia za kisasa kat...
Image
  Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe Rosemary Senyamule  tarehe 28 Julai 2023 Ameshiriki kongamono la wadau  na wafanyabiashara wa NMB lililofanyika katika ukumbi wa loyal vilage Dodoma. Akizumgumza na wafanya biashara na wadau wa NMB Bank Senyamule amesema kuwakumbuka wadau na kuongea nao ni jambo la muhimu na kuashiria kuwa mnawakumbuka na kuwajali kama iliyopo kauli yenu ya NMB karibu yako hivi ninawapongeza kwa jambo hili jema.  Amesema wafanyabiashara wanamchango kubwa katika kukuza na kueneza kila huduma na kwa asilimia kubwa ya ulipaji kodi katika kazi na nafasi tunapaswa kuwajali na kuwaaminisha kwa Huduma bora. “Tunategemea mazingira mazuri ya Huduma kwa wateja wenu na kuzidi kuongea ufanisi katika kazi na kuweza kupewa uwezeshwaji kwa wafanya biashara. “Nimefurahi kukutana na wafanyabiashara hivo nitoe fursa kuzidi kuendeleza juhudi ya Mhe. Dkt.Samia Suluhu Hassan ameweka miundombinu mingi hivo tuchangamkia Fursa za wafanyabiashara kama nia na lengo ya Rais wetu ku...
Image
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma amesema Tanzania ni miongoni mwa nchi zenye amani duniani kutokana  na maono na utashi wa viongozi wakuu wa nchi. Akizungumza katika Ibaada ya shukrani na uzinduzi wa Kitabu cha Askofu Evance Chande wa Kanisa la Kalmel Assemblies of God Ipagala Dodoma leo Julai 30, 2023, Senyamule ametoa rai kwa jamii kuenzi na kudumisha amani iliyopo.  "Viongozi wetu Wakuu wanadhamira njema sana kwa ajili ya watanzania kupitia maneno na vitendo vyao, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ni kiongozi jasiri na mwenye upendo mkubwa, ameweza kuendeleza miradi ya kimkakati ikiwa ni pamoja na ujenzi wa Reli ya Kisasa na Ujenzi wa Bwawa la Mwalimu Nyerere" Senyamule amesisitiza. Amesema Mkoa wa dodoma una mengi ya kujivunia ikiwa ni pamoja na ujenzi wa Mji wa Serikali, Ujenzi wa Makao Makuu ya Mahakama na Ujenzi wa barabara za Mzunguko Senyamule amesisitiza kuwa Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan anagusa maisha ya mtu mmoja moja kwakuwa %60-70 ya watanzania ni wakulima hivyo kat...

KAMILISHENI MICHORO YA UJENZI WA SHULE YA SEKONDARI MPWAYUNGU KWA WAKATI - SENYAMULE

Image
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule ameagiza wakandarasi wanaotekeleza mradi wa ujenzi wa Shule Mpya ya Sekondari Mpwayungu iliyopo Wilayani Chamwino kukamilisha michoro ya ujenzi huo ili kuwezesha kazi nyingine kuendelea Mhe. Senyamule ametoa agizo hilo tarehe 30 Julai 2023 wakati wa ziara yake ya kikazi katika Wilaya hiyo katika Kata ya Mpwayungu ambapo ametembelea miradi kadhaa ikiwemo Ujenzi wa Shule hiyo, Mradi wa kupambana na Ujangili na biashara haramu ya Wanyamapori katika mfumo wa ikolojia wa hifadhi za Ruaha [WMA] katika kijiji cha Ndogowe na Mradi wa Kilimo cha Pamoja (BBT) Amesema kuwa iwapo michoro hiyo itakamilika kwa wakati itatoa fursa kwa wananchi kuendelea na zoezi la kuchimba msingi ndani ya wiki moja. Mhe. Senyamule ameelekeza Watendaji kuhakikisha wanasimamia kazi zinazo wahusu ikiwemo Uchimbaji wa msingi, kusogeza kokote ,vifusi vya mchanga ili mradi huo uweze kwenda kasi na kukamilika kwa wakati. " Natarajia kuona uchimbaji wa msingi umekamilika...

DODOMA YAONGOZA KWA WINGI WA MADINI YA AINA TOFAUTI

Image
  Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST) leo tarehe 28/07/2023 wamewasilisha taarifa ya utafiti wa Madini yanayopatikana nchini Tanzania huku Dodoma ikiongoza kwa kuwa na orodha ya madini ya aina nyingi. Akiwasilisha taarifa hiyo leo Meneja Jiolojia kutoka (GST) Bw. Maswi Solomon amesema kuwa utafiti huo umeonyesha miongoni mwa madini matano ya kimkakati madini manne yako katika Mkoa wa Dodoma. Amesema Mkoa wa Dodoma ni maarufu kwa upatikanaji wa miamba yenye madini ya lithium , chrysoprase , chuma, nikeli, urania na jasi. Aidha, taarifa hiyo imeonyesha kuwa kuna madini ya yoderite yanayopatikana Mlima wa Mautia Wilayani Kongwa na imebainika kuwa madini haya hadi sasa yanapatikana Tanzania pekee duniani kote. Akipokea taarifa ya utafiti huo Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule amesema taarifa hiyo itakuwa ni nyenzo itakayosaidia   kuutangaza Mkoa wa Dodoma kimkakati husasan katika uwekezaji wa sekta ya madini. “Nawashukuru sana GST kwa kuw...

JITAHIDINI KUPINGA UKATILI KWA WATOTO

Image
Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma Bw. Ally Gugu amewaasa Maafisa Afya, Lishe , Elimu, Ustawi na Maendeleo ya Jamii wa Halmashauri zote 8 za Mkoa huo kutekeleza Mpango wa Taifa wa Malezi,Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto (MMMAM) ili kukabiliana na changamoto za ukatili kwa watoto wenye umri wa kati ya miaka 0-8.  Wito huo umetolewa leo Julai 28,2023 katika Kikao kazi cha kujadili namna ya kujenga uelewa na kutoa taarifa za utekelezaji za kazi zinazofanywa katika Halmashauri zote kwa robo nne ya mwaka na kujenga uelewa kuhusiana na utekelezaji wa programu hiyo iliyozinduliwa rasmi tarehe 21/09/2021 na kufikia maazimio ya utekelezaji wa majukumu waliyoazimia. Kikao hicho kimefanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Jengo la Mkapa Jijini Dodoma.  "Wataalamu wote mliopo hapa toka sekta zote 5, mfanye kazi kwa kushirikiana katika kutekeleza programu ya MMMAM kwakuwa mnahusika katika ulinzi na usalama wa mtoto mshirikiane ili kulinda tunu ya Taifa, Kila mmoja kuwa...

TANZANIA NI MOJA NA HAITAGAWANYIKA-RAIS SAMIA.

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt.Samia Suluhu Hassan amewataka Watanzania kuendelea kuenzi mashujaa kwa kudumisha amani na kusisitiza kuwa Tanzania ni moja na haitagawanyika. Rais Dkt.Samia amebainisha hayo leo Julai 25.2023 Jijini Dodoma katika Maadhimisho siku ya Kumbukumbu ya Mashujaa ambapo amesema ni muhimu kuenzi mashujaa kwa kudumisha amani ,Umoja na mshikamano. Aidha, Rais Dkt. Samia ameagiza mnara wa mashujaa unaoendelea kujengwa katika mji wa Serikali Mtumba katika utekelezaji wa agizo alilolitoa Siku ya Kumbukumbu ya Mashujaa 2022 ukamilike kwa wakati huku akiagiza Wizara ya Fedha kutoa fedha kwa wakati. Kwa upande wake Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe.Jenista Mhagama amesema mnara wa mashujaa wenye zaidi ya mita 100 utajengwa huku agizo la Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan la kujengwa mnara wa Mashujaa likitekelezwa. Halikadhalika, Mhagama ameipongeza Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kuto...