Posts

Showing posts from February, 2023

DUWASA YAJIPAMBANUA UHAKIKA WA MAJI DODOMA

Image
Mamlaka ya maji safi na usafi wa Mazingira Mkoa wa Dodoma (DUWASA) inaendelea kufanikisha lengo la upatikanaji wa maji kwa asilimia 100 kwa Mkoa wa Dodoma kufuatia juhudi za Serikali ya awamu ya Sita. Hayo yamebainishwa wakati wa mfululizo wa vipindi maalumu vya kutangaza mafanikio ya Serikali kwa Taasisi za Umma vilivyoandaliwa na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma ambapo leo kimeangazia sekta ya maji. Akiwasilisha hotuba yake mbele ya wanahabari wakati wa utangulizi wa kipindi hicho, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule ameelezea miradi mbalimbali ya maji inayoendelea katika Mkoa na utekelezaji wake ndani ya kipindi hiki cha miaka miwili ya Serikali ya awamu ya sita. “Tunafahamu maji ni kila kitu katika maisha ya mwanadamu, maji ni Uhai. Katika Mkoa wa Dodoma, kumekuwa na Uendelezaji wa vyanzo vya maji (uchimbaji wa visima na ujenzi wa mabwawa) kwa kutumia vyanzo vikuu kama vile Uchimbaji wa visima   virefu 34, Ujenzi wa Mabwawa 2 ya maji, miradi 10 ya maji inayotumi...

SENYEMULE AHIMIZA BALOZI KUJENGA DODOMA

Image
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule amesema mpaka sasa Balozi tatu (3) za Uganda, Zimbambwe na Zambia zimeanza ujenzi wa majengo ya Balozi hizo Mkoani Dodoma. Ameyasema hayo leo tarehe 28/02/2023 mara baada ya kukutana na balozi wa Norway nchini Tanzania Bi. Elisabeth Jacobsen aliembatana na ujumbe wake katika ziara ya kikazi ya siku mbili ya kutembelea Mkoa wa Dodoma. Mhe. Senyamule amemshukuru Balozi wa Norway kwa kutembelea Dodoma, kuona fursa za uwekezaji na kuimarisha ushirikiano mzuri uliopo baina ya nchi hizi mbili pia hatua mbalimbali za utekelezaji wa miradi ya kimkakati katika kuifaharisha Dodoma. “Tunawakaribisha sana Dodoma, makao makuu ya nchi yetu, viwanja 67 vimetengwa kwa ajili ya ujenzi wa Ofisi na makazi ya balozi mbalimbali” Senyamule alisisitiza. Ameongeza kwa kusema kuwa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kukamilisha miradi mikubwa ya kimkakati ili Dodoma iweze kufunguka kimataifa...

DODOMA KUWA KITOVU CHA BIASHARA NCHIN

Image
Mkoa wa Dodoma umezindua Baraza la Biashara la Mkoa chini ya Mwenyekiti wake Mkuu wa Mkoa Mhe. Rosemary Senyamule kuzungumzia mikakati ya kuuinua Mkoa kiuchumi. Uzinduzi huo umeambatana na mawasilisho kutoka kwa wadau mbalimbali wa Biashara wakiwemo Baraza la Taifa la Biashara (TNBC), Baraza la wawekezaji na wadau wengine. Wakati wa hotuba yake ya ufunguzi wa mkutano huo, Mhe. Senyamule amesema; "Mhe. Rais Dkt Samia Suluhu Hassan, amepunguza sheria kandamizi kwa Wafanyabiashara, ameendelea kuleta wawekezaji kutoka nje na wanaingia kwa wingi nchini. Mkoa wa Dodoma tunataka tuwe na mchango Mkubwa kwenye Biashara hivyo ni matarajio yangu Baraza la Mkoa litakua bora na lenye utashi wa kipekee kwenye makao makuu ya nchi" Amesema Mhe Senyamule   Amewataka wajumbe wa Baraza hilo ngazi ya Wilaya kwenda kufanya vikao vya mabaraza pamoja na wale wa Halmashauri, Wakurugenzi wakafanye vivyo pia. Amewataka waende wakatenge maeneo ya uwekezaji ambayo yatavutia wageni watakapohita...

MAFANIKIO YA SERIKALI AWAMU YA SITA KATIKA HOSPITALI YA BENJAMINI MKAPA

Image
  Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule  amesema sekta ya afya imeendelea kuimarika na kupata mafanikio kutokana na kuongezeka kwa uwekezaji  katika  maeneo ya utoaji huduma na ujenzi wa miundombinu ya vituo vya kutolea huduma za Afya chini ya Rais Mhe Dkt. Samia Suluhu Hassan.   Akizungumza leo na Waandishi wa Habari kwenye Ukumbi wa Mkapa katika muendelezo wa Programu maalumu ya kuelezea mafanikio ya Serikali ya Awamu ya Sita ndani ya kipindi cha miaka miwili katika Hospital ya Benjamin Mkapa Dodoma Mhe. Senyamule amesema, “kumekuwa na kituo cha Damu Salama Kanda ya kati kilichopo Mkoani Dodoma, uwepo wa kituo hiki umerahisisha upatikanaji wa damu salama na mazao ya damu na hivyo kusaidia katika kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi na vifo vya Watoto wachanga ikiwa ni pamoja na kupunguza gharama ambazo zilikuwa zinatumika kusafirisha sampuli za damu Kwenda Maabara Kuu ya Taifa iliyopo Dar- es Salaam.”    Kwa upande wa Mkurugenzi Mtend...

SERIKALI YABORESHA MIUNDOMBINU YA BARABARA DODOMA

Image
                                                                     Sekta ya Miundombinu ya Barabara imeendelea kuimarika kupitia Wakala wa Barabara Vijijini na Mijini (TARURA) pamoja na TANROADS Mkoa wa Dodoma hasa katika kipindi cha miaka miwili ya Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwa na uboreshaji mkubwa wa barabara tofauti na kipindi cha nyuma. Hayo yamebainishwa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule alipokua akizungumza na waandishi wa habari kwenye ukumbi wa Mkapa katika muendelezo wa vipindi maalumu vya kutangaza Mafanikio Serikali ya Awamu ya sita kwa TARURA Mkoa wa Dodoma. Amesema kubwa kwa Mkoa wa Dodoma katika miundombinu ni ujenzi wa Barabara za mzunguko zenye urefu wa kilometa 112 ambapo LOT 1 inatoka Nala-Veyula-Mtumba-Ihumwa yenye urefu wa ...

TEKNOLOJIA YA MAKINGA MAJI YAZINDULIWA CHEMBA

Image
    Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule, katika hotuba iliyosomwa kwa niaba yake na Mkuu wa Wilaya ya Chemba Mhe. Gerald Mongela amezindua teknolojia mpya ya kuzuia mmomonyoko wa udongo  shambani inayojulikana kama makinga maji iliyobuniwa na TARI - Makutupora kwa kushirikiana na Lead Foundation katika siku ya Mkulima iliyofanyika katika Kijiji cha Mirambo kilichopo Kata ya Goima kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Chemba. Amesema mwongozo huo unatarajiwa kuwasaidia maafisa ugani pamoja na wakulima kudhibiti mmomonyoko shambani kwa kutumia makinga maji aina ya "fanya juu" na upandaji wa mimea pia kusaidia kuhifadhi maji kwa ajili ya umwagiliaji. Mhe Senyamule amesema "Uzalishaji wa mazao ya kilimo hutegemea utunzaji na uhifadhi bora wa udongo. Mkulima asipozingatia uhifadhi au utunzaji bora wa udongo wakati wa kutumia, huathiri ubora wake katika kuzalisha mazao shambani. Serikali kupitia Wizara ya Kilimo inafanya kazi na wadau mbalimbali katika kuimarisha sekta ya...

MAFANIKIO YA SERIKALIYA AWAMU YA SITA TRA

Image
  Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule amesema kumekuwa na ongezeko la ukusanyaji wa Mapato kutoka kwenye Halmashauri na kuwezesha maendeleo ndani ya Mkoa pia kupitia Mamlaka ya Mapato Tanzania – Mkoa wa Dodoma. kizungumza na Waandishi wa Habari leo Ofisi kwake kupitia programu ya kutangaza Mafanikio ya Awamu ya Sita katika Kipindi cha miaka miwili, Mhe. Senyamule amesema Mkoa wa Dodoma ulipangiwa Fedha za miradi ya maendeleo kupitia mapato ya ndani ambapo kumekuwa na ongezeko kutoka shilingi 32,1 hadi kufikia shilingi 35.0 Sawa na 9%.   Mhe. Senyamule amesema ongezeko hili limesaidia kuboresha huduma za jamii kwa kujenga vituo vya afya 4 zahanati 12 na vyumba vya madarasa 135 kupitia fedha za mapato ya ndani ya Halmashauri. “Tunaposema mapato yanaweza kuchangia ongezeko la huduma kwa wananchi ni pamoja na sura hii ambayo imeonyesha ,Pia mapato ya Halmashauri yanapoongezeka yameonyesha ongezeko la utoaji asilimia 10 kwa wananchi kwa makundi maalumu, Wanawake ...

JITIHADA NDO CHACHU YA MAFANIKIO "DKT MGANGA"

Image
  Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma Dkt. Fatuma Mganga, amefungua rasmi mkutano wa kutoa mrejesho wa kazi zilizofanyika katika awamu ya kwanza na ya pili ya utafiti wa kutumia mbinu za vinasaba katika ufuatiliaji wa malaria katika kikao kazi kilichofanyika katika ukumbi wa jengo la Mkapa. Akizungumza na Wajumbe walioshiriki kwenye kikao hicho, Dkt. Mganga amesema kazi ya uchakataji sampuli zilizokusanywa mwaka 2021 imekamilika na matokeo zaidi yalitolewa kwenye mkutano wa wadau uliofanyika mwezi mei 2022. “Jitihada zenu mnazoendelea nazo ndizo zitakazokuwa chachu ya kufanikisha kazi muhimu kwa nchi yetu mchango mkubwa unatolewa na wadau mbalimbali katika mapambano dhidi ya malaria, katika ngazi ya Mkoa na Halmashauri na katika vituo vya kutolea huduma za afya. Napenda kuzishukuru taasisi na mashirika yote yanayohusika na Utafiti na Taasisi ya Bill and Melinda Gates kwa kutoa ufadhii kwa ajili ya kutekeleza utafiti huu, nawaomba muongeze juhudi ili tuweze kutokomeza malaria” amesema Dkt ...