Posts

Showing posts from March, 2023

DODOMA YAJIPANGA KUINUA ELIMU

Image
                                         Idara ya Elimu Mkoa wa Dodoma imefikia maazimio kadhaa yenye lengo la kuinua sekta ya Elimu kwenye Mkoa wakati wa kikao kazi kilichowashirikisha wadau mbalimbali wa Elimu chini ya Mwenyekiti wake Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe Rosemary Senyamule na Katibu Tawala Mkoa Bw. Ally Gugu kwenye ukumbi wa TAG - Mipango Miongoni mwa maazimio hayo ni pamoja na kuanzishwa kwa mfuko wa Elimu kwenye kila Halmashauri ili kusaidia wanafunzi wenye mahitaji maalumu, utoaji wa chakula shuleni, kuthibiti utoro, hili, kila shule kuhakikisha kila mwanafunzi anamudu mada inayofundishwa, kila mwanafunzi anayemaliza Elimu ya Msingi anaanza masomo ya kujiandaa na kidato cha kwanza wiki mbili baada ya kufanya Mitihani. Mhe. Senyamule amesema matarajio ya Serikali ya awamu ya sita ni kuona maendeleo makubwa kwenye sekta ya Elimu kutokana na uwekezajj Mkubwa uliofanyika ...

WANAWAKE PEANENI FURSA- SENYAMULE

Image
Mkuu wa mkoa wa Dodoma mhe. Rosemary Senyamule amewataka wanawake kutumia fursa za makongamano mbalimbali ili kubadilishana maarifa na kuinuana kiuchumi bila kujali viwango vya vipato vyao na kupeana uzoefu wa Mambo mbalimbali.  Akizungumza na wanawake katika kongamano la jukwaa la wanawake la kuwainua kiuchumi mkoa lililofanyika katika ukumbi wa Cathedral jijini Dodoma leo tarehe 27/03/2023 -Senyamule Amesema wanawake wanapaswa kushirikiana na kupeana fursa mbalimbali pale zinapojitokeza. "Kila mtu ananafasi yake Kuna wafanyabiashara, wakulima yaani hapa tunakutana watu mbalimbali na wenye uzoefu tofauti tofauti kwaiyo Ukija maeneo Kama haya hakikisha unaondoka na kitu kipya na Cha ziada bila kujali vyeo vyenu, uwezo wenu kifedha na nyadhifa zenu mkiwa hapa endeleni kuwa kitu kimoja. "Tunazo fursa nyingi katika mkoa wetu natamani kuwaona wanawake mabilionea wengi kutoka Dodoma wametokea baada ya Mhe.Dkt.Samia Suluhu Hassan kutengeneza fursa nyingi kwaiyo Kama una fursa jikon...

JIKITENI KWENYE KILIMO CHA UMWAGILIAJI MHE .SENYAMULE AWAASA WAKAZI WA KONDOA

Image
  Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule amewataka wananchi wa Wilaya ya Kondoa kujikita katika kilimo Cha Umwagiliaji Ili kuondoa Janga la njaa, kujiongezea kipato na kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.   Ameyasema hayo leo tarehe 24/3/2023 kwa nyakati tofauti alipofanya ziara ya kikazi katika Wilaya ya Kondoa ambapo amekagua maendeleo ya ujenzi wa Jengo la Ofisi za Halmashauri, Ujenzi wa Hospitali ya Mji, Ujenzi wa Zahanati ya Ausia na kufanya Mkutano wa hadhara na Wananchi wa Kata ya Mnenia Wilaya ya Kondoa katika kiwanja cha Ofisi ya Kijiji Mnenia. "Mhe.Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Serikali ya Awamu ya Sita ameamua kuhimiza Kilimo cha umwagiliaji, kilimo cha uhakika ambacho mvua ikiisha unaendelea kumwagilia mpaka mazao yatakapo komaa. Kilimo ambacho maji yanakuwepo mwaka mzima unalima mara tatu au mara nne unavuna unalima tena na sisi mkoa wa Dodoma tumepata bahati kwa Wilaya tatu kuchimbiwa mabwawa na kuwekewa miundombinu ya umwagiliaji katika ...

ZINGATIENI USAFI AWAASA WANANCHI - SENYAMULE

Image
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule amewaomba wakazi wa Jiji la Dodoma kuzingatia usafi wa mazingira kila siku ili kuliweka Jiji katika Hali ya usafi ili kuendelea kuipa hadhi na mvuto wa makao Makuu na kuepuka magonjwa ya mlipuko. Senyamule ameyasema hayo alipokagua usafi wa mazingira katika Kata ya Chamwino Jijini humo uliofanywa na wananchi wa kata hiyo katika mazingira ya ofisi ya kata hiyo. "Nitoe wito kwa wanachamwino tuendelee kufanya usafi siku zote tusiwe tunangoja siku ya Jumamosi ili mji wetu uingie katika miji Bora sio tu Tanzania bali Duniani. Ninyi wananchi ndio mtakaofanya mji uwe nadhifu ili kufanikiwa katika hili inatakiwa tusitupe taka hovyo na kuzingatia kanuni zote za usafi na hifadhi ya mazingira ikiwa ni pamoja na kutoa kwa wakati taka zinazokusanywa katika miji na kupelekwa dampo" Senyamule amesisitiza "Mji wa Dodoma Umepewa baraka ya kuwa makao Makuu ni lazima kila kitu kiwe kwa mpangilio na kuzingatia viwango vinavyokubalika kati...

KILA KITU NI UTALI DODOMA MHE.ROSEMARY SENYAMULE

Image
  Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule amefanya ziara ya Utalii wa Ndani siku mbili  huku akiambatana na Wakuu wa Wilaya ya Chemba, Mpwapwa, Bahi, na Mwenyeji Kondoa  katika Pori la Akiba  Mkungunero  Lengo la ziara hiyo ni kuitangaza Mbuga ya Wanyama Mkungunero iliyopo wilaya ya kondoa yenye ukubwa kilomita za mraba 743  na  urefu wa takribani kilomita 240 Kutoka Dodoma Mjini  huku ikiwa na vivutio vingi ikiwa ni pamoja na wanyama wanne wakubwa kati ya watano. Mnyama anaekosekana katika pori hilo ni mmoja tu mnyama aina ya Faru. Pori hili linajivunia kuwa na wanyama Tembo, Pofu, Punda-milia wanapatikana kwa wingi na Makundi makubwa Kiupekee mnyama Swalatwiga (Generac) katika eneo lote la Masai's Tepe anapatika katika eneo la Mkungunero tu na Tandara wa kubwa na wadogo ambacho ni kitu cha upekee  sana ambacho ndicho kinawatambulisha. "Tuendelee kuyaambia makundi mbalimbali katika Mkoa wa Dodoma  ambayo yamekuwa yakipend...

HUDUMA ZIENDANE NA UFANISI

Image
  Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule amefungua mafunzo ya wawezeshaji wa Mkoa na Wilaya (ToTs) wa Moduli ya Mfumo wa Mshitishi ('PVS IMPLEMENTATION MANUAL') pamoja na Mfumo wa kieletroniki wa mshitiri (PVIMIS)  Amefungua mafunzo hayo leo yatakayo fanyika kwa siku tatu yanayo ongozwa na wakufunzi Mfamasia Kirti Joshi na Bw. Haji Kisesa Afisa Tehama huku washiriki wakiwa ni Katibu Tawala wa Mkoa Bw. Ally Gugu, Mganga Mkuu wa Mkoa Dkt. Best Magoma, Waganga Wakuu wa Wilaya Wafamasia, Watalaamu wa Maabara na Maafisa Tehama mafunzo yaliyofanyika katika ukumbi wa Mkuu wa Mkoa uliopo jengo la Mkapa.  "Mtazamo wa Serikali, nchi na dunia kwa ujumla unaenda kwenye Tehama kila kitu kinafanyika kwa njia rahisi na kuondokana na mfumo wa Manual maana yake tunapopata njia ya tehama maana yake tunaongeza ufanisi wa jambo tunalo lifanya kwaharaka, ubora, muda mfupi kwa nia ya kuongeza uwazi na uwajibikajii katika masuala ya fedha. Nendeni mkafanyie kazi mfumo huu, Mjifu...

MACHINGA DODOMA WAMPONGEZA DKT. SAMIA SULUHU HASSAN

Image
Kundi la Machinga Mkoa wa Dodoma leo tarehe 23/03/2023 wamefanya maandamano ya amani ya kumpongeza Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuwaheshimisha ndani ya kipindi cha miaka miwili ya uongozi wake. Akipokea maandamano hayo ya amani Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule amewapongeza wafanyabiashara wadogowadogo (Machinga) kwa kufanya kazi zao kwa utulivu na juhudi na kutambua mchango wa Rais Mama Samia Suluhu katika kipindi cha miaka miwili madarakani. "Ninayo furaha kwasababu kundi hili ambalo nchi yetu imekuwa ikihangaika nalo leo ni kundi ambalo linafuraha na amani na linafanya kazi zake kwa utulivu katika mkoa wetu niwapongeze kwa juhudi, Utashi, busara na hekima na ndio maana leo hii mmeona umuhimu wa kumpongeza Mhe. Rais wetu. "Jambo mlilofanya Leo linaipa fahari Dodoma kama ambavyo risala yenu inasema Mambo yaliyofanyika ni mengi mno na yataandikwa kwenye historia ya nchi ya Tanzania lakini huenda Afrika Masharik...