Posts

Showing posts from June, 2024

"UTUNZAJI MAZINGIRA NI SUALA LA KIIMANI KWANI NI AGIZO LA MUNGU" RC SENYAMULE

Image
 Wito umetolewa kwa waumini wa Madhehebu mbalimbali, kuzingatia utunzaji wa Mazingira kwa kutumia nishati Safi kwani ni moja kati ya maagizo ya Mungu. Hayo yamesemwa wakati wa kufunga Kongamano la Maombi ya toba ya urejesho wa thamani ya Afrika 2024. Kongamano hilo kubwa lililofanyika kwa siku tatu kwenye ukumbi wa Mwangata uliopo Barabara ya Singida Jijini Dodoma, limefungwa June 28, 2024 na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule na lilishirikisha wanamaombi na wachungaji kutoka nchi tano za Afika. "Mazingira ni Imani kwani Mungu ametuagiza tutunze Mazingira. Tuungane katika matumizi ya nishati Safi ili kulinda mazingira yetu yanayoweza kuathiri Dunia nzima. Kupitia Maombi haya, naona mabadiliko kwa Dodoma na Afrika kwa ujumla kwani suala hili limewakutanisha viongozi wetu wakubwa wa nchi mbalimbali" Amesema Mhe. Senyamule  Akisoma risala yake mbele ya mgeni rasmi, Askofu Daniel Kitua wa Kanisa la Talitha Cuni na Mratibu wa Kongamano, Maombi hayo yameleta mafanikio c...

WILAYA YA CHEMBA YAPATA BARAZA LA ARDHI TANGU KUANZISHWA KWAKE

Image
  Wananchi wa Wilaya ya Chemba wanakwenda kutatuliwa kero yao ya muda mrefu ya kukosekana kwa Baraza la ardhi la Wilaya ambalo hutumika kutatua migogoro mbalimbali ya ardhi inayojitokeza kila wakati kabla ya kufikishwa kwenye ngazi ya Mahakama. Hayo yamebainishwa leo June 28, 2024 na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary wakati akiwaapisha wajumbe wanne wa baraza hilo, hafla ambayo imefanyika kwenye ukumbi wa ofisi yake jengo la Mkapa Jijini Dodoma. “Tangu kuanzishwa kwa Wilaya ya Chemba 2012, wananchi wake wamekua wakisafiri umbali mrefu kwenda Kondoa kutafuta haki zao za ardhi. Sasa wamepata baraza lao na kufanya Dodoma kuwa na jumla ya mabaraza 6 hivyo, kero ya wananchi wa Chemba kutokua na Baraza la ardhi inakwenda kutatuliwa” Mhe. Senyamule Mbali na hilo, Mkuu wa Mkoa, amemtaka Katibu tawala Mkoa pamoja na Mwenyekiti wa Baraza la Ardhi Mkoa, kusimamia mchakato wa kuhakikisha Wilaya ya Chamwino nayo inapata baraza la ardhi na kukamilisha mabaraza yote saba ya Mkoa wa Dodoma kwan...

WENGE WA UHURU DODOMA KUPITIA MIRADI YENYE THAMANI ZAIDI YA SH.BILIONI 21.2

Image
Mwenge wa Uhuru Mkoani Dodoma unatarajiwa kupitia jumla ya miradi 56 yenye thamani ya Jumla  ya Shilingi Bilioni 21.2. Mwenge huo utakimbizwa kwa siku nane katika Halmashauri zote nane za Mkoa huo na utakimbia kwa Kilometa 1,484  . Taarifa hiyo imetolewa leo tarehe 27.06.2024 na  Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule wakati akipokea Mwenge wa Uhuru katika uwanja wa Mpira wa Kata ya Chipogoro kwenye Wilaya ya Wilaya ya Mpwapwa kutoka kwa mkuu wa Mkoa wa Iringa Mhe. Peter Serukamba. Mhe. Senyamule amesema Mwenge huo utakuwa chachu ya uzinduzi wa miradi mbalimbali ya kimaendeleo na kimkakati kwenye Mkoa wa Dodoma kwa maendeleo ya Wananchi na Taifa kwa ujumla. Katika hatua nyingine, Mhe. Senyamule ameeleza kuwa kwa sasa Mkoa  huo  unaendelea na uhamasishaji wa wananchi kuhakiki majina yao katika daftari la kudumu la mpiga kura sambamba na kuwahamasisha kujitokeza kupiga kura katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa pamoja na uchaguzi mkuu wa 2025. Akizungumzia ...

RC SENYAMULE AMESHIRIKI KILELE CHA MAADHIMISHO YA WIKI HYA UTUMISHI WA UMMA

Image
 Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule, ametembelea baadhi ya Mabanda yaliyoshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma na uzinduzi wa Mifumo ya Kidigitali iliyosanifiwa na kujengwa na Ofisi ya Rais Utumishi leo tarehe 23 Juni,2024. Kilele hicho kilifanyika kwenye viwanja vya Chinangali Park Jijini Dodoma. #dodomafahariyawatanzania  #keroyakowajibuwangu

RAS MMUYA AMESHIRIKI KILELE CHA MAADHIMISHO WIKI YA UTUMISHI WA UMMA

Image
 Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma Bw.Kaspar K.Mmuya ameshiriki  kwenye kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma na uzinduzi wa Mifumo ya Kidigitali iliyosanifiwa na kujengwa na Ofisi ya Rais Utumishi leo tarehe 23 Juni,2024. Kilele hicho kilifanyika kwenye viwanja vya Chinangali Park Jijini Dodoma. #dodomafahariyawatanzania #keroyakowajibuwangu

DODOMA YANG'ARA RIPOTI YA MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU WA HESABU ZA SERIKALI

Image
  Mkoa wa Dodoma umefanikiwa kupata hati safi katika ripoti ya Mkaguzi na Mdhibiti  na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwa hesabu zilizoishia Juni 30,2023. Akizungumza kwenye kikao cha Baraza la Madiwani Juni 19, 2024  Wilayani Chamwino Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule amezipongeza Halmashauri zote za Mkoa huo kwa juhudi zake katika kupunguza hoja za Mkaguzi na kupata hati safi. " Sasa hivi Mkoa wa Dodoma wote umepata hati safi ,tunategemea sasa ni mwendo wa hati safi kwa Halmashauri zote. kazi yetu kubwa ni kuendelea kupunguza zile hoja ndogo ndogo za Mkaguzi ili nazo ikiwezekana kama siyo kumaliza basi zipungue kwa kiwango kikubwa" Ameeleza Mhe. Senyamule  Kwa upande Wake Mkuu wa Wilaya ya Chamwino Mhe. Janeth Mayanja amewasihi Menejimenti ya Wilaya hiyo kumtumia vizuri mkaguzi wa ndani kila anapotoa taarifa za kila  robo ya Mwaka wa fedha ili kupunguza hoja kwa Mkaguzi Mkuu. Kadhalika Mhe.Senyamule, Katibu Tawala Mkoa Bw.Kaspar Mmuya kw...

BODABODA WATAKIWA KUCHUKUA TAHADHARI JUU YA ABIRIA WAO

Image
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule ametoa angalizo kwa  Maafisa usafirishaji wa Pikipiki (bodaboda)  kuchukua tahadhari juu ya abiria wanaowapakia kutokana kuibuka kwa matukio ya kihalifu yanayofanywa na watu wasiojulikana dhidi ya Maafisa hao siku za hivi karibuni. Rai hiyo imetolewa Juni 18, 2024 wakati wa muendelezo wa utekelezaji wa kauli mbiu "kero yako, wajibu wangu" kwenye mkutano wa hadhara na wananchi wa kijiji cha Bahi Sokoni katika Halmashauri ya Bahi wenye Lengo la  kusikiliza na kutatua kero zinazowakabili.  "Bodaboda tuendelee kufuata maelekezo ambayo tunapewa juu ya umuhimu wa sisi kuchukua tahadhari ili kuongeza usalama wetu kwa kuangalia abiria tunao wapakia. Kama unaona humuelewi, achana naye usimpakie ili kuondoka na adha za namna hii" Ameagiza Mhe. Senyamule  Kero hiyo, iliibuliwa na mmoja wa wakazi wa eneo hilo Bw. Andrew Laurent wakati wa mkutano huo ambapo amesema siku za hivi karibuni kumetokea matukio ya aina hiyo ambayo yame...