TANROADS WATAKIWA KUTAFUTA NJIA MBADALA KWA WANANCHI WAKATI WA UJENZI WA DARAJA LA MORENA

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule (katikati), akitoa maelekezo kwa Meneja wa TANROADS Mkoa kutafuta njia mbadala kwa wakazi wa Morena wanaohitaji huduma upande wa pili wa daraja kipindi hiki cha ujenzi wakati alipotembelea mradi huo Aprili 29, 2025 Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Mhe. Jabir Shekimweri amesema upanuzi wa daraja la Morena utamaliza changamoto ya mafuriko kwenye makazi ya watu kipindi cha mvua kubwa, changamoto za kiafya na magonjwa ya mlipuko wakati wa ziara fupi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma kukagua mradi huo Aprili 28, 2025. Meneja wa TANROADS Mkoa wa Dodoma Mhandisi Zuhura Amani, amewaahidi wananchi kuwa pamoja na kuzingatia ubora, wataendelea kumhimiza Mkandarasi kukamilisha kazi hiyo mapema ili wananchi waone matunda yake wakati wa ziara fupi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma kukagua mradi huo Aprili 28, 2025. Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule alipofanya ziara fupi ya kutembelea mradi wa upanuzi wa daraja la Morena litakalotatua kadhia ya ku...